Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Mapishi ya Wali, samaki, bilinganya na spinach

Featured Image

Mahitaji

Samaki
Spinach
Bilinganya
Nyanya ya kopo (Kopo 1)
Vitunguu maji
Vitunguu swaumu
Tangawizi
Pilipli mbuzi
Chumvi
Limao
Carry powder
Mchele
Mafuta ya kupikia
Coriander
Hiliki
Amdalasini
Karafuu

Matayarisho

Osha samaki na kisha wamarinate na vitunguu swaumu, tangawizi, limao, chumvi na pilipili kwa muda wa masaa matatu. Baada ya hapo wakaange samaki na uwaweke pembeni kwa ajili ya mchuzi.
Osha spinach na kisha zikatekate na ziweke pembeni
Osha mchele na kisha uloweke kwenye maji kwa muda wa dakika kumi
Osha bilinganya kisha likatekate vipande vidogo dogo

Jinsi ya kupika

Mchuzi

Saga pamoja vitunguu maji, vitunguu saumu, tangawizi, nyanya.Kisha weka mchanganya katika sufuria na uinjike jikoni kwenye moto wa kawaida. Pika mchanganyiko mpaka ukauke kisha tia mafuta, chumvi na carry powder. pika kwa muda wa dakika kumi kisha tia samaki na tui la nazi. Acha mchuzi uchemke mpaka tui la nazi liive.kishaipua na tia coriander

Spinach

Kaanga vitunguu maji na mafuta, baada ya hapo tia spinach na chumvi acha ziive kidogo kisha ipua tayari kwa kuliwa.

Mabilinganya

Kaanga vitunguu maji na mafuta mpaka viwe vya brown kisha tia nyanya. Acha ziive kisha tiai mabilinganya na chumvi. Yakishaiva ipua weka pembeni tayari kwa kuliwa.

Wali

Chemsha maji ya wali kwenye sufuria, kisha tia hiliki, pilipili mtama mzima, karafuu na amdalasini, chumvi na mafuta. Kisha tia mchele na uufunike na uache uchemke mpaka utakapokauka maji. Geuza na uache mpaka uive. Kisha ipua. Tayari kwa kuliwa

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Sanaa ya Upishi Imara: Kupata Lishe Muhimu

Sanaa ya Upishi Imara: Kupata Lishe Muhimu

Sanaa ya Upishi Imara: Kupata Lishe Muhimu

Jambo hilo kuu kwa afya njema na maisha bora ni... Read More

Jinsi ya kupika Donati

Jinsi ya kupika Donati

Viamba upishi

Unga
2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)

Sukari
1/3 Kikombe ch... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu

Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu

MAHITAJI

Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2

... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

Mapishi ya Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

VIAMBAUPISHI

Mchele - 3 vikombe

Nyama ya kusaga - 1 LB

Mchanganyiko wa Nafaka... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mahitaji

Mchele wa basmati - 4 cups

Samaki nguru (king fish) - 7 vipande au zaidiRead More

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mahitaji

Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa - 2 LB

Mchanganyiko wa dengu (hadesi... Read More

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Viambaupishi Vya Masala

Nyama vipande - 3 LB

Mtindi - Β½ kopo

Kitunguu (thomu... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

MAHITAJI

Unga - 1 Kikombe

Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe

Siagi - 125 gms

<... Read More
Mapishi ya Supu ya makongoro

Mapishi ya Supu ya makongoro

Mahitaji

Makongoro (miguu ya ng'ombe) kiasi
Limao 1 kubwa
Kitunguu swaum
T... Read More

Tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na la kuku wa kisasa

Tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na la kuku wa kisasa

Kilishe mayai yote ni sawa. Virutubishi vinavyopatikana kwenye yai la kuku wa kienyeji kama proti... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tangawizi

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tangawizi

MAHITAJI

Unga - 2 Vikombe

Cocoa ya unga - 1 Kijiko cha supu

Sukari ya hudhuru... Read More

Jinsi ya kutengeneza Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Jinsi ya kutengeneza Slesi Za Chokoleti Na Karameli

VIAMBAUPISHI

Unga - 1 Magi (vikombe vya chai)

Sukari ya browni - Β½ Magi

Siag... Read More