Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Ziara za kushtukiza zinachekesha sana

Featured Image

Mimi Nimecheka sana
πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

ZIARA ZA KUSHTUKIZAπŸ˜€πŸ˜€
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti, na msikilizaji mzuri wa redio, huwa naangalia luninga mara chache sana kama nikibahatika kupita mahala kuna luninga. Sasa wiki hii nimesikia mengi kuhusu hizi ziara za kushtukiza za viongozi wetu, nikaona hili ni jambo zuri tena linafaa kuigwa na sisi wananchi wapenda maendeleo. Nikaona nijipange na mimi nifanye ziara kadhaa za kushtukiza katika sehemu mbalimbali zinazonihusu.

Nikaona nianze na ziara ya kushtukiza pale shuleni kwa huyu mwanangu, maana kila siku anakunywa chai na kuondoka na daftari zake na mie sijawahi kwenda shuleni kwao toka nilipomuandikisha shule mwezi Januari. Nilifika shuleni na kumuona mwalimu mkuu, ambae alianza kutetemeka nilipomuambia kuwa nimekuja pale kwa ziara ya kustukiza, sijui alidhani mi ni mmoja wa Mawaziri wapya, maana nilimuona jasho linamtiririka ghafla. Akanikaribisha ofisi yake iliyokuwa na vitabu kila kona, na kuita waalimu wote na kunitambulisha kuwa ni kiongozi nimekuja kwenye ziara ya kustukiza.

Nilipojitambulisha kuwa ni mzazi, waalimu wote nikawaona waanza kupumua kwa raha. Nikawaambia kuwa mimi nina mwanafunzi pale na nilikuja ziara ya kustukiza kujua maendeleo yake. Baada ya mwalimu mkuu kusaka jina la mwanangu nae akanambia, β€œMzee huyu mtoto hajaja shule mwezi wa tatu sasa, tulijaribu kukutafuta ikashindikana, hatujui yu wapi” Jasho likaanza kunitoka mimi, yule mtoto kila asubuhi nampa nauli anaenda shule, na mara nyingi ananiomba michango kumbe hata shule haji. Niliondoka bila kuaga presha ikiwa juu.

Nikaona niende kwenye genge la mke wangu nae nikamfanyie ziara ya ghafla nimhadithie mambo ya mwanae, nilipofika pale nikakuta kuna mdada mwingine anauza genge. Nikamsalimu, na kumuuliza mwenye genge ntampataje, jibu lake lingeniua kama ningekuwa si mkakamavu, β€œMume wake kaja kumchukua na gari wameenda kununua shamba Bagamoyo”. Nikaondoka nimechanganyikiwa, nikajuwa hapa dawa yangu moja tu, nayo ni Sabrina, mtoto wa Kinyaturu pale ambapo nikipata maudhi huwa naenda kubembelezwa.

Nikatwanga mguu kwa Sabrina nae nikamfanyie ziara ya ghafla ili anipoze moyo. Nilipogonga mlango wa chumba chake akatoka mbaba wa miraba minne, akanisalimia kwa upole, β€œSalama kaka unasemaje?” Jibu likanitoka β€œSamahani mie nilimkopesha huyu dada wa chumba hiki vitenge, nilikuja kuuliza kama ameshapata hela yangu” Ziara za kushtukiza zinataka moyo wa chuma jamani

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Mariam (Guest) on February 21, 2017

πŸ˜‚ Ninahitaji kuihifadhi hii milele!

James Mduma (Guest) on February 4, 2017

Hii ni kali sana! πŸ˜‚πŸ€£

Irene Akoth (Guest) on February 4, 2017

πŸ˜„ Hii ni ubunifu wa hali ya juu!

Frank Macha (Guest) on January 27, 2017

Hii imenipa kicheko cha siku! πŸ˜‚πŸ˜†

Monica Nyalandu (Guest) on January 18, 2017

Ucheshi wenu ni wa hali ya juu sana! πŸ‘πŸ€£

John Mushi (Guest) on January 15, 2017

Napenda jinsi mnavyofikiria! πŸ€”πŸ˜†

Paul Ndomba (Guest) on January 11, 2017

Hii imenibamba sana! πŸ˜…πŸ€£

Mary Njeri (Guest) on December 3, 2016

Nimecheka kwa sauti! 🀣🀣

Josephine Nduta (Guest) on November 24, 2016

Hizi jokes zinabamba sana! πŸ˜†πŸ˜‚

Sarafina (Guest) on November 21, 2016

πŸ˜† Hiyo punchline!

Ruth Kibona (Guest) on November 12, 2016

Nimeipenda hii joke! πŸ˜„πŸ˜‚

Margaret Anyango (Guest) on October 26, 2016

Hizi jokes ni za ukweli! πŸ˜†πŸ‘

David Ochieng (Guest) on October 26, 2016

Kweli mna ucheshi wa hali ya juu sana! πŸ‘πŸ˜†

Michael Mboya (Guest) on October 3, 2016

Hii ni joke ya maana sana! πŸ˜‚πŸ‘Œ

David Chacha (Guest) on September 27, 2016

Hii ndio nilihitaji leo! Asante! 😜

Agnes Njeri (Guest) on September 15, 2016

😁 Hakika hii ni kichekesho changu kipya!

Esther Cheruiyot (Guest) on August 21, 2016

Nimependa hii! Endelea kuzileta! 😁

Anna Sumari (Guest) on July 25, 2016

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€£

Alice Mwikali (Guest) on July 15, 2016

Hii ni kali! Itaingia kwenye vipendwa vyangu! πŸ˜„

Agnes Sumaye (Guest) on July 10, 2016

Bado nacheka, hiyo ilikuwa nzuri sana! 🀣

Ann Wambui (Guest) on July 8, 2016

Hii imenifurahisha kweli! πŸ˜†πŸ˜‚

Stephen Amollo (Guest) on July 8, 2016

πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜†πŸ‘

Bernard Oduor (Guest) on July 3, 2016

Mna talent ya jokes! πŸ‘πŸ˜‚

Jane Muthoni (Guest) on June 26, 2016

Hii imenikumbusha kicheko cha zamani! πŸ˜‚πŸ˜…

Edward Chepkoech (Guest) on June 22, 2016

πŸ˜…πŸ˜‚πŸ‘ŒπŸ˜Š

Chum (Guest) on May 19, 2016

πŸ˜‚ Ninashiriki mara moja!

Peter Tibaijuka (Guest) on May 6, 2016

Kweli mna ucheshi wa kipekee! πŸ˜‚πŸ€£

Francis Njeru (Guest) on May 4, 2016

πŸ˜„ Umenishika vizuri!

Richard Mulwa (Guest) on April 24, 2016

Hii ni kali kabisa! Siwezi kushiba! πŸ˜‚

Paul Ndomba (Guest) on April 23, 2016

Brilliant! Muda wake ulikuwa kamili! ⏰

Isaac Kiptoo (Guest) on April 22, 2016

πŸ˜‚ Sijacheka hivi kwa muda mrefu sana!

Anthony Kariuki (Guest) on March 31, 2016

Hii ni ya maana sana! πŸ˜‚πŸ‘Œ

Jacob Kiplangat (Guest) on February 29, 2016

Hii imenipa furaha ya siku! πŸ˜†πŸ˜‚

Edwin Ndambuki (Guest) on February 24, 2016

Siwezi kuamini jinsi hii ni kichekesho! πŸ˜‚

Mary Njeri (Guest) on February 5, 2016

Huyu mtu ni mcheshi sana! πŸ˜‚πŸ˜‚

Zakaria (Guest) on February 3, 2016

Asante Ackyshine

Amir (Guest) on January 23, 2016

Hii kichekesho inastahili tuzo! πŸ†

Chum (Guest) on January 11, 2016

πŸ˜† Bado nacheka, siwezi kuacha!

Lucy Wangui (Guest) on January 1, 2016

Haha, mbavu zangu zinauma kwa kucheka sana! 🀣

Sarah Mbise (Guest) on December 30, 2015

πŸ˜„ Dhahabu ya vichekesho!

Isaac Kiptoo (Guest) on December 9, 2015

Huyu alikuwa na point! πŸ˜‚πŸ‘Œ

Lucy Mushi (Guest) on November 27, 2015

Ucheshi wenu ni wa hali ya juu sana! πŸ‘πŸ˜‚

Mhina (Guest) on November 7, 2015

πŸ˜‚ Hii ni kali sana!

Lydia Wanyama (Guest) on November 7, 2015

Sikutarajia hiyo punchlineβ€”kichekesho! 🀣

Hellen Nduta (Guest) on November 2, 2015

Ucheshi wenu unanifurahisha kila siku! πŸ˜†πŸ˜„

Elizabeth Mrope (Guest) on November 2, 2015

Hii imenipa furaha ya siku! πŸ˜†πŸ‘Œ

Azima (Guest) on September 10, 2015

πŸ˜‚ Nacheka hadi nalia!

Alice Mrema (Guest) on August 30, 2015

Hii imenikuna hadi nina furaha sana! πŸ˜ŠπŸ˜‚

Joseph Njoroge (Guest) on August 17, 2015

Nimecheka hadi nimesahau shida! πŸ€£πŸ˜†

Andrew Mchome (Guest) on August 5, 2015

πŸ˜„ Siwezi hata kupumua, ni kichekesho sana!

Nora Kidata (Guest) on July 31, 2015

Haha, hii ni ya kuhifadhi! πŸ“Œ

Philip Nyaga (Guest) on July 15, 2015

πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜†

Charles Mrope (Guest) on June 22, 2015

Hii ni joke ya kipekee sana! πŸ˜ŠπŸ‘

Francis Mrope (Guest) on June 12, 2015

Hii ni joke ya kipekee sana! πŸ˜‚πŸ‘

Rose Mwinuka (Guest) on June 12, 2015

πŸ˜„ Sikutarajia hiyo ikitokea!

Tambwe (Guest) on May 19, 2015

πŸ˜‚ Siwezi kuacha kucheka!

Related Posts

Kapresha kakiamua kuja kanakujaga tuu, cheki kilichompata huyu mme wa mtu mpenda michepuko

Kapresha kakiamua kuja kanakujaga tuu, cheki kilichompata huyu mme wa mtu mpenda michepuko

Kimchepuko chako kinakuandikia meseji kama hii…

…Samahani baby kama unavyojua nimeokoka... Read More

Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza

Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza

Zuzu: Mambo Anna!
Anna: Poa!
Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyeshe…
Anna: Kitu gan?... Read More

Bongo usanii mwingi!!!

Bongo usanii mwingi!!!

BONGO USANII UMEZIDI DAAH!!

…yani nakupeleka dinner unakula sana vipaja vya kuku na chips... Read More

Kali ya mwaka iliyotokea Benki Baada ya wezi kuiba

Kali ya mwaka iliyotokea Benki Baada ya wezi kuiba

Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana

..unaenda kuoga, unakumbuka k... Read More

Angalia huyu baba alichowafanya mtoto wake wa kike na boyfriend wake

Angalia huyu baba alichowafanya mtoto wake wa kike na boyfriend wake

BABA OYEEEEEEπŸ’ͺπŸ’ͺ
Soma hii…

Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mar... Read More

Alichofanya mke baada ya mme wake kupenda kumchunga sana

Alichofanya mke baada ya mme wake kupenda kumchunga sana

Alifanya hivi;
Siku ya kwanza

MUME: Halooo vipi mke wangu salama weye... Read More

Unakumbuka hizi enzi za utoto?

Unakumbuka hizi enzi za utoto?

Kitambo tukiwa watoto ulikuwa unaitwa uje ule kwa lugha tofauti kulingana na chakula kilichopikwa... Read More

Angalia hawa wadada walivyoumbuliwa, Huyu kasuku jeuri kweli

Angalia hawa wadada walivyoumbuliwa, Huyu kasuku jeuri kweli

Kasuku alisimama mlango wa kuingia supermarket wakapita wanawake watatu akasema nyeupe, nyekundu, ki... Read More
Angalia hawa kina mama, ni shida..!

Angalia hawa kina mama, ni shida..!

Mama mdaku alishangaa kila siku mchungaji anaingia nyumba ya jirani yake ambaye hana mume, akawa... Read More

Askari na yeye kumbe muoga, cheki anachomjibu afande

Askari na yeye kumbe muoga, cheki anachomjibu afande

Askari wametumwa nyumba iliyokuwa kuna ugomvi wakafika wakatakiwa kuripoti ... Read More

Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake

Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake

Mtoto alimwuuliza baba yake,
Mtoto: Baba unaweza kumwachia hilo gari lako house boy/girl aka... Read More

Hii ya mamba na kiboko kali, Wewe unaonaje?

Hii ya mamba na kiboko kali, Wewe unaonaje?

Eti kati ya MAMBA na KIBOKO nani kiboko???😜😜😜😜... Read More