Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Ni umri gani ambapo vijana wanapaswa kuelezwa juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango?

Featured Image

Vijana balehe wote wana haki ya kupata habari juu ya mambo yote
wanayoyapenda. Watoto wanavyokuwa, wanapitia mabadiliko ya
kimwili, hisia na ya kisaikolojia katika maisha yao. Watu wazima,
hasa wale wanaowasimamia watoto wanapaswa kuwapa habari
juu ya mabadiliko na jinsi yanavyoshawishi ukuaji wa kimwili na
hisia. Hii ni muhimu ifanyike muda wote na katika kila rika.
Vijana wana mahitaji mbalimbali kutegemea umri wao, katika
hatua ya ukuaji na mazingira, mvulana wa umri wa miaka 11 au
kijana wa miaka 18 watakuwa na shauku tofauti. Pi wavulana au
wasichana wana haja tofauti na hata vijana wawili wenye umri
na jinsia moja wanaweza kukua kwa kasi na njia tofauti.
Tofauti hizi zinahitaji
kutambuliwa na kushughulikiwa.
Ni muhimu
pia kutambua
kwamba mahitaji
haya yatabadilika
kadiri ya muda unavyoenda
na pia kuweza
kubadilika kwa
haraka sana. Kwa
mfano mtu anapokuwa
na mhemuko wa
kujisikia kujamiiana.
Kwa njia yoyote, watoto
wana haja ya
kupata habari juu ya
uzazi kabla au mara
tu wapaoingia katika
ujana. Pia mada juu ya wajibu wa wavulana na wasichana katika
jamii, uhusiano na marafiki, na wazazi, uhusiano wa kijinsia na
matatizo yanayotokana na unyanyasaji wa kijinsia / ujinsia ni
muhimu yajadiliwe.
Iwapo vijana hawapati habari za kutosha juu ya mabadiliko ya
miili yao wanaweza kuingizwa katika matatizo ya kimaisha, ya
kijinsia na mimba yasiyotarajiwa au magonjwa yatokanayo na
kujamiiana pamoja na Virusi vya UKIMWI. Kwa hiyo wasichana
na wavulana wanahitaji kupata elimu ya ujinsia wanapokuwa vijana
wadogo. Hii ni pamoja na habari ya jinsi ya kujilinda wenyewe.
Siyo kweli kwamba elimu ya ujinsia inahimiza vijana wajamiiane.
Kinyume chake, wale vijana waliopata habari sahihi wanakuwa
na mwelekeo mzuri na wana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi
. kama vile kuamua kuahirisha kujamiiana mpaka baadaye na
pia wanajilinda mara wanapoanza kujamiiana. Elimu ya Afya ya
Uzazi na Ujinsia ina habari juu ya uzuiaji wa mimba na kondomu.
Kabla ya kuanza kujamiiana inatakiwa vijana waelezwe kuhusu
njia za uzazi wa mpango na hasa jinsi ya kutumia kondomu kwa
sababu kondomu huzuia maambukizo ya Virusi vya UKIMWI
na magonjwa yatokanayo na kujamiiana. Jambo la busara ni
kwenda kliniki kwa ushauri katika suala zima la njia za uzazi wa
mpango mara tu ukiamua kuanza kujamiiana.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, mtu anawezaje kuacha kutumia dawa za kulevya na itamchukua muda gani kurudia hali yake ya kawaida?

Je, mtu anawezaje kuacha kutumia dawa za kulevya na itamchukua muda gani kurudia hali yake ya kawaida?

Kitu muhimu ni kwamba, kweli uwe umedhamiria kuacha. Hatua ya kwanza ni kujiuliza kwa nini unatum... Read More

Sabau za ubakaji

Sabau za ubakaji

Ni vigumu kuelewa nini kinamfanya mtu aweze kubaka mwingine.
Ubakaji ni aina nyingine ya uka... Read More

Nifanyeje kuepuka vishawishi vya kujamiiana kutoka kwa watu wengine, hasa wakubwa?

Nifanyeje kuepuka vishawishi vya kujamiiana kutoka kwa watu wengine, hasa wakubwa?

Vijana wengi wanajikuta wanatumbukia katika matatizo mazito kama kupata mimba mapema, utoaji wa m... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Karibu vijana wapendwa! Leo, nataka kuzu... Read More

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Habari rafiki yangu! Leo tutaongea kuhusu umuhimu wa kuzungumza waziwazi juu ya ngono na kufanya ... Read More

Je, wazazi ambao wote ni Albino wanaweza kupata mtoto ambaye siyo Albino?

Je, wazazi ambao wote ni Albino wanaweza kupata mtoto ambaye siyo Albino?

Kwa kawaida, wazazi wote wakiwa Albino watazaa mtoto
Albino. Kwa maana hiyo basi, iwapo watu... Read More

Njia za Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Njia za Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Leo, tutajadili njia za kuunda uhusiano mzuri na wa furaha na msichana. Kuwa na uhusiano mzuri na... Read More

Albino anaweza kuwa na maisha ya kawaida na yenye mafanikio katika maisha?

Albino anaweza kuwa na maisha ya kawaida na yenye mafanikio katika maisha?

Imani iliyojengeka kwenye jamii kuwa Albino wana uwezo
mdogo si ya kweli. Ipo mifano mingi y... Read More

Vidokezo vya Kufurahia Safari za Pamoja na Msichana

Vidokezo vya Kufurahia Safari za Pamoja na Msichana

Kila mwanamume anapenda kukutana na msichana ambaye anaweza kuwa rafiki wa karibu na kuwa na uhus... Read More

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi? Swali hili linaweza kusababisha maj... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Ana kwa Ana na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Ana kwa Ana na Msichana

Mawasiliano mazuri ya ana kwa ana na msichana ni muhimu sana katika uhusiano wowote. Ni njia bora... Read More

Je, kama mwanamke na mwanaume wanapata watoto wa jinsia moja tu, ni kosa la nani?

Je, kama mwanamke na mwanaume wanapata watoto wa jinsia moja tu, ni kosa la nani?

Hakuna mwenye kosa, kwa sababu jinsia ya mtoto i inategemea na bahati na hamna uwezekano wa kupan... Read More