Updated at: 2024-05-25 10:34:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Leo tunaangalia mapishi ya fish finger ( sijui kama unaweza kusema kidole cha samaki)!, Ni mlo mzuri hasa kuliwa kama kitafunio au mboga ya pembeni.
Mahitaji
500g Fileti ya samaki 120g Chenga za mkate 100g Unga wa ngano Mayai 2 Ndimu 1 Kitunguu saumu 1 Kotmiri Mafuta ya kupikia
Matayarisho
Menya vitunguu saumu kisha visage
Katakata fileti kwa muundo wa mraba (kama vidole) kisha paka mchanganyiko wa vitunguu saumu
Kata ndimu na kamulia kwenye fillet yako
Weka chenga za mkate kwenye bakuli kisha uchanganye chumvi kiasi na kata kata kotmiri majani 3 na uchanganye pamoja.
Kwenye bakuli lingine weka mayai na uyapigepige yawe kama uji mzito
Weka unga kwenye bakuli jingine.
Chukua kipande cha fillet kiweke unga kidogo kisha kizamishe kwenye yai na baada ya hapo kizamishe kwenye mchanganyiko wa chenga za mkate. Fanya hivyo kwa vipande vyote.
Weka mafuta kwenye kikaago na subiri yachemke kisha weka fillet zako vizuri na zikaange pande zote hadi zimekuwa rangi ya brown ( hakikisha moto sio mkali sana).
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Mchele - 3 vikombe
Nyama ya kusaga - 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka upendazo; maharagwe, njegere, mbaazi n.k 1 mug
Vitunguu maji kata vipande vipande - 3 vya kiasi
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 vijiko vya supu
Mafuta - Β½ Kikombe
Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) - 2 vijiko vya chai
Vipande vya supu (Maggi cubes) - 3
Maji (inategemea mchele) - 5
Chumvi - Kiasi
MAPISHI
Osha mchele na roweka. Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown. Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo. Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive. Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo. Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo. Tia mchele, koroga kidogo. Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15. *Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil. Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Kabichi 1/2 kilo Nyanya ya kopo 1/2 Kitunguu 1 Curry powder 1/2 kijiko cha chai Chumvi Olive oil
Matayarisho
Kwanza kabisa bandua magada ya juu ya kabichi, kisha ioshe na uikaushe maji baaba ya hapo katakata kabichi (inapendeza zaidi kama ikikatwa nyembamba) kisha saga pamoja nyanya na kitunguu. Baada yahapo tia katika sufuria ya kupikia, ipike mpaka maji yote yatakapokauka kisha tia chumvi, curry powder na mafuta pika kwa muda kiasi kisha tia kabichi na upunguze moto. Pika mpaka kabishi itakapoiva kisha ipua na itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuila kwa wali au ugali.
Updated at: 2024-05-25 10:23:07 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 3 Vikombe
Sukari ya unga (icing sugar) 1 Kikombe
Siagi 250 gm
Mayai 3
Vanilla 2 Vijiko vya chai
Baking powder 1 Kijiko cha chai
JINSI YA KUPIKA
Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy). Tia mayai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini. Tia unga na baking powder changanya na mwiko. Tengeneza round upange kwenye tray utie nukta ya rangi. Nyunyuzia sukari juu ya hizo round ulizotengeneza kabla huja choma. Pika (bake) katika oven moto wa 350Β°F kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele - 2 Mugs
Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) - Mug
Tuna (samaki/jodari) - 2 kopo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi -2 vijiko vya supu
Garam masala - 1 kijiko cha supu
Nyanya - 2
Kitungu maji - 1
Mdalasini nzima - 2 vijiti
Karafuu - 6 chembe
Pilipili mbichi - 1
Chumvi - kiasi
Viazi - 3
Maji - 2 Β½ Mugs
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Maandalizi
Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20 Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Mimina viazi, thomu na tangawizi, bizari zote na kaanga. Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive. Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu. Tia maji, yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa Β½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:56 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Β· Osha mikono yako kwa sabuni kabla na baada ya kutayarisha chakula Β· Tumia vyombo safi na sehemu safi kwa kutayarisha na kula chakula Β· Viporo vipashwe moto vizuri kabla ya kula Β· Chemsha maji ya kunywa na kuyaacha jikoni dakika kumi baada ya kuchemka
Updated at: 2024-05-25 10:37:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Dagaa waliokaushwa (dried anchovy 2 kikombe cha chai) Bamia (okra 5) Nyanya chungu (garden egg 5) Tui la nazi (coconut milk 1 kikombe cha chai) Nyanya (fresh tomato 2) Kitunguu (onion 1) Curry powder 1/2 ya kijiko cha chai Turmeric powder 1/2 kijiko cha chai Limao (lemon 1/2) Chumvi (salt kiasi) Pilipili (scotch bonnet 1) Mafuta (veg oil)
Matayarisho
Safisha dagaa na uwaweke pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia dagaa wakaange kidogo kisha tia chumvi, pilipili, curry powder, turmeric, bamia na nyanya chungu, koroga vizuri mpaka mchanganyiko wote uchanganyike vizuri kisha tia nyanya na ufunike. Pika mpaka nyanya iive kisha kamulia limao,na pia hakikisha nyanya chungu na bamia zimeiva kidogo(usiache mpaka ziive sana manake zitavurugika pindi utakapotia tui la nazi) kisha malizia kwa kutia tui la nazi na uache lichemke mpaka rojo ibakie kidogo. Hakikisha nyanya chungu na bamia zimeiva ndo uipue. Na hapo dagaa wako watakuwa tayari kwa kuliwa na wali au ugali.
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kupika tambi ni kama ifuatavyo
VIAMBA UPISHI
Tambi pakti moja
Sukari ΒΎ kikombe cha chai
Mafuta Β½ kikombe cha chai
Iliki kiasi
Maji 3 Vikombe vya chai
Vanilla / Arki rose 1-2 Tone
Zabibu Kiasi (Ukipenda)
JINSI YA KUPIKA TAMBI ZAKO
1. Zichambue tambi ziwe moja moja.
2. Mimina mafuta kwenye sufuria yakisha pata moto mimina tambi,zigeuzegeuze mpaka zibadilike rangi na kuwa brown.
3. Punguza mafuta kwa kuyachuja na zirudishe jikoni.
4. Nyunyizia iliki zilizosagwa koroga kidogo na mimina maji na tia arki na acha zichemke mpaka maji yakikaribia kukauka mimina sukari koroga kidogo na punguza moto. 5. Kisha tia zabibu ukipenda, zifunike ili zikaukie vizuri.
6. Zikishakauka pakua kwenye sahani tayari kwa kuliwa
Kidokezi: Itategemea na aina za Tambi unazopika kwa kukisia maji, kama utaona hazijaiva unaweza kuongeza maji kidogo.
Updated at: 2024-05-25 10:22:14 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuandaa Chakula kwa Kupunguza Uzito: Vidokezo na Mapishi π½οΈπͺ
Kupunguza uzito ni lengo ambalo wengi wetu tunalipigia debe, lakini mara nyingi tunapata changamoto kubwa ya jinsi ya kuandaa chakula kinachosaidia katika mchakato huu. Kwa bahati nzuri, kuna njia nyingi za kuandaa chakula ambazo zitakusaidia kufikia lengo lako la kupunguza uzito. Katika makala hii, nitaenda kukushauri jinsi ya kuandaa chakula kinachofaa kwa ajili ya kupunguza uzito wako. Kama AckySHINE, mtaalam katika masuala haya, ninafahamu jinsi ya kukusaidia kupata matokeo bora.
Hapa kuna vidokezo vya jinsi ya kuandaa chakula kwa kupunguza uzito na mapishi ambayo yatakuwezesha kufurahia chakula chenye afya na bado ufikie lengo lako la kupunguza uzito.
Chagua vyakula vyenye kiwango cha chini cha mafuta: Ni muhimu kuzingatia kiwango cha mafuta katika chakula chako. Badala ya kukaanga, jaribu kupika kwa kutumia njia kama kuchemsha, kuchoma au kupika kwa mvuke. π₯¦π
Punguza matumizi ya sukari: Sukari ni tishio kubwa katika mchakato wa kupunguza uzito. Badala ya kutumia sukari ya kawaida, jaribu kutumia mbadala kama vile asali au sukari mbadala yenye kiwango cha chini cha kalori. π―π°
Ongeza mboga kwenye milo yako: Mboga ni tajiri katika virutubisho na hupunguza kalori katika mlo wako. Hakikisha unaongeza mboga kwenye sahani yako ili kuongeza ladha na thamani ya lishe ya chakula chako. π₯π₯¬
Pika kwa kutumia viungo vya asili: Kuandaa chakula chako mwenyewe kunakupa udhibiti wa viungo unavyotumia. Tumia viungo vya asili kama vile tangawizi, vitunguu, pilipili, na viungo vingine vyenye afya ili kuongeza ladha bila ya kuongeza kalori nyingi. πΆοΈπ§
Punguza matumizi ya chumvi: Chumvi inaweza kusababisha umeng'enyaji usiofaa na kuongeza shinikizo la damu. Jaribu kutumia chumvi kidogo au badala yake tumia viungo vingine kama vile pilipili, tangawizi na jani la bay kwa ladha zaidi. π§π₯
Pika sahani ndogo: Kula kwa kiasi kidogo kunaweza kukusaidia kupunguza ulaji wako wa kalori. Jaribu kutumia sahani ndogo wakati wa kuandaa chakula chako ili udhibiti kiasi unachokula. π½οΈπ₯
Subiri kabla ya kula tena: Mara nyingi tunapokula, tunahisi kushiba haraka. Kabla ya kukimbilia kula tena, subiri angalau dakika 20 ili kutoa nafasi kwa mwili wako kujua ikiwa umekula vya kutosha. ππββοΈ
Jaribu kupika kwa kutumia mafuta ya asili: Mafuta ya asili kama vile mafuta ya zeituni, mafuta ya alizeti, na mafuta ya avocado yana mafuta yenye afya ambayo yanaweza kukusaidia kupunguza uzito wako. Epuka mafuta ya trans na mafuta ya wanyama. π₯π³
Fanya chakula kiwe na rangi: Chakula chenye rangi nyingi huwa na virutubisho vingi na huongeza hamu ya kula. Jaribu kuchanganya matunda na mboga za rangi tofauti ili kuongeza ladha na mchanganyiko wa lishe katika milo yako. ππ
Kula kwa polepole: Kula polepole kunaweza kukusaidia kuhisi kushiba haraka na kula kwa kiasi kidogo. Chakula huchukua muda kufika kwenye tumbo, kwa hiyo jaribu kula kwa taratibu ili kujisikia kushiba haraka. π’π½οΈ
Epuka vinywaji vyenye sukari: Vinywaji vyenye sukari kama vile soda na juice ya kutoka kwenye pakiti huongeza kiasi kikubwa cha kalori zisizo na faida kwenye lishe yako. Chagua maji, juisi ya limau au chai zisizoongeza sukari. π₯€πΉ
Tumia sahani nyembamba: Kutumia sahani nyembamba kunaweza kukufanya uhisi kama una sahani kamili hata kama umechukua kiasi kidogo cha chakula. Hii inaweza kukusaidia kudhibiti sehemu unazochukua. π½οΈπ
Panga milo yako mapema: Kupanga milo yako mapema kunaweza kukusaidia kuepuka kula chakula kisicho na afya au kupita kiasi. Jipange vizuri na andika orodha ya unachotaka kula kwa kila siku ili kudumisha mpangilio mzuri wa lishe yako. ππ
Usiwe mkali kwako mwenyewe: Kupunguza uzito ni mchakato na hakuna njia ya mkato. Usikate tamaa ikiwa unaanguka kutoka kwenye mstari wako. Badala yake, jikumbushe lengo lako na endelea kujitahidi. Kila hatua ndogo inakaribishwa na inakusaidia kufikia lengo lako la mwisho. πͺπ«
Kwa hiyo, hapa ndio vidokezo na mapishi ya jinsi ya kuandaa chakula kwa kupunguza uzito wako. Kumbuka, chakula ni muhimu katika mchakato huu na inaweza kufanya tofauti kubwa katika matokeo yako. Jaribu vidokezo hivi na uone jinsi yanavyofanya kazi kwako. Je, una vidokezo vyovyote au mapishi unayopenda kutumia wakati wa kupunguza uzito? Tuambie katika sehemu ya maoni hapa chini. π£οΈπ
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 300gm
Siagi 225gm
Icing Sugar 60gm
Chokoleti iliyokoza (Dark Chocolate) - 225gm
Vanilla β Vijiko 2 vya chai
Yai -1
Baking Powder Β½ kijiko cha chai
Njugu za vipande Β½ kikombe cha chai
Njugu zilizosagwa ΒΌ kikombe cha chai
JINSI YA KUTAYARISHA
Piga sukari na siagi katika mashine ya keki mpaka iwe laini Kisha mimina yai na vanilla koroga vizuri Mwisho mimina unga na baking powder polepole mpaka ichanganyike. Kata kata umbo (shape) lolote unavyopenda (kama nyota, pembetatu,duara, kopa n.k) Panga kwenye treya na choma kwa moto wa 350Β°C , vikibadilika rangi kidogo tu vitoe Yayusha chokoleti tia kwenye bakuli ndogo. kisha paka kwa kijiko au chovyea upande mmoja mmoja wa biskuti kisha nyunyizia njugu za kipande na njugu ya unga. Panga kwenye sahani tiyari kunywewa na chai ya maziwa au kahawa.