Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Balehe ni kipindi cha mpito kati ya utoto na utu uzima, ambapo watoto wa ki... Read More

Je, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI vinaambukiza kwa kujamiiana kwa njia ya sehemu ya haja kubwa au mdomoni?

Je, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI vinaambukiza kwa kujamiiana kwa njia ya sehemu ya haja kubwa au mdomoni?

Ndiyo, kuna hatari kubwa ya kuambukizwa Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wakati wa kujamii ana kwa nji... Read More

Jinsi ya Kuwa na Ukaribu wa Kihisia na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Ukaribu wa Kihisia na Msichana

Kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na msichana ni jambo zuri sana. Hata hivyo, kuwa na ukaribu wa ... Read More

Jinsi ya Kuomba Msichana Awe Rafiki Yako

Jinsi ya Kuomba Msichana Awe Rafiki Yako

Kuomba msichana awe rafiki yako si jambo rahisi kama inavyoweza kuonekana kwa wengi. Hata hivyo, ... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Upendeleo wa ngono na kufanya mapenzi ni jambo muhimu katika mahusiano yetu ya kimapenzi. Inapasw... Read More

Jinsi ya Kuepuka Kupotoshwa kuhusu Ngono na Mitandao ya Kijamii

Jinsi ya Kuepuka Kupotoshwa kuhusu Ngono na Mitandao ya Kijamii

Jinsi ya Kuepuka Kupotoshwa kuhusu Ngono na Mitandao ya Kijamii πŸ“±πŸ”žπŸ”’

Karibu vijana... Read More

Je, watu wanapendelea kutumia kinga wakati wa kufanya ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kutumia kinga wakati wa kufanya ngono/kufanya mapenzi?

  1. Kutumia Kinga Hupunguza Hatari za Maambukizi ya Ngono Kutumia kinga ni hatua muhimu kat... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano? 🌼

Habari za leo... Read More

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mape... Read More

Nini matatizo ya watoto Albino shuleni?

Nini matatizo ya watoto Albino shuleni?

Ingawaje, akili zao hazina hitilafu watoto Albino mara nyingi
hawafanyi vizuri shuleni, na h... Read More

Je, ukinywa pombe unaongeza damu?

Je, ukinywa pombe unaongeza damu?

Si kweli.
Pombe haiongezi damu, vitamini wala nguvu. Ukweli ni kwamba unywaji po... Read More

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza?

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza?

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza? 🌍πŸ’₯😊

Karibu kijana! Le... Read More