Nikitafuta rafiki kwa nia ya kuoana (mchumba), je ni sifa gani niangalie kwa msichana/mvulana?
Date: April 17, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Kuchagua mchumba ni moja ya maamuzi ambayo kijana anahitaji kuyafanya kwa uangalifu mkubwa sana. Kwa sababu huyo ndiye atakayekuwa mwenzi wake wa maisha. Katika kuchagua mchumba kila mtu ana mawazo yake kuhusiana na kilicho muhimu kuzingatiwa. Mara nyingi mhemuko una nguvu zaidi kuliko uamuzi wa kimantiki
Hata hivyo, vifuatavyo ni kati ya vigezo ambavyo vinaweza kuangaliwa:
• Chagua mtu anayekuheshimu wewe na wengine; Chagua mtu unayemwamini;
• Chagua mtu ambaye unaweza kuongea, kujadiliana, na kuhojiana naye kwa uwazi bila kugombana;
• Chagua mtu mwenye umri unaokaribiana na wa kwako;
• Chagua mtu anayependelea vile unavyopendelea;
• Chagua mtu ambaye ataelewa matatizo yako na yuko tayari kukusaidia kuyatatua; na
• Chagua mtu mwenye afya nzuri.
Hii inamaanisha pia kumpata mtu ambaye kabla ya kuanza kujaamiana naye, atakuwa tayari kwenda kupima kwa hiari kujua hali yake ya VVU na pia kuwa tayari kutumia kinga kwa maana ya kondomu hadi hapo mtakapojua hali zenu.
Wafahamishe wazazi wako mtu uliyemchagua kama mchumba na mtambulishe kwao i ili wamfahamu na yeye awafahamu wazazi wako. Wakati huohuo na wewe jaribu kuwafahamu wazazi wake. Usifanye uchumba wa haraka. Pata muda wa kutosha kumwelewa rafiki yako.
Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.
Related Posts
Ubikira ni nini?: Maana halisi ya neno “bikira” ni mwanamke au mwanaume amb...
Read More
Pombe zinazotengenezwa kiwandani zinafuata viwango
ambavyo ubora wake umethibitishwa kihalal...
Read More
Ni kweli kwamba wakati wa kujamii ana na kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume i inayopenya kwe...
Read More
Nifanyeje Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba? 🌸🌍
Read More
Rafiki yako wa kike ana haki ya kukataa kujamiiana na wewe.
Labda hayuko tayari kujamiiana a...
Read More
Habari za leo rafiki yangu! Leo tutazungumzia jambo muhimu sana kwenye uhusiano wa mapenzi, ambal...
Read More
Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba 😊
Karibu...
Read More
Vijana wengi wanajikuta wanatumbukia katika matatizo mazito kama kupata mimba mapema, utoaji wa m...
Read More
Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano ya Wazi na Msichana Wako
Ndoa ni muunganiko wa wawili kuwa ki...
Read More
Jinsi ya Kujikinga na Mimba Kwa Ufanisi 🌟
Karibu vijana wenzangu! Leo, tutajadili njia ...
Read More
Tunatofautisha dawa za kulevya katika makundi mawili. Zile zinazokubalika na zile zisizokubalika ...
Read More
Albino wana ngozi nyeupe, nywele nyeupe au nyekundu na macho
ya kijivu au ya bluu. Ngozi yao...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!