Makovu sio kidonda naomba hili uelewe, ila makovu ni alama ya majeraha ambayo yamebaki kwenye ngozi baada ya kupona majeraha.
Kuna baadhi ya watu husumbuliwa na shida ya kuwa na makovu sehemu mbalimbali ya mwili.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwao maandishi haya yanakuhusu sana.
Zifuatazo ndizo mbinu za kuondoa makovu mwilini.
1. Tango
Unachotakiwa kufanya ni; Pondaponda tango na kisha kutumia mchanganyiko wake kwa kupaka juu ya kovu. Hii husaidia sana kulainisha makovu na ikiwa utatumia kwa muda mrefu huondoa makovu pia.
2. Aloe vera.
Unachotakiwa kufanya ni; kata majani hayo na utumie utomvu wake kupaka katika makovu kisha mara baada ya muda Fulani utaona mabadiliko na itapunguza na kuondoa makovu.
3. Asali
Unachotakiwa kufanya; Paka asali juu ya kovu na kuiacha usiku kucha. Rudia mara kwa mara kupaka asali hadi pale kovu litakapotoweka.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Mavazi ya Ofisini kwa Wadada
Madhara ya Kujichubua
Jinsi ya kuondoa kitambi Kitaalamu
Faida za kuoga maji ya Baridi
Faida za kuvaa saa ya Mkononi
Matumizi ya Papai Katika Urembo
Mambo ya Kuzingatia ili uwe na ngozi laini
Njia za kutunza nywele zako