Mzee kaingia pharmacy,
MZEE: Mambo mwanangu, kuna kitu naomba uonje nitakulipa
MFAMASIA: Kitu gani?….Mzee akatoa kichupa na kijiko akaweka …majimaji yaliyomo kwenye
kichupa kwenye kijiko na kumwambia mfamasia aonje, mfamasia akatia yale maji mdomoni na kuyazungusha zungusha mdomoni akionja;
Updated at: 2024-05-25 18:05:01 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mzee kaingia pharmacy,
MZEE: Mambo mwanangu, kuna kitu naomba uonje nitakulipa
MFAMASIA: Kitu gani?….Mzee akatoa kichupa na kijiko akaweka …majimaji yaliyomo kwenye
kichupa kwenye kijiko na kumwambia mfamasia aonje, mfamasia akatia yale maji mdomoni na kuyazungusha zungusha mdomoni akionja;
MZEE: Nipe jibu, ina utamu wa sukari au chumvi au pilipili?
MFAMASIA: Kama chumvichumvi
MZEE: Hakuna sukari
MFAMASIA: Sukari hakuna kabisa
MZEE: Loh asante chukua hii alfu tano nashukuru sana, dokta alinambia nipime mkojo wangu kama nina kisukari, kumbe sina asante bwana mdogo
Updated at: 2024-05-25 16:53:24 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
HAHAHAHAHAAAAAA DUH TAMAA MBAYA
Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna ki2, alipoifungua likatoka jitu la ajabu. Huku akitetemeka lile jitu likamwambia kijana asante sana kwa kuniokoa omba vi2 viwili sasa hivi. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko la hela na pete ya bahati vikadondoka. Akaambiwa ombi la pili,akasema nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada Hapohapo akageuzwa akawa chipsi yai.!!😂🤣🤣🤣
Cheki huyu mwanamke anavyomkomoa mme wake baada ya kumsaliti
Updated at: 2024-05-25 17:16:59 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
MKE: Mbona unanukia pafyumu ya kike? MUME: Yaa kuna mwanamke tulikuwa tumeminyana ndani ya daladala MKE: Na lipstiki kwenye shati? MUME: Tulikumbatiana na wageni toka Zambia walitembelea ofisi yetu MKE: Na ile kondom iliyotumika kwenye mfuko wa suruali? MUME: Bwana ee acha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi MKE: Lazima niulize mie huwa nahakikisha nimeacha kila kitu hukohuko ndio narudi nyumbani MUME: Umesema nini wewe? MKE: Bwana ee acha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi. 😄😄
Updated at: 2024-05-25 17:04:51 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jana niligombana na mke wng, Akaniambia nibebe kila kitu changu niondoke, Bas kiustaarabu tu nikachukua nguo zangu,mwishoni nikambeba na yeye nikamuweka begani nikaanza kuondoka nae
hua sipendagi ujinga, amesahau na yeye pia ni wangu