Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Featured Image

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo - 2lb

Nyanya - 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa - 1

Mafuta - 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) - ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu - 1

Chumvi - Kiasi

Ndimu - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage - 1 kopo

Kitunguu - 1

Nazi - 1 mug

Nyanya (itowe maganda) - 1 kiasi

Pilipili mbichi - 2

Mafuta - 1 kijiko cha supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi - 4/5

Kotmiri - 1 Kijiko cha supu

Ndimu - kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 chembe

Mafuta ya zaituni - 2 vijiko Vya supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji - 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe - 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Mchuzi Wa Kuku wa Tanduri

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Mchuzi Wa Kuku wa Tanduri

Vipimo vya Wali:

Mchele basmati - 3 magi (kikombe kikubwa)

Mchanganyiko wa mboga za... Read More

Jinsi ya kutengeneza Muhogo Wa Nazi Na Samaki Wa Kukaanga

Jinsi ya kutengeneza Muhogo Wa Nazi Na Samaki Wa Kukaanga

Mahitaji

Muhogo - 3

Tui La Nazi - 2 vikombe

Chumvi - kiasi

Pilipili mbi... Read More

Mapishi ya Supu ya makongoro

Mapishi ya Supu ya makongoro

Mahitaji

Makongoro (miguu ya ng'ombe) kiasi
Limao 1 kubwa
Kitunguu swaum
T... Read More

Mapishi ya Wali Wa Nyanya Wa Kukaanga

Mapishi ya Wali Wa Nyanya Wa Kukaanga

Vipimo

Mchele basmati, pishori - 3 vikombe

Vitunguu katakata - 2

Nyanya/tungu... Read More

Jinsi ya kupika Mboga Za Majani Makavu (Aina Yoyote)

Jinsi ya kupika Mboga Za Majani Makavu (Aina Yoyote)

Viamba upishi

Mboga za majani makavu ¼ kg
Mafuta vijiko vikubwa 3-4
Karanga zi... Read More

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe

Sukari - 1 Kikombe

Baking powder 1 kijiko cha c... Read More

Mapishi ya Borhowa

Mapishi ya Borhowa

Mahitaji

Daal (lentils) nyekundu au/na kijani - 1 Kikombe kikubwa

Bizari ya manjano... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu ... Read More

Mapishi ya Ndizi mzuzu

Mapishi ya Ndizi mzuzu

Mahitaji

Ndizi tamu (plantain) 3-4
Tui la nazi (coconut milk) kikombe 1 cha chai
Read More

Jinsi ya kutengeneza Nangatai

Jinsi ya kutengeneza Nangatai

MAHITAJI

Unga wa ngano - 2 - 2 ¼ Vikombe

Siagi - 1 ½ Kikombe

Sukari - 1 Kik... Read More

Kupima lishe au afya ya mtu

Kupima lishe au afya ya mtu

Njia za kupima Afya

Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;

Read More
Mapishi ya Half cake (Keki)

Mapishi ya Half cake (Keki)

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2
Sukari (sugar) 1/4 kikombe... Read More