Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Featured Image

Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iweze kuwa penseli bora kabla hajaituma kuingia kazini kwa matumizi.

“Kuna vitu sita unatakiwa uvitambue, “ Aliiambia penseli,

“Kabla sijakutuma kwenda kutumika, unatakiwa uviweke akilini vitu hivyo na usivisahau kamwe. Vitakusaidia siku zote na utakuwa penseli bora maisha yako yote.”

Alisema muumbaji wa penseli.

“Moja,” alianza kuvitaja,”utakuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi, lakini kama utakubali na utaruhusu kuongozwa na mkono wa mtumiaji wako”

“Mbili” aliendelea kutoa nasaha, “utapata maumivu makali kutokana na kuchongwa mara kwa mara. Lakini vumilia kwani itakusaidia kuwa penseli bora na kuandika vizuri.”

“Tatu, utakuwa na uwezo wa kusahihisha makosa utakayo yafanya.”

“Nne, kitu pekee cha muhimu katika maisha yako ni kile kilicho ndani yako kwa sababu ndicho chenye uwezo wa kuandika.”

“Tano” alisisitiza mtengenezaji penseli, “kwenye kila sehemu utakayotumika, utaacha alama yako. Hata ikiwa ni kwenye sehemu ngumu au mbaya kiasi gani, ni lazima alama yako ibaki.

“Na sita”, alimalizia muumbaji yule wa penseli, “ipo siku utaisha na kupotea. Hivyo usiwe na hofu wala woga wala hudhuni uikaribiapo siku hiyo na ukaogopa kutimiza wajibu wako kwa kuhofia kuisha. Ukiogopa kuisha hautotumika na umuhimu wako hautonekana kwani hautatimiza wajibu uliombiwa kuufanya”

Penseli ilielewa na kuahidi kukumbuka na ikaingia sokoni ikiwa na dhamira yake moyoni.

Sasa tutumie mfano huo wa penseli katika maisha yetu halisi. Ukivikumbuka vitu hivyo sita ilivyopewa penseli, utaweza kuwa mtu bora kabisa kwenye maisha yako yote.

Moja, una uwezo wa kufanya mambo mengi na makubwa, kama utajiweka kwenye mikono ya Mungu.

Mbili, utakutana na magumu mengi ya kuumiza, lakini hayo ndiyo yatakufanya uwe mtu imara na bora, usiyakimbie.

Tatu, una uwezo wa kurekebisha makosa yote uliyoyafanya. Usijilaumu.

Nne, sehemu yako ya muhimu ni ile iliyo ndani yako kwani ndiyo inayoandika maisha yako. Ilinde.

Tano, kila sehemu utakayopita, acha alama yako kwa kufanya mazuri yatakayokufanya ukumbukwe daima, bila kujali mazingira. Timiza wajibu wako kwa kiwango cha juu.

Sita, tambua kuwa ipo siku utakufa. Usiwe na hofu yoyote juu ya kifo kwani ukiogopa kifo hutafanya lolote hapa duniani.

Tumia mfano huu wa penseli upate ujasiri wa kutambua kuwa wewe ni mtu muhimu hapa duniani na umeumbwa kwa madhumuni maalumu na umepewa uwezo mkubwa sana na Muumba wako! Ni wewe pekee mwenye uwezo wa kutimiza dhamira uliyotumwa na Muumba.

UBARIKIWE SANA.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Grace Minja (Guest) on April 16, 2024

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

James Kimani (Guest) on July 25, 2023

Rehema hushinda hukumu

Violet Mumo (Guest) on July 10, 2023

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Edward Lowassa (Guest) on June 20, 2023

Nakuombea 🙏

Joyce Mussa (Guest) on December 25, 2022

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

David Sokoine (Guest) on April 13, 2022

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Henry Mollel (Guest) on October 19, 2021

Mwamini Bwana; anajua njia

Andrew Mahiga (Guest) on October 7, 2021

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Peter Mwambui (Guest) on August 6, 2021

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

John Lissu (Guest) on June 1, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Diana Mumbua (Guest) on April 22, 2021

Endelea kuwa na imani!

Nancy Kabura (Guest) on April 11, 2021

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Richard Mulwa (Guest) on September 17, 2020

Mungu ni mwema, wakati wote!

Edward Lowassa (Guest) on July 2, 2020

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

James Mduma (Guest) on July 1, 2020

Mwamini katika mpango wake.

Martin Otieno (Guest) on June 26, 2020

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Rose Amukowa (Guest) on February 22, 2020

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Samson Tibaijuka (Guest) on January 11, 2020

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Martin Otieno (Guest) on January 9, 2020

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Richard Mulwa (Guest) on November 25, 2019

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Charles Mboje (Guest) on July 25, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Raphael Okoth (Guest) on May 16, 2019

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Sarah Karani (Guest) on May 6, 2019

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Lydia Mzindakaya (Guest) on February 2, 2019

Dumu katika Bwana.

Benjamin Masanja (Guest) on January 19, 2019

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

John Malisa (Guest) on December 2, 2018

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Samuel Omondi (Guest) on September 12, 2018

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Thomas Mwakalindile (Guest) on August 11, 2018

Baraka kwako na familia yako.

Elizabeth Malima (Guest) on May 21, 2018

Neema na amani iwe nawe.

Simon Kiprono (Guest) on January 25, 2018

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Alice Jebet (Guest) on November 20, 2017

Katika imani, yote yanawezekana

John Lissu (Guest) on October 30, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Jane Muthoni (Guest) on September 23, 2017

Sifa kwa Bwana!

Andrew Mahiga (Guest) on June 3, 2017

Rehema zake hudumu milele

Diana Mumbua (Guest) on February 24, 2017

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Michael Onyango (Guest) on November 29, 2016

Mungu akubariki!

Betty Kimaro (Guest) on September 29, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Paul Kamau (Guest) on September 23, 2016

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Joseph Kitine (Guest) on June 8, 2016

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

John Lissu (Guest) on June 4, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

Irene Akoth (Guest) on May 15, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Peter Mugendi (Guest) on May 6, 2016

Nguvu hutoka kwa Bwana

Betty Kimaro (Guest) on March 17, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Nicholas Wanjohi (Guest) on February 28, 2016

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Grace Wairimu (Guest) on January 10, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Samuel Were (Guest) on November 5, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Nicholas Wanjohi (Guest) on August 10, 2015

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Chris Okello (Guest) on May 7, 2015

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Esther Cheruiyot (Guest) on May 6, 2015

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Moses Kipkemboi (Guest) on April 14, 2015

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha umuhimu wa kuishi imani katika matendo mema?

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha umuhimu wa kuishi imani katika matendo mema?

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha umuhimu wa kuishi imani katika matendo mema? Jibu ni... Read More

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Karibu kwenye makala hii ambayo in... Read More

Tofauti kati ya Ibada, Sadaka na Sala/maombi

Tofauti kati ya Ibada, Sadaka na Sala/maombi

Read More
Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Read More
Tarehe ya Pasaka inavyopatikana

Tarehe ya Pasaka inavyopatikana

KWANINI TAREHE ZA PASAKA HUBADILIKA KILA MWAKA ??

JIBU:
KALENDA za mwanzo ziliutumia m... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ekaristi?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ekaristi?

Sakramenti ya Ekaristi ni moja kati ya sakramenti saba zinazoheshimiwa na Kanisa Katoliki. Kwa mu... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Yesu Kristo?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Yesu Kristo?

Habari za leo kwa wapenzi wa Yesu Kristo? Leo nitapenda kuzungumzia kuhusu imani ya Kanisa Katoli... Read More

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Mungu katika Ekaristi Takatifu?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Mungu katika Ekaristi Takatifu?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Mungu katika Ekaristi Takatifu?

Ndio, Kanisa Katoliki lina... Read More

MAFUNDISHO MUHIMU KUHUSU MWILI NA DAMU YA YESU KRISTU | BIBLIA INAVYOELEZA KUHUSU EKARISTI

MAFUNDISHO MUHIMU KUHUSU MWILI NA DAMU YA YESU KRISTU | BIBLIA INAVYOELEZA KUHUSU EKARISTI

Read More
Heshima za Liturujia kwa Bikira Maria

Heshima za Liturujia kwa Bikira Maria

Read More
Jifunze kitu Kwenye mfano huu kuhusu Maombi na kuomba

Jifunze kitu Kwenye mfano huu kuhusu Maombi na kuomba

Nabii mmoja aliumwa
na Jino, lilimtesa sana…
Akapiga magoti kumlilia
Mungu ili a... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Kanisa Katoliki limekuwa likitetea uadilifu wa kijamii na tofauti za kijamii kama sehemu ya imani... Read More