Jambazi mmoja aliingia kanisani na bunduki akapiga risasi juu ya bati akasema "asiyempenda YESU atoke nje" wakatoka wote ispokuwa Mchungaji na Wazee wawili.
Updated at: 2024-05-25 18:07:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jambazi mmoja aliingia kanisani na bunduki akapiga risasi juu ya bati akasema "asiyempenda YESU atoke nje" wakatoka wote ispokuwa Mchungaji na Wazee wawili.
Jambazi likamwambia Mchungaji "unaweza kuendelea na ibada, nilikuwa nakuondolea wanafiki", Mchungaji akasema "ungewaacha kwanza nichukue sadaka…!
Padri Akimbia wakati wa kuungamisha, chanzo ni hiki
Padri alikuwa amekaa katika confession booth kanisani
peke yake.
Mara kukaingia jamaa mmoja akapiga magoti upande wa
pili, akafanya ishara ya msalaba kisha akaanza kuungama
{confess}
"Padri nimekuja kuungama dhambi zangu, leo nimefanya
dhambi kubwa sana."
Padri, "Endelea…"
Updated at: 2023-04-29 22:53:14 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Padri alikuwa amekaa katika confession booth kanisani peke yake. Mara kukaingia jamaa mmoja akapiga magoti upande wa pili, akafanya ishara ya msalaba kisha akaanza kuungama {confess} "Padri nimekuja kuungama dhambi zangu, leo nimefanya dhambi kubwa sana." Padri, "Endelea…"
"Bosi wangu aliniita nyumbani kwake, akaniambia amegundua nimeiba shilingi millioni 100 kazini. Akasema nisipozitoa atanipeleka polisi, sa kwa ukweli mi naogopa kufungwa. Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu,nikatoa bastola nikamuua….. Yesu atanisamehe?"
Padri: "Utasamehewa." "Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango unafunguliwa kutazama, Loh! Mke wa bosi, alipoona kilichotokea akasema anapiga polisi simu. Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikamuua na yeye pia… Yesu atanisamehe hilo?" Padri: "Utasamehewa."
Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke, lakini mlinzi akakataa kunifungulia, ati amesikia mlio wa bastola. Nikaona ataniletea kizuizi huyu. Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikamuua….. Yesu atanisamehe?" Padri:"Utasamehewa."
"Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi akabisha hodi, nikawaza mambo gani tena, akasema alirudi nyumbani na kukuta yaliyotokea akanionesha diary ya babake, inayoonesha nilikuwa na appointment naye wakati nilipomuua. Nikamuuliza nani mwingine anayejua? Akasema ameanzia kwangu kisha anaenda polisi.
Nikatazama huku na huku nikakuta tuko wawili peke yetu, nikamuua….. Yesu atanisamehe na hilo?"
Kimyaa…. "Padri yesu atanisamehe?" kimya….
Jamaa akatazama kwenye confession booth padri hayupo, lakini kwenye kona moja akaona kabati la nguo za mapadri linatikisika. Kufungua akaona padri kajificha ndani anatetemeka huku akitokwa na jasho.
Jamaa, "Sasa baba mbona umekimbia?" Padri kwa taabu akajibu, "Nilitazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu……."
Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza
Zuzu: Mambo Anna! Anna: Poa! Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyeshe… Anna: Kitu gan? Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda) Anna: Haya nionyeshe…
Updated at: 2024-05-25 18:07:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Zuzu: Mambo Anna! Anna: Poa! Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyeshe… Anna: Kitu gan? Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda) Anna: Haya nionyeshe…
Zuzu: Funga mlango na madirisha kwanza (akafunga) Anna: Haya nionyeshe sasa!.. Zuzu: Zima taa kwanza (akazima) Anna: Mhm…nionyeshe sasa! Zuzu: Haya njoo hapa kitandani… Anna: Ok, nionyeshe! Zuzu: Ona nimenunua saa ambayo inawaka yenyewe gizani… Acha mawazo mabaya ww???
Updated at: 2024-05-25 17:07:17 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text "mambo vipi?"…halafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu "shwari"halafu nikarudi nyumbani kulala zangu..
Jamaa aliamua kumtoa demu wake out kwaajili ya chakula cha usiku kufika hotelini wakakaa mezani mhudumu akaja,
Mhudumu: kaka nikuhudumie nini,
Jamaa: afathal NILETEE MENU LISTI
Updated at: 2024-05-25 18:03:52 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jamaa aliamua kumtoa demu wake out kwaajili ya chakula cha usiku kufika hotelini wakakaa mezani mhudumu akaja,
Mhudumu: kaka nikuhudumie nini,
Jamaa: afathal NILETEE MENU LISTI
Mhudumu: dada na wewe?
Demu akajibu kwa pozi tena kwakujishaua, "NA MIMI NILETEE MENU LIST ILA USIWEKE CHUMVI NYINGI"
Chezea mbulula wewe…!!!