Haya ndiyo madhara ya kutowapeleka watoto kanisani ⛪
Updated at: 2024-05-25 17:08:53 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MTOTO aliibiwa yeboyebo KANISANI akawa analia sana kwa uchungu mpaka MCHUNGAJI akamwambia usilie mwachie MUNGU. MTOTO akajibu Mungu hazimtoshi zile yebo ni ndogo! Usicheke,
Huu ni Mtihani Tuwapeleke Watoto KANISANI Wamjue MUNGU.
Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo
Updated at: 2024-05-25 17:14:16 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
😁😁😁😁 .. TABU KUDATE NA MADEMU WA CHUO Demu ; Baby Safari Hii Nataka Pale Hostel Niwafunike Mashoga Zangu Wote. Jamaa ; Poa Sweetie Ondoa Shaka Nitakununulia #Turubai Utawafunika Wote…!!! Demu: Mxiuuuuuuuu Lione Sura Kama Goti La mbuzi Na Namba yangu futa Nakublock Mpaka Sanduku la posta…!!!
Updated at: 2024-05-25 17:49:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Babu: Mjukuu wangu ngoja nikusimulie hadithi ya mimi babu yako kwenye vita ya kagera Mjukuu: Niambie babu Babu: Kwenye vita ya kagera tulienda sehemu tukakamatwa wote askari na maadui wakatuambia chagueni kuuliwa au kubakwa. Mjukuu: Sasa babu wewe ulichagua nn? Babu: Niliuliwa!!!
Cheki wanachokisema vichaa baada ya kuona ndege inapita angani
Updated at: 2024-05-25 18:01:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vichaa wawili walikuwa wamekaa sehemu ghafla ikapita ndege angani kichaa mmoja akasema ndege ile hitakua imembeba rais kichaa mwenzake akajibu hapana ile imebeba wazungu kama ingekuwa imembeba rais ungeona mapikipiki mbele
Huyu bwana leo kapatikana, Jamani nyodo nyingine mbaya
Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja.
Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.
Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka.
Updated at: 2023-04-29 22:52:17 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja. Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.
Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka. Wakati mdada alipokaribia Rwegashora alimkaribisha kwa ishara maana alijifanya yupo busy na kuongea na simu ya umuhimu. Wakati anaongea na simu akisikika akisema No, No, No….. Absolutely No. Wajuulishe hao lay person wa New York kua siwezi kushuhulika na kesi ambayo itanilipa chini ya 50 million. Mimi ni profesional lawyer and im crossing the border to sarve international community.
Aka pose kidogo na akanywa maji kisha akaendelea….. Naweza kuanza kukusanya primary evidence next weak but tell them watume kwanza ten million kwa kuanza… Hahahahaha you dont know my Account Mr Roger. Ok waambie watume kwenye Account ileile walionitumia million 100 last month…
Aka pose tena akameza fundo la maji na kurekebisha tai yake kisha akaendelea… Ok usisahau kumueleza muendesha mashtaka mkuu wa marekani kua nitakuja New York mwezi ujao maana nitapita kwanza Amsterdam kuwasilisha utetezi wa yule mteja wangu mholanzi kisha nitaenda Tokyo kulipia ile gari yangu niloagiza.
Wakati anaongea hayo yote yule mdada alikua ametulia na anamuangalia Bwana Rwegashora anavyojizunguusha kwenye kiti chake huku akiongea kwa tambo kwenye ile simu ya TTCL. Baada ya kumaliza kuongea na simu Bwana Rwegashora aliweka mkono wa simu yake ya TTCL chini kisha akamgeukia mdada mrembo.
Samahan sana kwa kukupotezea muda wako unajua tena kazi zetu zinaumiza kichwa sana kama unavyoona mwenyewe yaani niko busy sana ninapokea simu sana mpaka nimechoka na simu nyingi ni za wateja wa njee ya nchi.
Anyway nikusaidie nn? Mdada akajibu mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya TTCL nimekuja kuunganisha line yako ya simu kwani haipo hewani tangu wiki iliyopita…!!!
Updated at: 2024-05-25 16:55:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ukioa mke asiyesoma hata hili unaweza kufanya
KUOA MKE AMBAE HAJASOMA RAHA SANA LEO NIMEMUAMBIA MWEZI HUU HATUTOLIPWA MSHAHARA KWAKUA HAUNA TR 30 KAENDA KUNGALIA KARENDA KARUDI ANANIAMBIA HAMNA SHIDA MME WANGU TUTAVUMILIA TU
Updated at: 2024-05-25 17:11:24 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna siku nilichalala kipesa nikaamua kuomba dem wangu aniazime 10,000/= akanipa. Baada ya siku mbili nikapata pesa zaidi ya laki nne hivi, nikaamua kumpa 100,000/= mpenzi wangu bila yeye kuniomba. Baada ya siku 3 akaja kuniambia:- "Bae, ile 10,000/- niliyokuazima mwenyewe amekuja kunidai, so kama unayo naomba unipe nimrudishie maana ananisumbua leo siku ya 3." SAA HIZI NIPO ZANGU SINGLE NATAFUTA DEM MWINGINE
Updated at: 2024-05-25 18:10:22 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mama mdaku alishangaa kila siku mchungaji anaingia nyumba ya jirani yake ambaye hana mume, akawa anajiuliza anakwenda kufanya nini? Uzalendo ukamshinda akamuuliza "Mwenzangu, mbona kila siku mchungaji anakuja kwako, vipi anakuja kukuombea?" Akajibiwa "Nyoo, umbea tu! Mbona kwako kila siku anakuja mwanajeshi kuna vita! chefuuuu 😳😳😳😳😳