SOMO 1
Yer. 18-18-20
Waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yoyote.
Niangalie, Ee Bwana, ukasikilize sauti ya wanaoshindana nami. Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili nisema mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 31:4-5, 13-15 (K) 16
(K) Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako, Ee Bwana.
Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,
Maana Wewe ndiwe ngome yangu.
Mikononi mwako naiweka roho yangu;
Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli. (K)
Maana nimesikia masingizio ya wengi;
Hofu ziko pande zote.
Waliposhauriana juu yangu,
Walifanya hila wauondoe uhai wangu. (K)
Lakini mimi nakutumaini Wewe, Bwana,
Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.
Nyakati zangu zimo mikononi mwako;
Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia. (K)
SHANGILIO
Lk. 8:15
Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na unyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.
INJILI
Mt. 20:17-28
Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani; na njiani akawaambia, Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi nao watamhukumu afe; kisha watampeleka kwa Mataifa wapate kumdhihaki, na kumpiga mijeledi na kumsulibisha; na siku ya tatu atafufuka.
Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno. Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako. Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza. Akawaambia, Hakika mtakinywa kikombe change; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili. Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu yeyote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; na mtu yeyote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu; kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Rehema zake hudumu milele
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Tumaini ni nanga ya roho
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuwa na imani!
Baraka kwako na familia yako.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Katika imani, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Nakuombea 🙏
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Neema na amani iwe nawe.
Dumu katika Bwana.
Rehema hushinda hukumu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mwamini Bwana; anajua njia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Sifa kwa Bwana!