Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Je, zipo sheria zinazolinda watu wenye ulemavu hapa Tanzania?

Featured Image

Ndiyo, zipo sheria
hapa T a n z a n i a
z i n a z o w a l i n d a
watu wenye
ulemavu. Tanzania
ilitia saini na
kuridhia mkataba
wa kimataifa wa
ulinzi, haki na
usawa kwa watu
wenye ulemavu
mwaka 2006. Kwa
kitendo hicho
cha kuridhia
mkataba huo wa
kimataifa Tanzania
imeonyesha nia
yake ya kuwalinda
na kudumisha
haki za watu
wenye ulemavu.
Hata katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka
19772 inakataza ubaguzi wa aina yoyote kwa watu wenye
ulemavu.
Zipo sheria nyingi zinazolinda haki na usawa kwa watu wenye
ulemavu ambazo zinahusika na sekta mbalimbali. Kwa mfano;
elimu na mafunzo, ajira3, matunzo4 na ustawi5 kwa ujumla. Ipo
pia sera ya Taifa kuhusu ulemavu ya mwaka 20046. Sera hii
imeweka mazingira muafaka kwa watu wenye ulemavu kupata
haki sawa katika maendeleo ya kijamii, ikiwa ni pamoja na
kupata huduma na mahitaji ya msingi kutoka katika jamii.


Sheria zinazolinda haki za Albino

Hakuna sheria mahususi inayowalenga watu wanaoishi na ualbino
hapa Tanzaina. Ingawaje haki za msingi za Albino zinalindwa
chini ya Katiba
ya nchi pamoja
na Sheria
z i n a z o h u s i k a
na sekta
m b a l i m b a l i .
Sheria hizi
zinakataza na
kukemea aina
zote za ubaguzi
kwa misingi ya;
rangi, kabila,
ulemavu na
kadhalika.
Sera ya Taifa ya ulemavu inabainisha hali ya ulemavu kuwa ni,
“kutokuwa au kupungukiwa na uwezo wa kushiriki kwa usawa
katika shughuli za kawaida za kijamii kutokana na sababu
za mapungufu ya kimwili, akili au kijamii”. Sera hii inatoa
mwongozo wa kutolewa kwa haki na fursa sawa kwa walemavu
kupata mambo na huduma za msingi kama; elimu, taarifa, ajira,
matunzo, huduma za afya, kumudu na kufikia huduma muhimu.
Katika siku za karibuni kumeongezeka vitendo vya kikatili dhidi
ya Albino ambavyo ni pamoja na mauaji ya kikatili na kukatwa
viungo kutokana na imani za kishirikina. Watu wenye ualbino
wanalindwa kisheria kutokana na vitendo hivi kwa kupitia
sheria zilizopo za makosa ya jinai.

Serikali pia imechukua hatua za kudhibiti hali hii isiendelee
kutokea ikiwa ni pamoja na kuanza kuwaandikisha rasmi
(kufanya sensa) watu wenye ualbino, na pia kuanzishwa
kwa ulinzi kwa Albino kupitia jeshi la polisi na jamii kwa ujumla,
kwa mfano; watoto Albino wanapokwenda shule.
Suala la Albino limeendelea kupewa umuhimu mkubwa kitaifa,
ikiwa ni pamoja na mjadala wa kitaifa. Mfano; ujumbe wa mbio
za Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2009 ulilenga kuhamasisha
jamii kuhusu mauaji na vitendo vya kikatili dhidi ya Albino.
Mauaji na vitendo vya kikatili dhidi ya Albino vinavyotokea
sasa hivi pia vimepelekea serikali kuchukua hatua na kuongeza
ulinzi ili kulinda haki za Albino kwa mfano; zimeundwa
mahakama maalumu za kusikiliza makosa hayo ili kuharakisha
upatikanaji wa haki kwa wahusika. Mpaka sasa watuhumiwa
saba wa mauaji ya Albino wamekutwa na hatia na kuhukumiwa
kifo kwa kunyongwa.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, unaweza kufa kutokana na kuvuta sigara na kunywa pombe?

Je, unaweza kufa kutokana na kuvuta sigara na kunywa pombe?

Ndiyo. Unaweza kufa kutokana na kuvuta sigara au kunywa
pombe. Lakini pale tu utakapozidisha... Read More

Matatizo yanayotokana na ujauzito katika umri mdogo

Matatizo yanayotokana na ujauzito katika umri mdogo

Wataalamu wanashauri kwamba msichana anastahili kuanza kubeba mimba kuanzia umri wa miaka 18 hadi... Read More

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Ndiyo, unaweza kuambukizwa ukitumia nyembe kali au sindano kwa kuchangia pamoja na mtu mwenye vir... Read More

Je, ni sahihi kuzungumza na wenzio/ marafiki juu ya uhusiano wangu wa kimapenzi?

Je, ni sahihi kuzungumza na wenzio/ marafiki juu ya uhusiano wangu wa kimapenzi?

Kama unavyohusisha rafiki zako katika mihemuko mingine, inaeleweka kama utataka kuwashirikisha ka... Read More

Njia za Kuonyesha Msichana Wako Kuwa Ana thamani Kwako

Njia za Kuonyesha Msichana Wako Kuwa Ana thamani Kwako

Kama mwanaume, kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya ili kuonyesha msichana wako kuwa ana thama... Read More

Je, nikijamiiana na mtu mwenye virusi vya UKIMWI bila kutumia kondomu, nitapata virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Je, nikijamiiana na mtu mwenye virusi vya UKIMWI bila kutumia kondomu, nitapata virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Uwezekano wa kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI ukijamii ana na mtu mwenye virusi vya UKI... Read More

Je, kuna dawa yoyote ya kutibu ugumba?

Je, kuna dawa yoyote ya kutibu ugumba?

Hakuna jibu la ujumla kwa swali hili, kwa sababu tiba ya ugumba inategemea chanzo maalum cha ugum... Read More

Mahusiano ya kimapenzi kati ya msichana mwenye umri mdogo na watu wazima

Mahusiano ya kimapenzi kati ya msichana mwenye umri mdogo na watu wazima

Inawezekana kwa msichana mdogo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwenye umri mkubwa. Hata... Read More

Nifanyeje kujiepusha na vishawishi vya mpenzi wangu vinavyoweza kunifanya nisitumie kondomu?

Nifanyeje kujiepusha na vishawishi vya mpenzi wangu vinavyoweza kunifanya nisitumie kondomu?

Mara nyingine siyo rahisi kujiepusha na vishawishi vya kujamiiana bila kutumia kondomu kutokana n... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano? 🌼

Habari za leo... Read More

Je, ni kweli ukinywa maziwa baada ya kuvuta sigara huwezi kudhurika?

Je, ni kweli ukinywa maziwa baada ya kuvuta sigara huwezi kudhurika?

Hapana. Hii si kweli kwa sababu maziwa hayawezi kuondoa
uharibifu uliosababishwa na nikotini... Read More

Je, ni muhimu kujadili haki na usawa wa kijinsia katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, ni muhimu kujadili haki na usawa wa kijinsia katika ngono/kufanya mapenzi?

Kujadili haki na usawa wa kijinsia katika ngono/kufanya mapenzi ni muhimu sana katika jamii yetu.... Read More