Vituko Vya Kukuondoa Mawazo

Usichokijua kuhusu sungura, panya na jamii yao

JE WAJUA?

Sungura, panya na Jamii zao huwa na mwendo wa kukimbia na kuruka muda wote na umri wao wa kuishi ni miaka 15. Kobe ni mnyama mwenda pole, asiye na papara wala pilika, muda mwingi hujificha na kupumzika ndani ya jumba lake akikwepa maadui. Umri wa kuishi kobe hufikia hadi miaka 300.
FUNZO: Mazoezi ni kiinimacho na uongo mtupu. Jipumzikie mwaya!!!
๐Ÿƒ๐Ÿพ๐Ÿƒ๐Ÿฟโ€

Huyu mgeni wa huyu jamaa ni shida

Pale unapokuwa umefulia sanaโ€ฆ

Mgeni anakutembelea Maskani kwakoโ€ฆ.Unaamua Kuchukua Ile Sh 600 iliyobaki na kwenda Dukani Kumnunulia Soda Unaondoka na Chupa Mbili Unanunua Fanta Moja kwaajil ya Mgeni na Ile Chupa ya Sprite Unaijaza Maji ili Ukirudi Uweze kumpa Kampani Mgeniโ€ฆโ€ฆUnafika Seblen Unampa Ile soda ya Fanta Mgeni anakuambia Fanta huwa situmii Nipe hiyo sprite โ€ฆ..Bwanaโ€ฆ.Bwana. โ€ฆBwanaโ€ฆ.Weee ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Soma huyu mtoto anachosema sasa, Ndoto za watoto bwana! Kazi ipo!

Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?

ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe Nehemiah ??
Nehemiah : mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiweโ€ฆโ€ฆ”
Akameza mate kisha akaendeleaโ€ฆ.
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa Nehemiah .!!

Status za Whatsapp za Wazungu na Wabongo

STATUS ZA WAZUNGU kwenye Whatsapp vere vere kliaaaโ€ฆ
๐Ÿ‘‰sick
๐Ÿ‘‰at movie
ย ๐Ÿ‘‰ in a meeting2
๐Ÿ‘‰ kind of happy,, ๐Ÿ‘‰busy,,
๐Ÿ‘‰available
๐Ÿ‘‰Driving
๐Ÿ‘‰sleeping

STATUS ZA WABONGO SASA MBUTA NANGA MBONGO NGAFU

“Akutake nani una shepu la Kitorondo utaishia kumegwa na kuachwa

“Watu tuna nyota za Chips Mayai sio wewe mwenye Nyota ya Punda,halulaaa”

๐Ÿ‘ŒKantangazeee ndo Kwanza naanza na ntakukomesha Mwanaharamu we!

๐Ÿ˜ I love yu so much ur my only one,No one lyk yu and I mean it ๐ŸŽถ Yu ma numba1 ma sweet sweet namba1 roho yangu mama,,

๐Ÿ‘ Asante ๐Ÿ˜ vimenitoshaaa tena kama ulijua ๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜,

๐Ÿ’ช unajifanya simba kumbe nyau mimi ndo maji kama hujanioga utaninywaa,

๐Ÿ™ˆ nauza Ubuyu kwa bei nafuuu kama unataka inbox me plz

๐Ÿ˜” poleee jaman utapona wangu,,,

๐Ÿ’ช utalijua jiji na chuki zako walingia na tako wakati hadi nyani analo kitu sura dadaโ€ฆ

๐Ÿ˜ก usinisemeshe usiniongeleshe tena utaniambia vizur ulikuwa wapi..

๐Ÿ˜ท mdomo kaumbiwa mwanadamu ongeeni nyie me sijali ya wanafiki nafanya yangu huna hadhi ya kujibiwa na mimi
pamoja na ya kwako uloweka๐Ÿ™ˆ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

Angalia huyu ticha wa Hesabu alichofanyiwa

Looku Looku* ๐Ÿ‘€๐Ÿ‘€

*Ama Kweli Mkuki Kwa Nguruwe kwa Binadamu Mchungu Skia Hiiโ€ฆ.!!*

*Ishawahi kutokea Pale nilipokutana njiani na mwalimu aliyekufundisha MATHS secondary afu akaniambia nimuelekeze njia ya kwenda sehemu fulani.*

*_Nenda mbele kama 2KM hivi kisha kata kushoto,ila hakikisha ANGLE inakuwa ni 30.5 KUSINI MASHARIKI.Kisha tumia PYTHAGORAS na hakikisha una FOUR FIGURE ili kupata thamani ya ANGLE._*

*Mwalimu alisonya na kuondoka.*๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜’๐Ÿ˜’

*Stakagi ujinga kabisa mimi, wakati ananichapa alifikiri sifa*๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

๐Ÿ˜…๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ *Mniache Tuu Mimi Sio Kwa Bifu Ilo Aiseee*๐Ÿƒ๐Ÿพ

Angalia hawa kina mama, ni shida..!

Mama mdaku alishangaa kila siku mchungaji anaingia nyumba ya jirani yake ambaye hana mume, akawa anajiuliza anakwenda kufanya nini? Uzalendo ukamshinda akamuuliza “Mwenzangu, mbona kila siku mchungaji anakuja kwako, vipi anakuja kukuombea?” Akajibiwa “Nyoo, umbea tu! Mbona kwako kila siku anakuja mwanajeshi kuna vita! chefuuuu ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Misemo 17 ya kuchekesha

1) gari la kuvutwa halina overtake
2) kisigino hakikakai mbele
3) wimbo wa taifa haupgwi disko
4) feni haiwashwi beach
5) mshkaki hauchomwi kwa jiko la ges
6) mganga haagiz tembele
7) hata bibi alikuwa bint
8) mke wa mtu sumu,mume wamtu maziwa
9) kipara bila pesa ni kovu
10) mbwa hanenepi migiuu
11) picha ya rais haina bodyguard
12) mjini shule kijiji tuition
13) saa ya ukutani haivaliwi mkonon
14) heshima pesa shkamoo makelele
15) ulinz pesa bastora mzgo
16) kuku ni kuku jogoo mbwembwe
17) kusoma kuelewa kukesha mbwembwe

Jinsi mzunguko wa elimu ulivyo

01.๐Ÿ‘‰ Wale wanafunzi walioongoza
Mashuleni, wanaenda kwenye
Engineering na Medical school.

02.๐Ÿ‘‰ Wale waliokuwa wa pili, wanachukua MBA na LLB na kuja kuwa Mameneja wa
wanafunzi walioshika nafasi ya kwanza.

03.๐Ÿ‘‰ Wale waliokuwa wa tatu, wanageukia
Siasa na kuwaongoza wote hapo juu.
Yaani wa kwanza na wa pili.

04.๐Ÿ‘‰ Wale waliofeli, wanaenda Jeshi, hawa wakigoma, basi hao wa juu
wote hawana raha.

05.๐Ÿ‘‰ Wale waliopata Zero na waliokataa
shule wanakuwa waganga wa kienyeji,
wote hapo juu watamtafuta huyu, pale
mambo yao yanapokwenda kombo. Tuache kudharauliana, kila mtu ni boss akiwa kwenye nafasi yake.
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‰๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿƒ๐Ÿฟ๐Ÿƒ๐Ÿฟ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About