Visa Vya Wasichana Na Wavulana
Haya mapenzi jamani! Umewah kumpenda kwa kihivi??
Sijui Kama ushawai fall in love ile haswaa..
yani unampenda mtoto hadi akikupigia ile sauti ilivo tamu unajiskia kutafuna na kuimeza hiyo simu
Akikuita tu “my love”unajiskia tu kuvua nguo mwenywe
..
hicho kiupendo ukiwa nae unajskia unaweza piga wanaume 8 kwa pamoja
Yani ile love mtashinda pamoja kutwa nzima afu usiku unakopa salio umpigie muongee
Yani yale mapenz kiasi ukiona love story za romeo na Juliet unaona hakuna wanachofanya coz mapenz yao hayafikii yenu..
ile true love akikuangalia machoni akuguse mashavu afu akwambie,”I love u”
Unajishikilia kwenye ukuta usizimie..
yani ukimfikiria unaweza kulala chini ya kitanda Ku dilute hiyo feeling coz ni too much..
Umewahi kufeel hivyo??
Kama ushawai experience hivyo?? Basi HIYO SIYO “LOVE” NI “BANGI” PLZ ACHA KUTUMIA!
#ishakua_biashara_kichaa
Hizi swaga za huyu jamaa ni shida, Google!
Jamaa alikuwa kwenye daladala pembeni kuna
dada mrembo kakaa. Kamlia timing kwa muda
kisha halafu akamuuliza “Samahani dada
unaitwa Google?”.
Dada: “hapana, kwanini umedhani naitwa
hivyo?”. Jamaa: “Una kila kitu nnachokitafuta
“😅😃😃😃😃😃😃😃😃😃
Kilichotokea Baada ya mlevi na mchungaji kukutana
MCHUNGAJI; “Unakunywa bia!?
MLEVI; “Ndio.
MCHUNGAJI; “Kwa siku unakunywa bia ngapi!?
MLEVI; “Nakunywa bia tano!
MCHUNGAJI; “Bia moja bei gani!?
MLEVU; “2500/
MCHUNGAJI; “Ulianza lini kunywa bia!?
MLEVI; “Miaka 18 iliyopita!
MCHUNGAJI; “Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000??
MLEVI; “Ndio!
MCHUNGAJI; “Kama u gekuwa unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover!?
MLEVI; “Samahani, naweza kukuuliza swali!?
MCHUNGAJI; “Uliza!
MLEVI; “Unakunywa bia!?
MCHUNGAJI; “Hapana!
MLEVI; “Nionyeshe Range Rover yako!
MCHUNGAJI; “akasepa”
Kichekesho cha mtalii na mbongo
Duh! Sikubali bora mbavu zituume wote!
Watalii wana dharau sana bana, Mtalii alikodi boti akazunguka nayo kwenye mto Rufiji kuangalia mandhari, akamuuliza kijana anayeongoza boti, “Do you know Biology, Psychology and Anthropology?” Kijana akajibu “NO,” Mtalii akamwambia “nothing you know under the sun? You are useless, and u’ll die with your illiteracy!” baada ya muda boti ikaanza kuzama, kijana akamwambia mtalii “Do you know kuogelealogy and kusepalogy from mambalogy? Mtalii akajibu huku ametoa macho “No” kijana akamwambia “You will kufalogy and mambalogy wil eat your matakology because of your bad-mdomology..😂😂😂😂😂😂
Huu ndio uhondo na raha ya kupanda daladala wajameni
Wasiopanda dalaladala wanakosa uhondo wa kauli hizi
1. nitakupa
2. Atapewa mbele
3. Hujapewa mbele?
4. Utapewa nyuma
5. Nitakupa nikikaa vizuri
6. Ngoja isimame nikupe
7. subiri asimamishe nikupe
8. hivi nlivyo kaa ntakupaje?
9. Utapewa tulia
10. Nikupe mara ngapi?
Mambo ya pesa haya..
MAMBO YA FEDHA AISEE……. Kuna jamaa alipewa shilingi 983628763600/= …acha uvivu, najua hujasoma ni kiasi gani hicho cha fedha na mbaya zaidi hujagundua kwamba katikati ya namba hizo kuna herufi A… safi sana, najua umeangalia tena kuiona hiyo herufi, bahati mbaya hujaiona. 😜😜😜😜😜😜😜
Acha usumbufu…
UNAMNG’ANG’ANIZA MPENZI WAKO AKUWEKE KWNY PROFILE PICHA MLOPIGA PAMOJA
HIVI ULIDHANI MWL.NYERERE ALISHINDWA KUKAA NA MKEWE MARIA KWNY NOTI YA BUKU
😂😂😂😂😂😂😂
Acha Usumbufu…..
Chezea kufulia!
Huu Mwezi jinsi nilivyofulia yaani hata nikikuta mende wamesimama wawili najua wananisema
😂😂😂
Tofauti kati ya Binti wa Kizungu na Binti wa Kibongo mwanamme anapotoka kuoga
Tofauti ya Binti wa Kizungu na Binti wa Kibongo pale ambapo Mwanaume wake atokapo kuoga.
Binti wa Kizungu: Baby you look nice and fresh.
Binti wa Kibongo: Naona safari imeiva, Mwanaume hupumziki kama nesi wa zamu
😆😆😆😆
Angalia huyu Jamaa alivyomuweza huyu mrembo
Nipo kwenye daladala siti ya nyuma kabisa nimekaa na mrembo mzurii.sasa nikawa namtongoza kwa sauti ya chini sana watu wengine wasiskie,akawa hanijibu kitu,mala gafra akapayuka kwanguvu na kwa sauti ya juu iliyomshtua kila mtu.
”Nimesema stakii,stakii tena unikome”😳😳
Nami nikamjibu kwa sauti ya juu vile vile
”Kama umejamba nisikwambie bhanaa,kwani ww nani?”☹
😂😂😂😂😂😂😂😂😂
MIMI SIO MTU WA MCHEZO MCHEZO
Sipendag ujuinga mim
Cheki kilichonipata sasa, ungekua wewe ungefanyaje?
Siku moja katika pitapita zangu nikakutana na mtoto mmoja mkali balaa yaani ni mzuri sanaaaa, moyo ukanituma nimuimbishe mtoto akakubali kwamba nitafute siku tukae tuongee vizuri akasema nimpe namba yangu ya simu.
Ebwana si akatoa simu hiyo inauzwa laki sita mimi hapa nina kisimu cha tochi tena nimefunga na rababendi
Je, wewe ungeendelea kumtajia namba zako!!!
Utani wa wahindi, cheka kidogo
Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili
(1) Mfa maji ?……………….. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?………… Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?……….. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?……………… Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?……. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?……… Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?…….. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?…… Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?……… Takosa guo ya sikukuu…
(10) Kila ndege ?………….. …Hutua Airport
(11) Bandu bandu ?….. …….Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?… Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?….Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?………. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?…….. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?…. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? …….. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? …………..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?…….. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?….Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?…….. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? ……….Taenda Chadema
(23) Bendera ?……………. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?……. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?………. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? …….. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.
Mwizi kawezwa ki kwelii
Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae maana hta hela ya kula Jana sikua nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu? sipendagi ujinga🚶🏻 na kitu hela mm!
Je, hili nalo ulilipitia ulipokua Shuleni?
Hakuna Kitu Kilikua Kinaniumizaga Kipindi Nipo Shuleni.
Time Mmetoka Kwenye Mitihani Wa Mathematics Halafu Mpo Kikundi Fulani Either Mnarudi Nyumbani Au Mnapumzika Kwa Ajili Ya Next Exam.
Unasikia Jamaa Wanabishana Pale Jibu Lilikua 4 Mwingine Anasema 5, Na Wewe Ulijaza 80.
Maajabu ya wananchi wa Tanzania, Je, wajua hili?
JE WAJUA TANZANIA NI NCHI PEKEE AMBAYO WATU WANAPOANZA KUCHAT huanza kwa kiingereza ‘morning’ na hupiga stor zote kwa kiswahil mwishon humalizia tena kwa kiingereza ‘ g9t
Mambo ya mke na mume haya, chezea mchepuko!?
Mume akamwambia mke wake:
“Funga macho yako tufanye maombi”
Akaanza kwa Kimombo:-
“… Lord I pray for Grace, I pray for Mercy, I pray 4 Joy, I pray 4 Love, I pray 4 Hope, I pray 4 GLORY, I pray 4 Faith, I pray 4….”
Mke akadakia, “Unadhani mimi sina ee” akaanza:-
I pray 4 Felix, I pray 4 Temu, I pray 4 Rweyemamu, I pray 4 Masawe, I pray 4 Benson, I pray 4 Onyango, I pray 4 Swai, I pray kwa wote niliowasahau!!
Chezea mchepuko…!!
Huyu Jamaa kawaweza polisi kweli
Et jamaa kawekwa jela kwa kosa la kupoteza mamiilion.ya kampun akiwa gerezan babayake alituma barua
Ikisema yan.mwanangu tumapata shida maana shamba halijalimwa na jatujii litalimwaje na msimu ndio huo nataman.ungekuwepo ningepata msaada wa kulimiwa hili shamba
Yule kijana alijibu tafadhal baba usilime hilo shamba maana pesa zote nilizo ibwa nimeficha.huko
Kwakuwa barua zote laxima zipite kwa mkuu wa gereza ndio xiende kwa muhusika kesho yake mzee alikuwa shamba lote limelimwaa na polisi
Akatuma ujumbe tena yule kijana
Nashukulu umepata msaada sasa nazan unaweza ukaendelea kupanda mazao shamban.kwetu😂😂😂😂😂
Mimi ndio nimeelewa hivi!
Leo nimepishana na Vitz imeandikwa, “Never trust women”
Nikajua huyu mtu lazima alikuaga na Range Rover
😂😂😂😂😂😂
Baada ya kumkuta mwanamme mwingine chumbani kwake na mke wake cheki huyu anachokifanya
NAKUA(BABA) karudi kazini mwanae mdogo akamuwahi,
DOGO: Baba usiingie ndani kina jini chumbani kwenu
NAKUA: Hakuna kitu kama hicho
DOGO: Kweli baba kuna jini liko kwenye kabati lenu la nguo….
NAKUA kaingia ndani kamkuta mkewe kalala kitandani kajifunika shuka gubigubi hadi kichwani. Kaenda kwenye kabati kufungua mlango , akamkuta rafiki yake wa miaka mingi yuko uchi ndani ya kabati
NAKUA: Aise unajua we fala sana, we rafiki yangu miaka yote hiyo halafu unamtisha mwanangu eti wewe jini, hebu toka huko nenda kwenu kacheze michezo hiyo na mwanao.
Recent Comments