Siku moja mwalimu wa shule aliandika ubaoni kama ifuatavyo:
9Γ1=7
9Γ2=18
9Γ3=27
9Γ4=36
9Γ5=45
9Γ6=54
9Γ7=63
9Γ8=72
9Γ9=81
9Γ10=90
Alipo maliza kuandika tu, akaona wanafunzi wote walikua wanamcheka, kwasababu alikua amekosea swali la kwanza.
Mwalimu aliwatazama wanafunzi, kisha akawaambia yafuatayo:
`”Nimejikosesha lile swali la kwanza makusudi, kwasababu nilihitaji mjifunze kitu kimoja muhimu sana. Mnapaswa kujua namna ambavyo dunia inaweza kuwachukulia. Unaona hapo, nimeandika kwa usahihi mswali tisa (9), lakini hakuna kati yenu aliyenipongeza kwa hilo; wote mmecheka na kunilaumu kwasababu ya kosa moja tu nililofanya.”`
Hivyo, hili ni somo kwenu:
`”Dunia haijali mazuri unayofanya hata ukiyafanya mara milioni, lakini fanya baya moja uone jinsi watakavyo kulaumu…”`
“`Hata hivyo usikatetamaa, MARA ZOTE SIMAMA IMARA NA USHINDE VIKWAZO VYOTE.” `
JIAMINI
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Hichi ndicho unatakiwa uwe nacho kulingana na umri wako
Unashangaa kwa nini hufanikiwi?
JITAMBUE : Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana, Anza sasa
Siri 39 za kuwa Milionea, Jinsi ya kupata pesa na kuwa tajiri
Kwa nini watu wanapenda pesa
Kuwa na kawaida ya kujiwekea Akiba ni njia na Siri ya kuwa tajiri
Hii ndio sababu kwa nini huwezi kufanikiwa kibiashara
Ujumbe wa leo kwa mtu anayetaka kufanikiwa katika maisha kiuchumi