Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Wali:
Mchele mpunga - 4 Vikombe
Tui la nazi - 6 vikombe
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele weka kando. Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi. Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.
Maharage Ya Nazi
Maharage - 3 vikombe
Tui la nazi zito - 1 kikombe
Tui la nazi jepesi - 1 kikombe
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa -1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha maharage mpaka yaive. Katiakatia kitunguu maji na tia thomu, tia na tui jepesi kikombe kimoja. Tia tui zito endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi yakaribie kukauka yakiwa tayari.
Samaki Nguru Wa Kukaanga
Samaki Wa Nguru - 4 vipande
Kitunguu saumu(thomu/galic) & tangawizi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi - 4
Ndimu - 2 kamua
Bizari ya samaki -1 kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki. Mwache akolee viungo kwa muda kidogo. Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Maini ya kuku 1/2 kilo Vitunguu vikubwa 2 Hoho 1 Pilipil 1 Limao 1/2 Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chai Curry powder 1/2 kijiko cha chai Mafuta ya kupikia
Matayarisho
Safisha maini weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu,swaum na tangawizi pamoja (hakikisha vitunguu visiwe vya brown), kisha tia maini, curry powder, pilipili, chumvi ,hoho na limao kisha changanya vizuri na ufunike. Pika mpaka maini yaive na hakikisha yanakuwa na rojo kidogo. Baada ya hapo ipua na yatakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama vile chapati, chips, ugali, wali.
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Blue band vijiko vikubwa 2 Maziwa vikombe 2 Royco kijiko kikubwa 1-2 Pilipili manga (unga) kijiko cha 1 Chumvi kiasi Maji lita 2-3 Boga kipande ½ Viazi mviringo 2 Vitunguu 2 Karoti 2 Nyanya 2
Hatua
• Menya boga, viazi, karoti, nyanya na kwaruza weka kwenya sufuria kubwa. • Menya, osha na katakata vitunguu kisha ongeza kwenye mboga. • Ongeza maji na chumvi chemshwa mpaka vilainike. • Pekecha ikiwa jikoni na moto kidogo • Ongeza blue band, maziwa royco na pilipili manga ukikoroga kwa dakika 5. • Onja chumvi na pakua kama supu. Uwezekano Tumia siagi badala ya margarine.
Updated at: 2024-05-25 10:34:51 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga 1 Magi (vikombe vya chai)
Sukari ya browni ½ Magi
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Nazi iliyokunwa ½ Magi
Mjazo wa karameli (Caramel filling)
Syrup 1/3 kikombe cha chai
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Maziwa matamu ya mgando 2 vikopo (condensed milk)
Mjazo wa chokoleti (Chocolate filling)
Chokoleti 185 g (dark chocolate)
Mafuta 3 Vijiko vya chai
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Changanya unga, sukari, siagi na nazi iliyokunwa kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.
2. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in) unaweza kuweka karatasi ya kuchomea chini ukipenda.
3. Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa dakika 15 mpaka 18 au mpaka ibadilike kuwa rangi ya browni.
4. Kwenye sufuria ndogo tia syrup siagi na maziwa matamu ya mgando na changanya kwa moto mdogo mpaka uwe mzito kasha mimina juu ya keki uliyochoma na choma tena kwa muda wa dakika 20 mpaka karameli iwe rangi ya dhahabu.
5. Kwenye sufuria ndogo nyingine tia vipande vya chokoleti na mafuta na ukoroge kwa moto mdogo mpaka iyayuke kisha wacha ipoe kidogo mimina juu ya mjazo wa karameli kisha weka kwenye friji mpaka ishikamane.
6. Kata vipande weka kwenye sahani tiyari kwa kuliwa
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele basmati, pishori - 3 vikombe
Vitunguu katakata - 2
Nyanya/tungule katakata - 5 takriban
Viazi/mbatata menya katakata - 3 kiasi
Thomu (saumu/garlic) ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha kulia
Hiliki ya unga - ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu - 2
Chumvi - kisia
Mafuta - ½ kikombe
Maji ya moto au supu - 5 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha na roweka mchele Katika sufuria weka mafuta yashike moto, tia viazi, vitunguu ukaange. Vikianza tu kugeuka rangi tia thomu na bizari, hiliki, endelea kukaanga kidogo. Tia nyanya kaanga lakini usiache zikavurugika sana. Tia mchele ukaange chini ya dakika moja. Tia maji ya moto, na kidonge cha supu au supu yoyote kiasi cha kufunika mchele yazidi kidogo. Koroga vichanganyike vitu, kisha funika upike kama pilau. Pakua ikiwa tayari, tolea kwa samaki wa kukaanga au kitoweo chochote kile
Updated at: 2024-05-25 10:34:47 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vyakula vingine. Inawezekana ni kutokana na watu wengi kutoelewa namna ya kuoika chakula hiki kutokana na kuhitaji viungo vingi ambavyo huwapa usumbufu wapishi. Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi. Biriani la mbogamboga ni miongoni mwa aina hizo za upishi. Chakula hiki kinaweza kuliwa na kila mtu hususan wale wasiotumia nyama wala samaki.
Mahitaji:
½ kg mchele wa basmati Kitunguu maji kikubwa 1 Nyanya 1 kubwa Karoti 1 kubwa Njegere robo kikombe Kiazi ulaya 1 kikubwa Tangawizi za kusaga kijiko 1 Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1 Karafuu kijiko 1 Majani ya kotimili fungu 1 Maziwa ya mtingi ¼ kikombe Chumvi na pilipili kiasi Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani Mafua ¼ lita
Maandalizi:
Chemsha mchele na kisha weka pembeni Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30 Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa
Updated at: 2024-05-25 10:34:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Ndizi mbichi - 10
Nyama - kilo 1
Nazi ya kopo - 1
Chumvi - 1 Kijiko cha chakula
Ndimu - 1
Bizari ya manjano - 1 Kijiko cha chai
Pili pili mbichi - 3
Nyanya (tomatoes) - 2
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chakula
Namna ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande na uisafishe. Chemsha nyama weka chumvi, thomu, tangawizi na ndimu. Iache iwive. Kata kata nyanya na kitunguu, kisha mimina kwenye nyama inayochemka, weka na bizari nusu kijiko. Wacha supu iwive kisha weka pembeni. Ukumbusho: Hakikisha supu inakuwa kiasi na si nyingi. Menya maganda ndizi na uzikate vipande vipande vya kiasi. Zikoshe ndizi na uziweke ndani ya sufuria. Weka maji ndani ya sufuria kisha zichemshe ndizi mpaka ziwe laini kidogo. Zimwage maji ndizi kisha mimina supu na nyama ndani ya ndizi. Mimina nazi pili pili na bizari nusu kijiko ndani ya ndizi na uziweke kwenye jiko zichemke mpaka zibakie na urojo kiasi. Onja chumvi na uongeze kadri utakavyopenda. Weka pembeni zipoe. Pakua ndizi kwenye sahani au bakuli tayari kwa kuliwa.
Chemsha nyama na chumvi na nusu ya limao mpaka iive kisha weka pembeni. Baada ya hapo andaa vitu vya pilau kwa kuloweka mchele kwenye maji kwa muda wa dakika 10.Menya na kukatakata vitunguu na viazi kisha weka pembeni na pia chemsha maji ya moto na uweke pembeni. Baada ya hapo weka sufuri jikoni na tia mafuta kiasi . Yakisha pata moto tia vitunguu na uvikaange mpaka viwe vya rangi ya kahawia na kisha uitie nyama na ikaange mpaka ipate rangi ya bown pia. Baada ya hapo tia kitunguu swaum na tangawizi na uikoroge vizuri kisha iache ikaangike kwa muda wa dakika 2 kisha tia spice ambazo ni Binzari nyembamba ya unga, hiliki,karafuu, amdalasini na pilipili mtama na viazi. Baada ya hapo unatakiwa ugeuze geuze mpaka mchanganyiko uchanganyike vizuri kisha tia mchele na ugeuzege mpaka uchanganyike na viungo. Baada ya hapo tia chumvi na maji ya kutosha na ukoroge vizuri kisha funika na uache uchemke katika moto wa wastani. Maji yakikaribia kukauka tia binzari nyembamba nzima na ufunike uache mpaka maji yakauke kabisa. maji yakisha kauka ugeuze na ufunike tena na uuache mpaka uive. Baada ya hapo andaa kachumbali kwa kukatakata vitunguu katika bakuli na kisha tia chumvi kwa ajili ya kuondoa ukali wa vitunguu. Baada ya hapo vioshe mpaka chumvi yote iishe. osha nyanya, Pilipili, hoho na kisha katakata slice nyembamba na uchanganye na vitunguu. Baada ya hapo tia chumvi, kamulia limao na uchanganye zote pamoja. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuliwa.
Jinsi ya kupika Cookies Za Jam Ya Peach Na Raspberry
Updated at: 2024-05-25 10:34:43 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga kikombe 1 ½
Siagi ½ kikombe
Sukari ½ kikombe
Yai 1
Vanilla 1 kijiko cha chai
Jam ya peach na raspberry
MAANDALIZI
Wash oven moto wa takriban 180 – 190 Deg F Piga siagi na sukari katika mashine mpaka iwe laini na nyororo (creamy) kisha weka yai na vanilla. Tia unga kidogo kidogo uchanganye kwa mwiko wa mbao (wooden spoon). Pakaza mkononi unga uchukue vidonge ubonyeze kufanya vishimo vya kuwekea jam. Panga katika treya uliyopakaza siagi. Tia nusu yake jam ya peach na nusu jam ya raspberry Bake katika oven kiasi robo saa mpaka ziwive na kugeuka rangi ya brown light. Epua vikiwa tayari
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 2 Vikombe Sukari ya icing - 1 Kikombe Siagi - 250 gm Yai - 1 Vanilla - 2 Vijiko vya chai Baking powder -1 Kijiko cha chai Jam - ¼ kikombe Lozi - ¼ kikombe
JINSI YA KUPIKA
Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy). Tia yai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini kama sufi. Tia unga na baking powder changanya na mwiko. Chota mchanganyiko kwa mkono (kiasi cha kijiko kimoja cha supufanya duara kisha weka kwenye treya ya kupikia. Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam na tupia lozi zilizomenywa na kukatwa katwa. Pika (bake) katika oven moto wa 375° F kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama