Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Sababu, dalili na jinsi ya kujikinga na tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito

Featured Image

Hii ni hali inayowakumba mama wajawazito walio wengi. Inaweza kutokea kipindi chochote cha ujauzito ila mara nyingi hutokea katika umri wa mimba kuanzia miezi mitatu.

Kiungulia ni nini?

Kiungulia ni maumivu mithili ya moto yanayotokea kifuani sehemu ya katikat ya kifua. Maumivu haya hayana uhusiano na moyo.Yanatokea pale asidi ya kwenye tumbo inapopanda na kurudi kwenye koo la chakula.

Asidi hii ikiwa tumboni haisababishi madhara wala maumivu kwani inazalishwa muda wote na kuta za tumbo kumeng'enya chakula. Seli za kuta za tumbo haziathiriki na asidi hii ndio maana inapokuwa tumboni haileti shida yoyote.
Ila seli za kuta za koo la chakula haziwez kustahimili asidi hii ndiyo maana inapopanda kwenye koo la chakula unapata maumivu ya kiungulia.

Dalili ya kiungulia

Kiungulia mara nyingi hutokea wakati unakula au baada ya kula na kinaweza kuzidi makali wakati umelala.

Dalili ni kama, Kuhisi maumivu kama ya kuungua kwenye kifua au chembe moyopamoja na kujisikia radha ya uchachu mdomoni.

Saabu za kiungulia kwa wajawazito.

Sehemu mbali mbali za mwili hupata mabadiliko wakati wa ujauzito. Wakati wa ujauzito mwili hutengeneza kwa wingi hormone ya progesterone na relaxin ambazo huathiri mfumo wa chakula.

Progesterone hormone hii hufanya chakula kutembea na kufyonzwa kwa taratibu sana.
Relaxin hormone hufanya misuli laini ya mwili kulegea ikiwemo misuli inayobana sehemu ya juu ya tumbo (sphincter) inayozuia chakula au vitu vya tumboni visirudi kwenye koo la chakula .
Mabadiliko haya hufanya kuwa rahisi asidi na chakula vilivyomo tumboni kurudi kwenye koo la chakula na kusababisha kiungulia.

Vitu vingine vinavyoweza kusababisha kiungulia kwa mama mjauzito ni;

  1. Kula chakula kingi sana
  2. Vyakula vyenye viungo
  3. Vyakula vyenye mafuta mengi
  4. Matunda jamii ya limao na machungwa
  5. Chocolate
  6. Soda
  7. Kahawa
  8. Sigara
  9. Pombe
  10. Baadhi ya madawa
  11. Stress
  12. Uzito uliopitiliza.

Jinsi ya kujikinga na kiungulia kwa wajawazito.

  1. Kuwa na uzito unaowiana na urefu wako
  2. Epuka vyakula vinavyosababisha kiungulia kama nilivyoainisha hapo juu
  3. Epuka kula chakula kingi kwa wakati mmoja. Bali kula chakula kidogo kila baada ya muda.
  4. Kunywa maji ya kutosha. Angalau lita moja na zaidi kwa siku
  5. Epuka kuvaa nguo zinazobana sana tumbo na kiuno
  6. Usilale muda mfupi baada ya kula.
  7. Epuka kuwa na msongo wa mawazo /stress
  8. Onana na Daktari kupata ushauri wa dawa za kupunguza makali ya asidi hii ambazo ni salama kwa wajawazito
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Matumizi ya Mrehani (basil) kutibu presha ya kushuka

Matumizi ya Mrehani (basil) kutibu presha ya kushuka

Hii ni dawa nzuri ya kutibu shinikizo la chini la damu sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamin... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia maganda ya ndizi

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia maganda ya ndizi

Maganda ya ndizi ni dawa nyingine nzuri ya kuondoa chunusi. Unachohitaji ni kuwa tu na maganda ya... Read More

Faida na jinsi ya kutumia mbegu ya Parachichi kiafya

Faida na jinsi ya kutumia mbegu ya Parachichi kiafya

Leo nimekuletea matumizi ya mbegu ya parachichi yenyewe yaani ile inayokuwa katikati ya tunda la ... Read More

Faida za kunywa juisi ya ubuyu

Faida za kunywa juisi ya ubuyu

Mungu ameumba miti na mimea kwa ajili ya binadamu. Kila mti au mmea una makusudio yake. Mbuyu ni ... Read More

Madhara ya kunywa soda

Madhara ya kunywa soda

Tafiti zinasema kwamba mtu mmoja anayekunywa soda moja kwa siku, anakunywa zaidi ya galoni au dum... Read More

Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza

Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza

Vyakula hivyo ni;

  1. Maharage
  2. Nyanya
  3. Samaki
  4. Mboga za majani zenye... Read More
Jinsi msongo wa mawazo unavyoweza kukusababishia ugonjwa wa moyo

Jinsi msongo wa mawazo unavyoweza kukusababishia ugonjwa wa moyo

Kila mmoja wetu anaweza kuwa na sababu tofauti inayoweza kumsababishia msongo (stress). Sababu ku... Read More

Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Shelisheli lililokomaa huwa na uzito wa hadi kilo 6, ambapo mshelisheli unaweza kukua kwa urefu w... Read More

Jinsi ya kuongeza kiasi cha utokaji wa maziwa kwa kina mama wanaonyonyesha na kwa afya ya mtoto

Jinsi ya kuongeza kiasi cha utokaji wa maziwa kwa kina mama wanaonyonyesha na kwa afya ya mtoto

Maziwa ni chakula kikuu cha mtoto punde anapozaliwa. Mama anahitaji kuwa na Maziwa ya kutosha ili... Read More

Dalili za homa ya dengu (Dengue fever)

Dalili za homa ya dengu (Dengue fever)

Dengue ni moja kati ya homa kali inayodhoofisha na kuambatana na maumivu makali. Kwa sasa hakuna ... Read More

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Inasemwa kuwa “wewe ni kile unachokula” kwa kumaanisha kuwa mwonekano wetu na afya ya mwili n... Read More

Mambo ya msingi kujua kuhusu ugonjwa wa ngiri

Mambo ya msingi kujua kuhusu ugonjwa wa ngiri

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinaz... Read More