Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Featured Image

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako, ukachagua Mapadri wawe Wachungaji na Viongozi wa roho za watu. Nakuomba sana; ubariki nia na bidii inayowapasa Mapadri wote katika kazi zao. Uwaongezee Utakatifu.

Uwatie moyo mzuri wenye mapendo makubwa kwako na roho za watu. Hivyo wakiisha kupata wenyewe Utakatifu, waweze kuwaongoza vizuri watu walio chini ya ulinzi wao, katika njia ya Utakatifu na furaha ya milele. Uwajalie neema zote za hali ya Upadri. Uwajalie ili waonyeshe kila siku ya maisha yao mfano wa kila fadhila ya mapendo na ya uaminifu katika Kanisa, kwa Baba Mtakatifu na kwa Maaskofu.

Yesu mpendelevu, uangalie kwa mapendo kazi na mateso ya Mapadri wako; ubariki na ustawishe mafundisho yao; wanapowafundisha watoto, wanapowahubiria watu, wanapowatuliza wakosefu watubu na wanapowasaidia wagonjwa na wale wanaokaribia mauti, Ee Yesu uwe pamoja nao. Uwakinge na hatari zote za roho na za mwili.

Mwokozi Yesu, ulijalie Kanisa liwe na Mapadri wengi walio Watakatifu. Uwajalie watoto na vijana wengi wasikie wito wa Upadri, uwatie furaha na Utakatifu na roho za Mapadri waliokufa uzijalie punziko la amani.

Kwa mimi mwenyewe Ee Yesu mpendelevu, naomba unijalie roho ya imani na utii mnyenyekevu ili niwaheshimu Mapadri kama Mawakili wa Mungu. Niwatii katika njia zote za wokovu wa roho yangu. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Faith Kariuki (Guest) on August 20, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Nancy Kabura (Guest) on August 16, 2017

πŸ™πŸ™πŸ™

Elizabeth Mtei (Guest) on July 17, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Sarah Achieng (Guest) on June 22, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Peter Mwambui (Guest) on June 12, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Grace Majaliwa (Guest) on May 23, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Lucy Mushi (Guest) on March 29, 2017

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Anna Sumari (Guest) on December 31, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Peter Mwambui (Guest) on November 5, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

James Malima (Guest) on October 31, 2016

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Irene Akoth (Guest) on August 5, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

James Malima (Guest) on July 24, 2016

Baraka kwako na familia yako.

Joyce Nkya (Guest) on July 5, 2016

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Grace Mushi (Guest) on May 17, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Grace Njuguna (Guest) on May 9, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Christopher Oloo (Guest) on February 17, 2016

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Mary Kendi (Guest) on January 6, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

John Lissu (Guest) on January 6, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Agnes Lowassa (Guest) on November 14, 2015

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Sharon Kibiru (Guest) on September 4, 2015

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Anna Mahiga (Guest) on July 11, 2015

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Irene Makena (Guest) on June 28, 2015

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Joseph Njoroge (Guest) on June 7, 2015

Rehema hushinda hukumu

Related Posts

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

Sala ya Saa Tisa

Sala ya Saa Tisa

✝⌚✝

Sala ya saa tisaπŸ™πŸΎ

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.... Read More

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote... Read More

Malkia wa Mbingu

Malkia wa Mbingu

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya. Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya. Amefufuka alivyosema, A... Read More

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto... Read More

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA YA MAPENDO

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu,

nakupenda zaidi ya cho chote,

kwani ndiwe mwema,

ndiwe mwenye kupe... Read More

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu ... Read More