SOMO 1 – Kut. 3:1-8a, 13-15
Basi, Musa alikuwa akilichunga kunda la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpka mlima wa Mungu, hata Horebu. Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali.Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, Mimi niko ambaye niko, akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; Mimi niko amenituma kwenu. Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI – Zab. 103:1-4, 6-8, 11 (K) 8
(K) Bwana amejaa huruma na neema.Ee nafsi yangu umhimidi Bwana.Naam, vyote vilivyo ndani yanguVilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,Wala usizisahau fadhili zake zote.
(K)Akusamehe maovu yako yote,Akuponya magonywa yako yote,Aukomboa uhai wako na kaburi,Akutia taji ya fadhili na rehema.
(K)
Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki,Na hukumu kwa wote wanaoonewa.Alimjulisha Musa njia zake.Wana wa Israeli matendo yake. (K)
Bwana amejaa huruma na neema,Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi,Kadiri ileile rehema zake ni kuu kwa wamchao. (K)
SOMO 2 – 1 Kor. 10:1-6, 10-12
Ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe na Musa katika wingu na katika bahari; wote wakala chakula kile kile cha roho; wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.Wala msinung’unike kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO – Zab. 95:8
Msifanye migumu mioyo yenu; Lakini msikie sauti yake Bwana.
INJILI – Lk. 13:1-9
Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha Yesu habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichangaya damu yao na dhabihu zao. Akawajibu akawaambia.Je! Mwadahni ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo. Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamb awao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate. Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu? Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Nakuombea 🙏
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Endelea kuwa na imani!
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Neema na amani iwe nawe.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mungu ni mwema, wakati wote!
Rehema hushinda hukumu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Sifa kwa Bwana!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema zake hudumu milele
Baraka kwako na familia yako.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini katika mpango wake.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Tumaini ni nanga ya roho
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Imani inaweza kusogeza milima
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu akubariki!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Dumu katika Bwana.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mwamini Bwana; anajua njia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha