Je,mwanaume akitoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga shahawa anaweza kuambukizwa yeye au mwanamke na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?
Updated at: 2024-05-25 16:22:31 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndiyo, hata akitoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga mbegu anaweza akaambukizwa Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Ni hatari kwa mwanamke na pia kwa mwanaume, kwa sababu vijidudu vimo ndani ya majimaji ukeni na uumeni. Hasa kama mmoja kati ya wapenzi ana vidonda au michubuko midogo sehemu za siri, Virusi vya UKIMWI. huingia kwa urahisi.
Kutoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga shahawa siyo njia salama ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.
Updated at: 2024-05-25 16:24:26 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna matatizo na magonjwa mengi na ya aina mbalimbali unayoweza kuyapata kutokana na utuvaji wa sigara. Kiungo rahisi kuathirika ni mapafu. Baada ya kuvuta huo moshi, kaboni na tindikali iliyomo kwenye tumbaku huishia kwenye mapafu. Malimbikizo haya ya kaboni na tindikali husababisha ugumu katika kupumua na kusabisha usaha kwenye mapafu. Matatizo haya ya mapafu humfanya mvutaji awe mwepesi kupata maambukizo mengine. Hii inaweza ikawa kikohozi sugu na pia inaweza kusababisha nimonia (kichomi) pamoja na kifua kikuu na sarakani. Nikotini vilevile ni mbaya kwa tumbo. Husababisha kupoteza hamu ya kula na maumivu katika sehemu za chini ya tumbo.
Unaweza ukaona kwamba wavutaji wakubwa wa sigara wakawa na meno meusi au machafu. Hii ni kwa sababu kaboni imejilimbikiza juu ya meno, na hivyo kubadilika kwa rangi. Watu wanaovuta mara kwa mara hutoa harufu mbaya mdomoni na hupata matatizo ya ngozi.
Updated at: 2024-05-25 16:22:18 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Hakuna jibu la ujumla kwa swali hili, kwa sababu tiba ya ugumba inategemea chanzo maalum cha ugumba huo kwa mhusika. Kuna matatizo ya ugumba ambayo yanaweza kutibiwa, lakini mara nyingi ni vigumu au hata haiwezekani kumtibu mwanaume au mwanamke mgumba. Kwanza kabisa, lazima daktari atafute sababu za ugumba kwa kufanya uchunguzi wa kitaalamu kwa mwanamke na mwanaume. Baada ya uchunguzi daktari anaweza akawashauri kuhusu uwezekano wa kuwatibu. Mara nyingine tiba ni rahisi, lakini matatizo mengine ni mazito na ni vigumu au haiwezekani kuyatibu.
Updated at: 2024-05-25 16:24:18 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mboni katika macho ya Albino haina pigimenti ya rangi. Kwa hiyo, ni rahisi macho yao kuathiriwa na mwanga. Kwani mboni ndiyo inayolinda jicho la ndani lisipatwe na mwanga mkali. Vilevile kama mboni inavyolinda jicho dhidi ya mionzi ya jua, inakuwa vigumu kuona kwa usahihi utofauti katika picha. Kwa hiyo uwezo wa kuona unatiwa mawingu mawingu. Hivyo basi, ni muhimu sana kukwepa inavyowezekana mionzi ya jua na kulinda macho kwa kuvaa miwani ya jua.
Albino mara nyingi hawaoni vizuri, na hii i n a t o f a u t i a n a k w a m m o j a hadi mwingine. Inawezekana ni kutoona mbali, kutoona karibu au kuona mawingumawingu (ukungu). Matatizo haya hutofautiana katika Albino. Ukweli ni kuwa Albino anaweza kushiriki katika michezo mbalimbali, baadhi wanaweza kuendesha magari na wengi wanaweza kusoma maandishi ya kawaida.
Je, mwanamke anaweza kufikia mshindo (kufika kileleni)?
Updated at: 2024-05-25 16:22:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndiyo, mwanamke anaweza kufikia mshindo wakati wa kujamiiana. Dalili ya mwanamke kufikia mshindo katika kujamiiana ni ile hali ya pekee ya kujisikia vizuri kimwili. Tofauti na mwanaume, anapofikia mshindo mwanamke hakojoi kitu chochote.
Kwa kawaida mwanaume anakojoa manii wakati wa kujamii ana anapofikia mshindo. Kwa sababu dalili hii ni rahisi kuona baadhi ya watu wanadhani kwamba ni wanaume tu wanaofikia mshindo wakati wa kujamii ana. Lakini hii siyo kweli. Mwanamke pia hufikia mshindo, ingawa siyo rahisi kuuona.
Je, kuna wataalamu Tanzania wanaowasaidia watu wenye matatizo ya dawa za kulevya?
Updated at: 2024-05-25 16:22:34 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndiyo. Kuna mashirika yasiyo ya kiserikali (AZISE) yanayotoa ushauri nasaha kwa watumiaji wa dawa za kulevya. Katika AZISE hizi kuna wataalamu wenye kusikiliza na kujaribu kutafuta ufumbuzi wa matatizo yako. Kama mtu anategemea dawa za kulevya au anahitaji msaada wa kitaalamu, basi kuna vituo vya kuwasaidia kwenye hospitali za serikali,
Watu wanaamini kuwa Albino wana joto katika mapenzi kuliko watu weusi, Je, hiyo ni kweli?
Updated at: 2024-05-25 16:24:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Hii siyo kweli, tofauti baina ya Albino na mtu a s i ekuwa na ualbino i m e e l e z w a hapo mwanzoni ambapo tofauti ipo tu kwenye muonekano wa rangi ya ngozi, nywele n a macho. Mifumo yao yote mingine ya mwili iko sawa na watu wasio na ualbino. Watu wanaweza tu kuanzisha uvumi kama huo popote pale. Ipo pia mifano kama: Wajerumani wanaamini kuwa Wafaransa wana joto katika mapenzi, Wazungu pia huamini kuwa Waafrika wana joto n.k. Hizo ni hisia tu na siyo ukweli. Katika jamii wapo watu ambao wanapenda kufanya ngono sana, wapo wa wastani na wapo wale ambao hawajisikii msukumo wa kujamiiana. Uvumi huu unatokana na mawazo ya kifikra na siyo ukweli halisi.
Updated at: 2024-05-25 16:24:28 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Si kweli. Pombe haiongezi damu, vitamini wala nguvu. Ukweli ni kwamba unywaji pombe kupita kiasi huvuruga ufyonzaji wa vitamini na madini kutoka kwenye chakula kuingia mwilini.
Vitamini ni muhimu kwa kuimarisha kinga ya mwili ambayo inasaidia kujikinga na magonjwa, pamoja na maradhi kama UKIMWI. Kwa hivyo, unatakiwa uhakikishe unakula matunda na mboga za majani kwa sababu vinakuongezea vitamini.
Updated at: 2024-05-25 16:22:03 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mapenzi salama ni yale yanayofanyika bila wasiwasi wa kupata mimba zisizotarajiwa, magonjwa ya zinaa pamoja na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Mapenzi salama yanaweza kuwa ni pamoja na kumaliza hamu bila ya kujamiiana au kuchukua tahadhari kwa maana ya kutumia kondomu wakati wa kujamiiana.
Kumaliza hamu bila ya kujamiiana ni pamoja na kupiga busu, kukumbatiana, na kupiga punyeto. Vyote hivyo ni vitendo salama kabisa. Kama utajamiiana (kwa maana uume unaingizwa ukeni), ni lazima uhakikishe kuchukua tahadhari muhimu za kinga. Moja ya tahadhari inaweza kuwa wote ni waaminifu kabisa, lakini jambo hili linahitaji nyie wote wawili kuwa waaminifu na kuwa wote muwe mmepima virusi vya UKIMWI na pia msiwe mmefanya ngono hapo kabla (hamkuwa na uhusiano wa kimwili na mtu yeyote kabla. Tahadhari nyingine ni kutumia kondomu. Kondomu inazuia mimba pamoja na magonjwa ya zinaa na uambukizi wa Virusi vya UKIMWI.
Je, Tanzania kuna wataalamu wanaosaidia watu wenye matatizo ya ulevi wa kupindukia?
Updated at: 2024-05-25 16:24:23 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndiyo. Hapa Tanzania kuna kitengo maalumu kinachojishughulisha na masuala ya akili. Wataalamu mbalimbali hufanya kazi pamoja kama vile matibabu ya magonjwa ya akili na wanasaikolojia. Wanaustawi wa jamii ambao wana mbinu za kuelewa kiwango cha unywaji pombe katika jamii kulingana na tamaduni mbalimbali ambao pia wana utaalamu wa masuala ya utoaji ushauri, wanaweza kushirikiana na wataalamu wa afya ambao hufanya kazi hospitalini na kwenye jamii.