Updated at: 2024-05-25 09:52:20 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa) Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa) Hamira ( Nusu ya kijiko cha chai) Hiliki (Nusu ya kijiko cha chai) Tui la nazi ( Kikombe kimoja kikubwa) Unga wa ngano (Vijiko viwili vya chakula) Mafuta ya kuchomea (Vegetable oil)
Matayarisho
Unachanga unga, sukari, hamira, hiliki, unga wa ngano na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastiki. Kisha unaukoroga mpaka mchanganyiko unakuwa kama uji mzito. Kava bakuli lililokuwa na mchanganyiko kisha hifadhi katika sehemu yenye joto kwa muda wa masaa matatu.
Jinsi ya kupika
Weka chuma cha kuchomea vitumbua katika moto wa wastani, kisha weka mafuta kwenye chuma cha kuchomea ( Kijiko kimoja cha chai) mafuta yakisha pata moto tia uji wako (upawa mmoja) katika kila shimo la chuma cha kuchomea. Acha mpaka kitumbua kikauke kisha geuza na tia mafuta. Acha upande wa pili wa kitumbua mpaka uwe rangi ya kahawia na hapo kitumbua kitakuwa kimeiva utakitoa. Rudia hatua hizo kwa vitumbua vyote vilivyobaki.
Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Wali:
Mchele mpunga - 4 Vikombe
Tui la nazi - 6 vikombe
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele weka kando. Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi. Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.
Maharage Ya Nazi
Maharage - 3 vikombe
Tui la nazi zito - 1 kikombe
Tui la nazi jepesi - 1 kikombe
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa -1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha maharage mpaka yaive. Katiakatia kitunguu maji na tia thomu, tia na tui jepesi kikombe kimoja. Tia tui zito endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi yakaribie kukauka yakiwa tayari.
Samaki Nguru Wa Kukaanga
Samaki Wa Nguru - 4 vipande
Kitunguu saumu(thomu/galic) & tangawizi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi - 4
Ndimu - 2 kamua
Bizari ya samaki -1 kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki. Mwache akolee viungo kwa muda kidogo. Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7
Nyama ng’ombe ½ kilos
Tangawizi ilosagwa 1 kijiko cha kulia
Haldi (bizari manjano/turmeric) ½ kijiko cha chai
Tui zito la nazi vikombe 2
Chumvi kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Safisha nyama kisha weka chumvi, bizari ya manjano, tangawizi mbichi, ukaushe kwanza katika sufuria kwa kukaanga kaanga. Ikianza kukauka, weka maji funika uchemshe iwive. Menya majimbi ukate kate na uweke katika sufuria nyengine. Mimina supu na nyama katika majimbi uchemshe yawive majimbi. Mwisho weka tui zito la nazi uchanganye vizuri kisha weka katika moto kidogo tu bila kufunika yakiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:23:14 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele - 1 kilo
Kuku - 1
Vitunguu - 3
Viazi/mbatata - 5
Jira/bizari ya pilau nzima - 3 vijiko vya supu
Mdalasini - 1 kijiti
Pilipili manga - 1 kijiko cha supu
Hiliki - 3 chembe
Karafuu - 5 chembe
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 3 vijiko vya supu
Tangawizi mbichi ilosagwa - 3 vijiko vya supu
Mafuta ya kupikia - ½ kikombe
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Baada ya kumsafisha kuku na kumkatakata, mchemshe kwa chumvi na ndimu, kijiko kimoja cha kitunguu thomu/somu na tangawizi yote.. Menya viazi, katakata vipande vya kiasi. Katakata vitunguu maji kisha kaanga kwa mafuta katika sufuria ya kupikia pilau. Tia bizari zote isipokuwa hiliki. Saga hiliki kisha tia pamoja na kitunguu thomu/somu ukaange kidogo. Mimina kuku na supu yake ikichemka kisha tia mchele na viazi. Koroga kisha acha katika moto mdogomdogo wali uwive kama kawaida ya kupika pilau.
2. Unaweza kutwanga kwa kutumia kinu au kuchemsha kidogo na kisha kusaga kwa kutumia mashine. Ukitumia mashine uwe makini usije ukasaga sana ukaharibu.
3. Kaanga karanga kidogo na kisha zisage ziwe unga unga.
4. Chemsha kisamvu chako hadi kiive.
5. Katakata kitunguu, karoti na na nyanya
6. Anza kuunga kisamvu kwa kukaanga vitunguu, weka karoti na kisha nyanya na vikishaiva weka kisamvu na koroga pamoja kisha weka karanga. Acha vichemke kwa muda na unaweza pia weka na nazi tui la kwanza.
7. Baada ya muda mfupi epua na kitakiwa tayari. Waweza kula kwa ugali, wali, chapati, makande n.k
Mapishi ya Ugali Mchuzi Wa Samaki Nguru Wa Nazi Na Bamia Za Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo Vya Ugali:
Unga wa mahindi/sembe - 4
Maji - 6 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chota unga kidogo katika kibakuli uchanganye na maji kidogo . Weka maji mengineyo katika sufuria kwenye moto. Changanya na mchanganyiko mdogo ufanya kama uji. Kisha kidogo kidogo unaongeza sembe huku unakoroga na kuusonga ugali hadi uive.
Vipimo Vya Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi
Samaki nguru - 5 vipande
Pilipili mbichi ilosagwa
Kitunguu maji kilosagwa - 1 kimoja
Nyanya ilosagwa - 2
Haldi/tumeric/bizari ya manjano - ¼ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Ndimu - 2 kamua
Tui la nazi zito - 2 vikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Baada ya kumuosha samaki, weka katika sufuria. Tia chumvi, ndimu, pilipili mbichi ilosagwa. Tia vitunguu na nyanya zilosagwa Mkaushe kwa hivyo viungo, akianza kukauka tia tui la nazi. Acha kidogo tu katika moto tui liwive mchuzi ukiwa tayari.
Vipimo Vya Bamia
Bamia - ½ kilo takriban
Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai
Methi/uwatu/fenugreek seeds ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Dania/corriander ilosagwa - ½ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Mafuta - 1 kikombe cha kahawa
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata bamia kwa urefu. Weka mafuta katika karai, kisha tia bizari zote na nyanya kopo, kaanga kidogo. Tia bamia endelea kukaanga, kisha acha katika moto mdogomdogo ufunike. Kila baada ya muda funua karai ukaange bamia hadi ziwive zikiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:34:46 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
1 kilo unga wa ngano 240 ml maji ya vugu vugu 2 olive oil kijiko kikubwa cha chakula 2 asali kijiko kidogo cha chai 1 chumvi kijiko kidogo cha chai 1 hamira ya chenga kijiko kidogo cha chai
JINSI YA KUPIKA
Chukua bakuli weka maji ya uvugu vugu, amira ya chenga, asali na chumvi kisha koroga ichanganyike vizuri acha itulie kwa dakika 10. Kisha chukua olive oil na unga wa ngao mimina kidogo kidogo changanya mpaka ichanganyike safi kabisa kisha anza kukanda kama mchanganyiko wa chapati au maandazi. Baada ya mchanganyiko wako kua mgumu safi kabisa funika bakuli lako na mfuko wa plastiki au cling film kwa muda wa saa 1 katika joto la chumba na mchanganyiko wako utaumuka baada ya muda huo. kisha ukandamize mchanganyiko huo wa unga na kua flati kama mwanzo. Kata mafungu matano hadi saba ya ujazo sawa inategemea na ukubwa wa piza unaopenda we mlaji kisha sukuma umbo la duara. Tengeneza mchuzi mzito wa nyanya kisha weka juu ya kitako cha piza na kuitandaza vizuri kwenye pizza yako kama unavyopaka siagi kwenye mkate. Usisahau kuweka chumvi na sukari kidogo katika mchuzi wa nyanya ili kukata uchachu. Katakata nyanya, kitunguu, pili pili hoho, na bilinganya na kuziweka juu ya pizza yako kwa mpangilio ukitanguliza biringanya, ikifuatiwa na pili pili hoho, kitunguu maji na nyanya. Kisha chukua mozarella cheese ikwaruze katika mkato mdogo rahisi kuyeyuka kwa kutumia kwaruzo la karoti linafaa. kisha chukua mkwaruzo wa mozarella cheese na unyunyizie juu ya hizo mboga. Weka pizza yako kwenye sahani ya bati au pizza pan ili isaidie kuiva upande wa chini. Weka pizza yako kwenye oven ambayo imeshawashwa na ina joto 400 - 450 F. Choma kwa dakika 20 hadi 25 iwe kaukau na rangi ya kahawia pia cheese itakua imyeyuka na kusambaa vizuri juu ya pizaa.
NB: Unaweza weka mchanganyiko wa nyama yeyote ile kama salami, nyama ya ngombe, nyama ya kuku au samaki kwa kufata maelekezo sawa sawa na hii piza ya mboga, tofauti yake itakua huweki mboga unaweka nyama.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele (rice vikombe 2 na 1/2) Vitunguu (onion 2) Nyanya ya kopo (tin tomato kopo 1) Tangawizi (ginger paste kijiko 1 cha chakula) Kitunguu swaum (garlic paste kijiko 1 cha chakula) Paprika (kijiko 1 na 1/2 cha cha chai) Pilipil (scotch bonnet pepper 1) Curry powder (kijiko 1 cha chai) Maggi cubes 3(unaweza kutumia yenye ladha ya chicken, beef au vegetable. Inategemea unasevu na mchuzi wa aina gani) Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Loweka mchele kwa muda wa dakika 10.Katakata vitunguu kisha weka pembeni, saga pamoja nyanya ya kopo,pilipili, tangawizi na kitunguu swaum kisha weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu vikiiva tia curry powder, maggi cubes, chumvi na paprika na uchanganye vizuri. Kisha tia mchanganyiko wa nyanya na uupike mpaka uive. Baada ya hapo tia mchele na maji na uupike mpaka ukaribie kuiva kisha ugeuze na umalizie kwa kutia njegere na umalizie kuupika mpaka uive. baada ya hapo utakuwa tayari kuseviwa na mboga yoyote kama kuku, nyama, samaki au assorted meat (Mchanganyiko wa utumbo, makongoro na nyama), Hapo mimi nili-save na mchuzi wa kuku wa kienyeji.
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Maziwa mazito matamu (condensed milk) - 2 vibati
Sukari - 1 kikombe
Samli 1 ½ kikombe
Vanilla 2 kifuniko cha chupa yake
Hiliki ilosagwa - 2 vijiko vya chai
Sinia kubwa ya bati Paka samli
MAANDALIZI
Changanya maziwa, sukari na samli katika sufuria isiyogandisha chakula (non-stick) uweke katika moto. Koroga huku ikipikika hadi ianze kugeuka rangi na kuanza kuachana. Usiache mkono kuroga isije kufanya madonge. Tia hiliki na vanilla, endelea kuipika. Itakapogeuka rangi vizuri mimina katika sinia na haraka uitandaze kwa mwiko huku ukiuchovya katika maji na kuendelea kuitandaza hadi ikae sawa kote. Pitisha kisu kuikataka ili ikipoa iwe wepesi kuitoa vipande.
Kila inapozidi kupoa na kukaa ndipo fagi inakauka na kumumunyuka.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mihogo kilo 1 Kidali cha kuku 1 kikubwa Nyanya 1 kubwa Kitunguu maji 1 cha wastani Swaum/tangawizi i kijiko cha chai Nazi kopo 1 curry powder 1 kijiko cha chai Binzari manjano 1/2 kijiko cha chai Limao 1/2 Pilipili 1 Chumvi kiasi
Matayarisho
Saga pamoja nyanya, kitunguu na swaum/ginger pamoja na vimaji kidogo. Kisha vitie kwenye sufuria isiyoshika chini na uvishemshe mpaka maji yote yakauke kisha tia mafuta na upike ktk moto mdogo mpaka viive.Baada ya hapo tia spice na uzipike kidogo kisha tia mihogo na kuku (kuku na mihogo vikatwe vipande vya wastani) vichanganye vizuri kisha tia nazi na vimaji kiasi,limao chumvi na pilipili na ufunike kisha punguza moto. Pika mpaka mihogo na kuku viive na ibaki rojo kidogo kisha ipua na mihogo yako itakuwa tayari kwa kuliwa