Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Faida 13 za kunywa juisi ya miwa

Featured Image

Unapopita maeneo mengi ya mijini na pembezoni wa miji utakutana na wafanyabiashara wa miwa wanaouza miwa na juisi yake. Wengi hununua juisi ya miwa kwa kuwa hufurahia utamu wake. Lakini umeshajiuliza juisi miwa ina faida gani kiafya?

Kuna faida nyingi za juisi ya miwa. Baadhi ya faida hizo ni kama zifuatazo;
1. Juisi ya miwa ina uwezo mkubwa wa kuipatia miili nguvu kwa haraka na kukata kiu ya maji. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari “sucrose” ambayo kazi yake kuu ni kutengeneza nguvu mwilini. Kwa hiyo wakati mwingine ukiwa na uchovu, badala ya kunywa vinywaji vya viwandani tafuta juisi ya miwa.

2. Ingawa juisi ya miwa ina utamu lakini inafaa sana kwa watu wenye kisukari. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari halisi ambayo ina uwezo mdogo wa kuzidisha kiwango cha sukari mwilini au kitaalamu inaitwa “Low Glycemic Index”. Kutokana na hilo juisi ya miwa inashauriwa kutumiwa kama mbadala wa vinywaji vingine vya viwandani. Ni muhimu pia kwa watu wenye kisukari kutumia juisi hii kwa kiasi kidogo au kulingana na ushauri wa Daktari.

3. Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa cha madini ya calcium, magnesium, potassium, chuma na manganese. Madini haya yana uasili wa ualkali ambao husaidia kupunguza uwezekano wa kupata kansa kama vile kansa ya Tezi dume “Prostate cancer” na kansa ya maziwa “Breast Canser”.

4. Juisi ya miwa inasaidia kuongeza kiwango cha protein mwilini na ku-imarisha ufanyaji kazi wa figo.

5. Juisi ya miwa iliyochanganywa na maji ya Nazi husaidia kupunguza maumivu hasa yanayosababishwa na maambukizi ya ngono “STDs” na kidney stones.

6. Juisi ya miwa husaidia kulinda maini yasipate maambukizi. Hii ndo maana Madaktari hushauri matumizi ya juisi ya miwa kwa watu wenye ugonjwa wa Homa ya Manjano.

7. Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa cha madini ya potassium ambayo husaidia kuimarisha mmeng’enyo wa chakula.

8. Husaidia kuzuia maambukizi katika tumbo na utumbo.

9. Vilevile husaidia katika kutibu matatizo ya choo kigumu au kitaalamu inaitwa “constipation”.

10. Uchunguzi unaonyesha juisi ya miwa husaidia kuzuia meno kuoza na matatizo ya kupumua kutokana na kuwa na kiasi kikubwa cha madini. Kwa hiyo kama unafikiria kwenda kwa daktari kung’arisha meno yako, kunywa juisi ya miwa mara kwa mara.

11. Juisi ya miwa husaidia katika kupambana na mabaka mabaka na kung’arisha ngozi.

12. Juisi ya miwa huweza kutumika kama ” face mask na scrub” kwa kuipaka kwenye ngozi na hivyo kusaidia katika kuing’arisha na kuiimarisha uso.

13. Juisi ya miwa ina faida nyingi mwilini, ni muhimu kuhakikisha usafi katika utengenezaji wake.

Kumbuka: Juisi ya miwa isiyokuwa salama inaweza ikawa ni chanzo kikubwa cha magonjwa ya tumbo na kuhara.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Faida za kula ukwaju

Faida za kula ukwaju

Ukwaju ni tunda maarufu sana ambalo hupatikana katika maeneo yenye uoto wa kitropiki. Kwa kingere... Read More

Matumizi ya karoti na asali kutibu presha ya kushuka

Matumizi ya karoti na asali kutibu presha ya kushuka

Hatua za kufuata

1. Tengeneza glasi moja ya juisi ya karoti

2. ... Read More

Dondoo muhimu za afya

Dondoo muhimu za afya

Tafadhali soma na uwapelekee wengine.

Dr. Chriss Mosby wa Tanzania amegundua kensa mpya kwa... Read More

Mambo ya kufanya unapostuka usiku ili kulinda afya yako

Mambo ya kufanya unapostuka usiku ili kulinda afya yako

Kumekuwepo na tatizo la vifo vya ghafla sana tena kwa watu ambao wana afya njema na hii inatokana... Read More

Faida za Korosho Kiafya

Faida za Korosho Kiafya

Korosho zina faida hizi zifuatazo;

1. Zinakinga Maradhi ya Saratani Haswa kwenye matumbo ma... Read More

Matumizi ya Tangawizi kutibu shinikizo la chini la damu

Matumizi ya Tangawizi kutibu shinikizo la chini la damu

Hatua za kufuata

  1. Chukua Kijiko kikubwa kikubwa cha tangawizi mbichi i... Read More
Hizi ndizo faida za kiafya za kuota jua

Hizi ndizo faida za kiafya za kuota jua

Kuna mambo ambayo huwa tunayachukulia ya kawaida na wala hatuko tayari kufahamu umuhimu wake. Jua... Read More

Tiba kwa kutumia maji

Tiba kwa kutumia maji

⭕Tiba kwa kutumia maji⭕
💧💧💧💧💧💧💧💧💧

Hamuwezi kuamini! mar... Read More

Athari za Moshi wa sigara kwa mtoto

Athari za Moshi wa sigara kwa mtoto

Utafiti uliofanyika nchini Marekani umebaini kwamba watu wazima wasiovuta sigara lakini walipokuw... Read More

Faida za kula uyoga kiafya

Faida za kula uyoga kiafya

Uyoga una vitamini na aina nyingi na madini. Virutubisho vilivyothibitishwa kuwemo kwenye uyoga n... Read More

Mchanganyiko wa asali na mdalasini una faida hizi

Mchanganyiko wa asali na mdalasini una faida hizi

Mchanganyiko wa mdalasini na asali unasaidia katika mambo ya aiana tofauti tofauti kama ifutavto:... Read More

Faida ya kunywa maji yenye limao au ndimu kila siku

Faida ya kunywa maji yenye limao au ndimu kila siku

Watalam mbalimbali wa afya wanasema ya kwamba kwa kila siku ni vyema... Read More