Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Featured Image

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia kipato chao na kulisha familia zao.
Wewe u Msimamizi wa wafanyakazi, tujalie kwamba pasiwepo kati yetu mtu asiye na ajira, na kwamba wale wote ambao wako tayari kufanya kazi waweze kuelekeza nguvu zao na uwezo wao katika kuwatumikia wanadamu wenzao na kujipatia kipato halali.


Wewe u Msimamizi wa familia, usiwaache wale wenye watoto wa kuwatunza na kuwalea wakose namna ya kufanya hivyo. Uwahurumie ndugu zetu waliokosa ajira na kugubikwa na umasikini kwa sababu ya magonjwa au mipango mibaya ya kijamii. Wasaidie viongozi wetu wa kisiasa na walioshika usukani katika nyanja mbalimbali za kiuzalishaji wavumbue suluhu mpya na za haki za jambo hili. Utujalie ili kila mmoja wetu apate kujipatia kipato halali na kufurahia fursa ya kushiriki kadri ya uwezo wake, katika maisha bora zaidi kwa wote. Utujalie ili wote tushiriki pamoja katika raslimali alizotujalia Mungu, na pia utujalie tuwe tayari daima kuwasaidia wale walio wahitaji kuliko sisi.
Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Elijah Mutua (Guest) on February 4, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Ruth Mtangi (Guest) on January 8, 2017

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Nancy Akumu (Guest) on December 20, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Agnes Njeri (Guest) on December 9, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Alice Jebet (Guest) on November 11, 2016

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Dorothy Nkya (Guest) on October 14, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Agnes Lowassa (Guest) on September 12, 2016

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Muslima (Guest) on July 14, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

Janet Mbithe (Guest) on July 11, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Hellen Nduta (Guest) on May 21, 2016

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Jackson Makori (Guest) on April 24, 2016

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Dorothy Mwakalindile (Guest) on March 18, 2016

Neema na amani iwe nawe.

Francis Njeru (Guest) on February 14, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Christopher Oloo (Guest) on January 25, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Andrew Mchome (Guest) on November 16, 2015

Mwamini Bwana; anajua njia

Ann Awino (Guest) on September 30, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

David Musyoka (Guest) on September 2, 2015

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Carol Nyakio (Guest) on July 6, 2015

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Isaac Kiptoo (Guest) on July 5, 2015

Rehema hushinda hukumu

Rose Waithera (Guest) on June 23, 2015

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Robert Ndunguru (Guest) on June 12, 2015

Tumaini ni nanga ya roho

Emily Chepngeno (Guest) on June 4, 2015

Sifa kwa Bwana!

Edwin Ndambuki (Guest) on April 28, 2015

Imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Read More
LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

SALA YA IMANI

SALA YA IMANI

Mungu wangu,

nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma;Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina y... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaok... Read More