Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Jinsi ya kupika Mseto Kwa Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi

Featured Image

Vipimo vya mseto

Tanbihi: Kiasi ya vipimo inategemea wingi wa watu, unaweza kupunguza au kuongeza. Hiki ni kiasi cha watu 6 takriban.

Chooko - 3 Vikombe

Mchele - 2 Vikombe

Samli - 2 vijiko Vya supu

Chumvi - kiasi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

Safisha na kosha chooko utoe taka taka zote.
Osha mchele kisha roweka pamoja na chooko kwa muda wa saa au zaidi.
Pika chooko na mchele ukiongeza maji inapohitajika, tia chumvi, funika pika moto mdogo mdogo huku unakoroga kwa mwiko kila baada ya muda huku unaponda ponda.
Karibu na kuwiva na kupondeka tia samli endelea kupika hadi karibu na kukauka. Epua.

Samaki

Vipande vya samaki (nguru) - 6 – 7 (4LB)

Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa ukipenda - 1 kijiko cha chai

Bizari ya samaki - 1 kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Ndimu - kiasi

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Namna Ya Kutaysha Na Kupika

Changanya thomu/tangawizi, pilipili, bizari, chumvi pamoja na ndimu iwe masala nzito.
Paka vipande vya nguru kwa masala hayo weka akolee dakika kumi hivi.
Kaanga vipande vya nguru katika mafuta madogo kwenye kikaango (fyring pan) uweke upande.

Mchuzi Wa Nazi

Vitunguu maji – katakata vidogodogo - 4

Nyanya zilizosagwa (crushed) - 3- 4

Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Bizari ya mchuzi - 1 kijiko cha chai

Bamia zilizokatwa ndogo ndogo - 2 vikombe

Chumvi - kiasi

Ndimu - 2 vijiko vya supu

Tui la nazi - 3 Vikombe au 800 ml

Namna Ya Kupika

Katika karai au sufuria, tia mafuta ukaange vitunguu hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya zilizosagwa, nyanya kopo, uendelee kukaanga, kisha tia bizari, chumvi.
Tia nazi na mwisho tia bamia uache ziwive kidogo tu.
Tia vipande vya samaki vilivyokwisha kaangwa.
Tayari kuliwa na mseto upendavyo.

Vidokezo:

Bizari nzuri kutumia ni ya 'Simba Mbili' inaleta ladha nzuri katika mchuzi.
Ni bora kupika mchuzi kwanza kabla ya mseto kwani mseto ukikaa kwa muda unazidi kukauka.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

Vipimo Vya Wali

Mchele wa Basmati/Pishori - 1 kilo moja

Vitunguu maji - 3

Kar... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu

Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu

Mahitaji

Mchele wa Par boiled au basmati - 5 vikombe

Nyama kondoo/mbuzi ya kusaga -... Read More

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 Vikombe

Dengu - 2 vikombe

Viazi - 3 vikubwaRead More

Jinsi ya kupika wali wa Tuna (samaki/jodari)

Jinsi ya kupika wali wa Tuna (samaki/jodari)

VIAMBAUPISHI VYA TUNA

Tuna (samaki/jodari) - 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) - 4

<... Read More
Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Vipimo - Mahitaji Ya Nyama

Nyama ya n’gombe ya mifupa - 3 lb

Tangawizi mbichi il... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

MAHITAJI

Mchele Basmati - Mugs 2 ½

Vitunguu (Vikubwa kiasi) - 3

Tuna - Vibat... Read More

Jinsi ya kupika vitumbua inavyotakiwa

Jinsi ya kupika vitumbua inavyotakiwa

Mahitaji

Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa)
Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa)
H... Read More

Mapishi ya wali wa mboga

Mapishi ya wali wa mboga

Mahitaji

Wali uliopikwa (cooked rice) kiasi
Hoho la kijani (green pepper) 1/2
H... Read More

Jinsi ya kupika Magimbi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Jinsi ya kupika Magimbi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Vipimo

Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7

Nyama ng’ombe ½ kilos

Tangawizi ilosa... Read More

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mahitaji

Kambale 2
Nazi kopo 1
Nyanya kopo 1
Vitunguu 2
Curry powder ... Read More

Mapishi ya choroko

Mapishi ya choroko

Mahitaji

Choroko kikombe 1 na nusu
Nazi kopo 1
Kitunguu kikubwa 1
Nyanya 1... Read More

Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mahitaji

Maini (Cow liver) 1/4 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2
Nyanya (chopped ... Read More