Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mimi ni msichana Albino ninaogopa kuwa na rafiki mwanaume kwa kuhofia kuwa anataka tu kujamiiana na mimi na halafu aniache

Mimi ni msichana Albino ninaogopa kuwa na rafiki mwanaume kwa kuhofia kuwa anataka tu kujamiiana na mimi na halafu aniache

Wakati mwingine kuwa na muonekano tofauti na watu wengine
huvuta udadisi. Na hasa tukikumbuk... Read More

Jinsi ya Kuonyesha Mapenzi kwa Msichana Wako

Jinsi ya Kuonyesha Mapenzi kwa Msichana Wako

Leo tutazungumzia juu ya jinsi ya kuonyesha mapenzi kwa msichana wako. Ingawa kuna njia nyingi to... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Leo tutajadili jinsi ya kujiking... Read More

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Ushirikiano na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Ushirikiano na Msichana

  1. Anza kwa Kujijenga Kimaumbile Kabla ya kumwomba msichana tarehe ya ushirikiano, ni muhi... Read More

Msichana akijamiiana mara moja tu anaweza akapata mimba?

Msichana akijamiiana mara moja tu anaweza akapata mimba?

Msichana anaweza kupata mimba akijamii ana mara moja tu. Inategemea na mzunguko wa hedhi. Kama nd... Read More

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Kusisimua na Msichana Wako

Jinsi ya Kuwa na Tarehe ya Kusisimua na Msichana Wako

Tarehe ya kusisimua inaweza kuwa ngumu kupanga, hasa ikiwa unataka kumpendeza mpenzi wako. Lakini... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Karibu vijana wapendwa! Leo, nataka kuzu... Read More

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Kila mwanamume anataka kupata msich... Read More

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Ni kweli kuwa daktari anaweza kufanya vipimo vya kugundua
kama mtoto aliye tumboni ni mwenye... Read More

Je, Ni Vipi Kupata Msaada wa Kielimu Kuhusu Ngono?

Je, Ni Vipi Kupata Msaada wa Kielimu Kuhusu Ngono?

Je, umewahi kujiuliza ni vipi unaweza kupata msaada wa kielimu kuhusu masuala ya ngono? Leo, tuta... Read More

Wakati wa kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume inayopenya kwenye yai, mbegu nyingine zinaenda wapi?

Wakati wa kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume inayopenya kwenye yai, mbegu nyingine zinaenda wapi?

Ni kweli kwamba wakati wa kujamii ana na kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume i inayopenya kwe... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono? 😊

  1. Kwanz... Read More