Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Vyakula vya kukusaidia kupunguza uzito

Featured Image
Kuchagua vyakula sahihi kwa mlo wako inaweza kuwa changamoto na tungependa kuamini kwamba kupungua uzito ni jambo tu la kula kalori chache na kufanya mazoezi zaidi. Hata hivyo, si mara zote zoezi hili linakuwa rahisi. Kama ni lengo lako kupunguza uzito, kuchagua chakula gani ule ni muhimu kama kuchagua kiasi gani cha chakula ule.

Ukweli ni kwamba , baadhi ya vyakula vinauwezo wakusaidia kupunguza uzito kutokana na tabia zake za kuunguza mafuta mwilini.

Vifuatavyo ndivyo vyakula vinavyosaidia kupunguza uzito:


Mafuta ya Nazi


Mafuta ya nazi yanapanda chati kwa haraka kabisa na kufanya kuwa mojawapo ya vyakula bora kabisa kwa afya ya binadamu.

Mojawapo ya vitu muhimu kabisa katika mafuta haya ni uwezo wake wa kupunguza uzito wa mwili.

Mafuta ya nazi ni yana kemikali yenye mlolongo wa kati wa mafuta (“Medium Fatty Chain Acids”) ambayo humeng’enywa tofauti na yale yenye mlolongo mrefu wa mafuta (“Long Fatty Chain Acids”)

Kemikali zenye mlolongo mrefu wa mafuta(“Long Fatty Chain Acids”) hupatikana kwa wingi katika vyakula vingi vya mafuta kaa vile nyama, chips n.k.

Kemikali zenye mlolongo wa kati wa mafuta hutumiwa na mwili kwa ajili ya nishati badala ya kuhifadhiwa kama mafuta katika mwili.

Hii ndio sababu mafuta ya nazi ni moja ya vyakula vyenye uwezo wa kuchoma mafuta mwilini na kusaidia kupungua uzito.

Siki ya Apple (Apple Cider Vinegar)


Siki ya Apple ina kiwango kikubwa cha kemikali za amino (amino acids) ,kemikali za kumeng’enya chakula na madini na vitamini. Utafiti unaonyesha kwamba kutumia Siki ya Apple kabla ya kula vyakula vya wanga inasaidia kupunguza kupanda kwa insulin hivyo kusaidia kutopata hamu ya kula mara kwa mara.

Ndimu na Limao


Utafiti unaonyesha kuwa kiasi cha vitamini C mwilini kinahusiana na uzito wa mwili.

Watu wenye viwango vya kutosha wa vitamini C wana uwezo wa uwezo wa kuvunja asilimia 30 zaidi ya mafuta wakati wa mwili unapofanya shughuli za nguvu kama kazi za nyumbani,shambani na mazoezi kama kutembea, kuliko wale walio na kiwango cha chini cha vitamini C.

Kama una dhamira ya kupungua uzito, basi fikiria kuanza siku yako kwa kunywa glasi moja ya maji yenye ndimu au limao au anza kutumia siki(vinegar) kwenye kachumbali au saladi unapokula chakula.

Balungi


Balungi yana kiasi kidogo cha kalori , kiwango cha juu cha tindikali za kumeng’enya chakula na inaweza kukufanya usijisikie njaa kwa muda mrefu.

Watafiti wamegundua kwamba kula nusu ya balungi kabla ya mlo ni inachangia sana kupoteza uzito . Pia kula nusu tu ya balungi kabla ya mlo inaweza kusababisha kupungua kwa kiasi cha glucose-insulin katika muda wa masaa mawili tu.

Kama wewe unahitaji kupungua uzito zingatia kula vyakula vinavyo kata mafuta na ongeza vyakula hivi vilivyotajwa katika mlo wako.

Kwa mafanikio ya muda mrefu , kazania kula vyakula kamili (vyakula visivyo kobolewa au kusindikwa) na kufanya mazoezi ya mara kwa mara.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Sababu ya meno kubadilika rangi

Sababu ya meno kubadilika rangi

Wapo baadhi ya watu wanashindwa hata kuachia kicheko chenye bashasha hii ni kwa sababu meno yao y... Read More

Mbinu 11 za kufuata ili uweze kuacha pombe

Mbinu 11 za kufuata ili uweze kuacha pombe

Pombe ni kinywaji kinachotumiwa na watu wengi pasipo hata kufahamu athari zake. Pombe ina athari ... Read More

Namna ya kuongeza nguvu za kiume bila kutumia dawa

Namna ya kuongeza nguvu za kiume bila kutumia dawa

Upungufu wa nguvu za kiume umekua tatizo kubwa sana kwa wanaume wengi. Tatizo hili limewakumba wanau... Read More
Unachotakiwa kujua kuhusu Shinikizo la chini la damu

Unachotakiwa kujua kuhusu Shinikizo la chini la damu

Ugonjwa wa Shinikizo la chini la damu ambao hujulikana kama hypotension kwa Kiingereza ni hali am... Read More

Aina ya vyakula vinavyotakiwa kwa wajawazito

Aina ya vyakula vinavyotakiwa kwa wajawazito

Kwa ajili afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, mwanamke anatakiwa apate chakula bora kilicho na ... Read More

Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba wakati wa hatari

Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba wakati wa hatari

Watu wengi hasa vijana watakuwa wanafahamu dawa ambazo hutumiwa sana kuzuia ujauzito pale ambapo ... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia limau au limao

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia limau au limao

Dawa nyingine nzuri kwa ajili ya chunusi usoni na mwilini ni limau. Limau linajitokeza kwenye vya... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa Siki ya tufaa

Jinsi ya kutibu chunusi kwa Siki ya tufaa

Siki ya tufaa (Apple cider vinegar) ni moja kati ya dawa zinazojulikana katika kutibu chunusi ahs... Read More

Faida za kula Karoti kiafya

Faida za kula Karoti kiafya

Asilimia kubwa tunapenda kutumia karoti katika kuunga katika mboga ya nyama na si kuila karoti ka... Read More

Kutibu shinikizo la chini la damu kwa kutumia maji chumvi

Kutibu shinikizo la chini la damu kwa kutumia maji chumvi

Kunywa Maji yenye chumvi husaidia kutibu shinikizo la chini la damu sababu sodiamu iliyomo kweny... Read More

Faida 8 za kula pilipili mbuzi

Faida 8 za kula pilipili mbuzi

Watu wengi tumekuwa hatufahamu utumiaji wa pipilipili, hasa pilipili mbuzi. Naomba leo tuangalie ... Read More

Dondoo kuhusu tezi dume

Dondoo kuhusu tezi dume

Tezi dume kila mwanaume anazaliwa nayo ambayo inasaidia kutoa maji maji ambayo yanaweza kusaidia ... Read More