Updated at: 2023-04-29 22:53:38 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Karibuni tuangalie aina hizi 10 za ndoa.
1. NDOA YA MKEKA
Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu. Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika mwaka mmoja tu,baada ya wanandoa kugundua hawakuwa wakipendana!
2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)
Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati mume18 mke 16.Huvunjika baada ya miaka 3 au 4 ya ndoa.
4. NDOA YA MAONYESHO
Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha barabarani.Ila ndani hazina utii.Hupigana kila wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa zinazoongoza kwa kuchepuka!
5. NDOA YA UHAMISHO.
Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa kijijini ahamie mjini.Mahari utoa anaetaka kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini kwenda kijijini.
6. NDOA YA MIMBA.
Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na kufikisha mwaka 1.
7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)
Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa hizi hulea watoto wasio wao.
8. NDOA YA KWASABABU.
Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au kaolewa.Huwa hazina utii wala upendo dhati. Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.
9. NDOA YA UPENDO.
Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya kagera.Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.
10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta wanakufa wao kwanza. Kuwa mwangalifu!
Updated at: 2024-05-25 17:09:54 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jamaa: Mambo honey, upo ok? Mrembo: Sipo ok my dear Jamaa: Una tatizo gani baby? Mrembo: Nimetoka hospitali kupima, nna mimba. Jamaa: Weeh usiniletee balaa hiyo mimba imeingiaje wakati huwa tunatumia kinga? Mrembo Kwani nani kakwambia mimba ni yako, hebu tuliza mshono huo.
Updated at: 2024-05-25 17:48:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Tukiwa kanisani mdada alikuwa amelala , akaamka akasikia Pastor anasema " SIMAMA" Yule dada akasimama akashangaaa kanisa zima linamtizima kwa mshangao akiwemo mumewe, akaangalia kanisa zima akashtuka kujiona yeye peke yake ndiye aliesimama Pastor akaendelea vizur endelea kusimama, tumepata mmoja hadi sasa aliyesimama narudia kwa mara ya mwisho kama hujasikia vizuri " kama wew umewahi kumsaliti au bado unasaliti ndoa yako SIMAMA" Binti akazimia
Updated at: 2024-05-25 17:58:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndio hizi sasa
1.Hicho ndicho chuo chako usiwe na chuo kingine ila hicho. 2.Usilitaje bure jna la chuo chako mana utawaumiza wengine. 3.Ikumbuke cku uliyochaguliwa na kuiheshimu. 4.Waheshimu tcu, bodi ya mkopo na uongoz wa chuo ili upate kuendelea kuwepo chuon. 5.Usisapu 6.Usidisko 7.Usitumie mkopo ovyo. 8.Usitaman chuo cha mwenzio 9.Usitamani fakat ya mwenzio 10. Usitaman bumu lake wala chochote alichonacho. hahaha chezea chuo weye!
Updated at: 2023-04-29 22:52:35 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Baba- : Halloo mke wangu.. yaani ni shida sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi dar haiwezekani MAMA:- Mme wangu morogoro ulienda bila kuniaga! ? BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia MAMA:- kha! Sasa watoto nani atawaangalia BABA:- Unasemaje! We uko wapi kwan MAMA:- Niko bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi. BABA:- Unasemaje we mwanamke.. nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15 Baada ya dk 15 Baba kafika nyumban. MAMA:- Haya umefkaje kutoka morogoro? BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe..
Jamaa kaingia Bar; Jamaa: Muhudumu, nipe kinywaji na mpe kila mtu humu ndani kinywaji, maana wakati napata kinywaji lazima kila mtu apate kinywaji. Haraka sana muhudumu akagawa vinywaji,
Updated at: 2023-04-29 22:53:32 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Jamaa kaingia Bar; Jamaa: Muhudumu, nipe kinywaji na mpe kila mtu humu ndani kinywaji, maana wakati napata kinywaji lazima kila mtu apate kinywaji. Haraka sana muhudumu akagawa vinywaji,
Jamaa: Muhudumu nipe supu na kila mtu humu ndani mpe supu maana ninapokunywa supu kila mtu lazima anywe supu. Watu wakapewa supu tena safari hii wakapiga makofi. Jamaa: Muhudumu nipe bili, na kila mtu humu ndani mpe bili maana wakati nalipa bili yangu kila mtu lazima alipe yake. Zogo lilianzia hapo…….
Updated at: 2024-05-25 17:08:18 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Sitasahau mwaka ule ambapo nilipeleka barua ya maombi yangu ya kazi kwenye kampuni moja maarufu. Wakati nasubiri majibu siku moja nikaenda kwa mama ntilie kununua maandazi akanifungia vizuri, kufika nyumbani hamu yote ya maandazi iliniishia pale nilipogundua karatasi iliyofungiwa maandazi ni barua yangu ya kuombea kazi😂😂