Visa Vya Xmass
Hapo sasa patamu, cheki jamaa alivyowezwa na huyu dogo
Mfugaji mmoja alikwenda kwa mfugaji mwenzake (ambae pia ni bwana mifugo wa eneo lao) asubuhi moja. Alipobisha hodi mtoto wa kiume wa umri upatao miaka 12 akamfungulia mlango. Mazungumzo yafuatayo yakafuatia:
Mkulima: Baba yako yupo?
Mtoto: Hapana Mzee, amekwenda mjini.
Mkulima: Mama yako?
Mtoto: Nae kaenda mjini na baba.
Mkulima: Kaka yako Howard yupo?
Mtoto: Nae hayupo, wote yeye, baba na mama wamekwenda mjini. Kwani una shida gani? Kama kuna kitu unahitaji niambie maana nimeachiwa funguo na najua vifaa vinapowekwa.
Mzee akawaza kidogo halafu akasema: Kwa kweli nilitaka kuongea na baba, mama au kaka yako kwa kuwa kaka yako amempa mimba binti yangu.
Mtoto akafikiria kidogo halafu akasema: Kusema ukweli itabidi umsubirie baba, ila kwa kukusaidia ni kuwa baba hulipisha shilingi laki moja kwa kupandisha dume la ng’ombe na elfu hamsini kwa beberu. Ila sijui baba hutoza shilingi ngapi kwa Howard akifanikiwa kutia mimba.
Raha ya kuoa mke ambaye hajasoma
Ukioa mke asiyesoma hata hili unaweza kufanya
KUOA MKE AMBAE HAJASOMA RAHA SANA LEO NIMEMUAMBIA MWEZI HUU HATUTOLIPWA MSHAHARA KWAKUA HAUNA TR 30 KAENDA KUNGALIA KARENDA KARUDI ANANIAMBIA HAMNA SHIDA MME WANGU TUTAVUMILIA TU
🤣🤣🤣
🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂
Hakuna mtu mwenye mbio duniani kama huyu
HAKUNA MTU MWENYE MBIO, KAMA MSICHANA ALIYEPAKA MAKE UP ALAFU MVUA INYESHE….. 😂😂
Mabinti wengine kwa kupenda hela! cheki huyu anachokifanya
Phone call
gal: hellow
Boy: sweety mambo vipi?
Girl: poa
Boy: utakuwa free weekend? nilikuwa nataka uje nyumbani
Girl: oh sorry ctoweza kuja sababu kuna haruc ya aunt yangu
Boy: kama ni hivyo sawa nilikuwa nataka nikufanyie sapraiz nimekununulia BLACKBERRY.
Girl: oh ucjal ntakuja na hata ntalala huko huko
Boy: na haruc je?
Girl: nilikuwa nakutania
Boy: hata mi nilikuwa nakutania
Huyu mchaga kazidi sasa, angalia anavyomfanya huyu mbuzi
Mchaga alinunua mbuzi akamwambia mpishi Nyama nusu ipike pilau na ingine itie kwenye friza. Kichwa fanya supu, miguu fanya mchuzi chukuchuku. Ngozi usitupe tutafanya mswala, utumbo pikia ndizi na mifupa tutawauzia wenye mbwa. Kinyesi kihifadhi kwa mbolea ya bustani.
Mpishi akamuuliza Hutaki na sauti ya mbuzi tufanye ring tone kwenye simu yako? Mchaga akajibu Yesuu! hivi inawezekana? bac fanya hivyo tuwauzie na wengine hiyo ringtone. Chezeya mchaga!
Wanawake wanavyopenda hela, hadi kutoka kwa nyani na ngedere
Kama Nyani na ngedere wangekuwa na pesa…
Trust me Kuna wanawake wangekuwa wanaishi misituni mda huu…..
Wanavyopenda hela
😂😂😂😂😂😂😂😂
Angalia huyu jamaa alivyowafanyia watu uhuni bar
Jamaa kaingia Bar;
Jamaa: Muhudumu, nipe kinywaji na mpe kila mtu humu ndani kinywaji, maana wakati napata kinywaji lazima kila mtu apate kinywaji. Haraka sana muhudumu akagawa vinywaji,
Jamaa: Muhudumu nipe supu na kila mtu humu ndani mpe supu maana ninapokunywa supu kila mtu lazima anywe supu. Watu wakapewa supu tena safari hii wakapiga makofi.
Jamaa: Muhudumu nipe bili, na kila mtu humu ndani mpe bili maana wakati nalipa bili yangu kila mtu lazima alipe yake. Zogo lilianzia hapo…….
Unakumbuka haya enzi za shule?
Kama umesoma st Kayumba utakuwa una aidia na haya…
1.Unaenda shule umechelewa unakuta mwalim anakamata wachelewaj unaamua urudi nyumbani
2.unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni af unamuunguza mwenzio
3.mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu y kurudia nyumban
4.MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)
5.MTU akikunyima kitu chake unamwambia “Ahaa eeh utaona sa nne”
6.wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao
7.ukiibiwa daftar jipya unalia kuliko hata uliloandika
8.unajaza mapeni kwenye mkebe(compass) na mengine hayaandiki
9.vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba😂
10.hakuna habari nzur kama kuambiwa Leo hamna shule mwalim haupo
11.habari mbaya zaidi n kurud nyumban kutoka shule una njaa af unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa
12.mtoto wa mwalim utamgundua tu kwanzia sweta begi na viatu vyake
13.usiombee umpige mtoto wa mwalim utataman uache shule
14.unatengeneza kifutio cha ndala af unatishia eti kinafuta hadi peni😂
15.ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu af unaongeza kijiti katikati
16.siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na naji wanakagua kuni au mbolea😆
😂
Dah shule zetu hizi kiboko!!
Ipi umeipitia wewe
Share na wengine
Mzunguko wa elimu kiafrikaafrika
01.👉 Wale wanafunzi walioongoza Mashuleni, wanaenda kwenye Engineering na Medical school.
02.👉 Wale waliokuwa wa pili, wanachukua MBA na LLB na kuja kuwa Mameneja wa wanafunzi walioshika nafasi ya kwanza.
03.👉 Wale waliokuwa wa tatu, wanageukia Siasa na kuwaongoza wote hapo juu. Yaani wa kwanza na wa pili.
04.👉 Wale waliofeli, wanaenda Jeshi, hawa wakigoma, basi hao wa juu wote hawana raha.
05.👉 Wale waliopata Zero na waliokataa shule wanakuwa waganga wa kienyeji, wote hapo juu watamtafuta huyu, pale mambo yao yanapokwenda kombo. Tuache kudharauliana, kila mtu ni boss akiwa kwenye nafasi yake. 😂😂😂😂😉😆😆😆🏃🏃😜😜😜😜😜
MAJIBU YA MAKONDA WA DALADALA ZETU GONGOLAMBOTO HUKU
1. wewe Dada unaturingia nini na matiti yako mawili , mbwa pia ana matiti nane na haturingii eboo !!!!
2. Ka wafikiri Una haraka sana Shuka ukimbie.
3. Nauli kulipa lazima ,Chenji ukikumbuka.
4. Kutapika ndani ndani ya Daladala fain 250/= ,ukijamba pia 250/= ,Sasa jamba tukujue viti vina alarm!…
5.Hatujasema wewe ni Mnene ila Ukikalia SITI mbili Lipia….
6. Hio Elfu kumi yako nenda nunua avocado upake alafu uteleze hadi posta ,nauli ya daladala ni 350/=.
7. usifungue dirisha ungetaka upepo ungepanda pikipiki..
8. wewe Dada hebu sogea hukoo, Unaringa nini wakati asubuhi hii umeoga na sabuni ya kuoshea vyombo…
Kilichotokea Baada ya mlevi na mchungaji kukutana
MCHUNGAJI; “Unakunywa bia!?
MLEVI; “Ndio.
MCHUNGAJI; “Kwa siku unakunywa bia ngapi!?
MLEVI; “Nakunywa bia tano!
MCHUNGAJI; “Bia moja bei gani!?
MLEVU; “2500/
MCHUNGAJI; “Ulianza lini kunywa bia!?
MLEVI; “Miaka 18 iliyopita!
MCHUNGAJI; “Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000??
MLEVI; “Ndio!
MCHUNGAJI; “Kama u gekuwa unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover!?
MLEVI; “Samahani, naweza kukuuliza swali!?
MCHUNGAJI; “Uliza!
MLEVI; “Unakunywa bia!?
MCHUNGAJI; “Hapana!
MLEVI; “Nionyeshe Range Rover yako!
MCHUNGAJI; “akasepa”
Angalia nilichomjibu huyu kuhusu kabila langu
Kuna mtu kanikera et nmemkubalia urafiki Leo tu Facebook anataka kujua kabila langu
Bac akajifanya mjanjaa et akaniuliza mbu kwenu mnawaitaje
Mimi nkamjibu hatuwaiti wanakujaga wenyewe
😂😂😂😂😂😂😂
Si kwamba cjamuelewa ila sipendagi Ujinga Mimi
Kilichotokea baada ya mzungu na mbongo kukaa siti moja, bongo wasanii wengi
Mzungu akamdharau sana Mbongo nakujiona anajua kila kitu duniani!,
Akamwambia Mbongo waulizane maswali na Mbongo akishindwa anatoa sh.500 na endapo yeye atashindwa atatoa 100,000/=.
Mzungu akauliza ni nchi ipi ilishindwa kwenye vita kuu ya kwanza ya Dunia?
Mbongo akatoa 500 kuashiria hajui.
Na yeye akamuuliza Mzungu ni kitu gani kikienda juu kina miguu minne na kikirudi chini kina miguu mitatu?
Mzungu akafikiria akakosa jibu akatoa 100,000/= kuashiria hajui ila akataka kujua, akauliza ni nini hicho?
Mbongo akatoa 500 kuashiria hata yeye hajui!.
SHARE na marafiki kama umemkubali Mbongo kwa ujanja. Lakini unafikiri Mbongo huyu kwa akili hizi atakuwa ametokea mkoa gani!?.
Balaa la mitoto isiyopenda shule
SINA MBAVU NA HIKI KISA;
BALAA LA MITOTO ISIYOPENDA SHULE!
Baada ya mwiz kuvamia nyumba moja usiku na kuiba vitu vngi wakati anajiandaa kuondoka ghafla akadakwa mguu na dogo
DOGO: Usipoondoka na begi langu la shule NAPIGA KELELE….😂😂😂
Cheki huyu dingi alivyo mnoko
Unamtumia baba ako meseji ukiwa shule “Baba naomba unitumie 100,000 ya pckt mny” anakuuliza “pckt mny” ndo nini? Unamjibu ni kifupi cha “pocket money” af ankutumia 10,000, unamuuliza hiyo hela ni ya nini? Anakwambia ni kifupi cha 100,000.
Hapo ndo unatamani kuchoma shule ufe.
Jinsi Mapenzi yanavyoweza kukupa stress
Mapenzi ni balaa
Mapenzi ujue yanawez kukupa stress adi mama ako akikuuliz what’s wrong🤔-—unawez kumjib MAMA WE BADO MDOGO UWEZ ELEW🤣🤣🤣
Angalia huyu boyfriend alivyomuweza huyu msichana wake
Siku moja msichana alikuwa anapita maeneo ya A.T.M gafla
akamuona boyfriend wake anatoa pesa kwenye A.T.M binti
akaamua kujificha na kumtumia boyfriend wake sms ya
kimahaba
“Honey kama upo nyumbani umelala naomba unitumie ndoto
zako,
Kama unakula nitumie chakula, Kama unacheka nitumie kicheko
chako,
Kama unalia nitumie machozi yako,Kama unatoa pesa kwenye
A.T.M nitumie pesa.” Boyfriend akajibu “NIKO CHOONI LABDA
NIKUTUMIE KINYESI MPENZI!!
Stori za simu za wavulana na wasichana
STORY ZA WASICHANA KTK SIM
Mary… Hallow mpenzii
Lily…. Niambie my dear
Mary..Pouwaa za siku jamani
Lily…Nzuri rafiki Yangu wa damu
Mary…Jioni nakuja kwako tule Na
kunywa japo wine wanguu
Lily…Nakusubiri kwa hamuu
mpenziiii
BAADA YA KUKATA SIMU…KILA
MMOJA ANAWAZA
Lily…Huyu mchawi wa kike Leo
anataka kuja kwangu wala hanikuti.
Mary..Hahahahaaaa Uwiiiiiiiiii huyu
kahaba eti nakusubir Kwa hamuu
nani aende!!!
STORY ZA WAVULANA KATIKA SIMU
John…Niaje we mbwaa
Sam…Pouwa kichaa wanguu
John..Upo wap mpumbavu wewe
Sam…Niko hom, we fala Uko wap?
John..Baadae nakuibukia jambaz
langu tukale bata
Sawa… Pouwaa we ms**nge
nakusubiri
BAADA YA KUKATA SIMU…KILA
MMOJA ANAWAZA
John…Dah baadae nikakae na
mwanangu Sam sijamuona long
time
Sam…John bwana akiwa Na pesa
lazima anitafute mwanaeee.
FUNZO..
Baadhi ya Wasichana
hujifanya wanapendana Kwa
maneno lkn ni Kwa nje tu!! lkn
WANACHUKIANA
WAVULANA unaweza Kudhani
hawapendani Kwa Maneno lkn
WANAPENDANA..
Mpe TANO mchizi wako kudumisha upendo wetu wavulana…
High 👊👊👊👊👊 boys
hiyo apo
Angalia huyu jamaa alivyoachika na msichana wake kwa kujidai kuongea kingereza na mwishowe kuchanganya maneno
MSICHANA: Mbona jana nimekupigia simu hujapokea?
JAMAA: please beby forget me.
MSichAnA: eeeh unaniambia hivo mimi?
JAMAA: nakuomba sana forget me.
MSICHANA: aya bwana poa maisha mema.
Msichana anakata simu jamaa ndo ananiuliza.”sasa
sijui amekasirikia lipi?” Mi nikamwambia we zuzu
umemwambia AKUSAHAU, dah, kumbe
ningemwambiaje? hahaha, ungemwambia
ForgivE me! au Ungesema Tu NaombA nSameHe.
Recent Comments