Visa Vya Kukubadilisha Mudi
Angalia huyu mvulana anachomwambia huyu daktari baada ya rafiki yake wa kike kupata ujauzito
😂😂😂😂
MVULANA: Daktari, rafiki yangu wa kike ni mjamzito, lakini mara zote nimekua nikitumia kinga. Inawezekanaje hii?
DAKTARI: Ngoja nikusimulie hadithi. Kulikua na Muindaji ambaye alikua anabeba bunduki kila aendako. Siku moja, alichukua mwamvuli badala ya bunduki na akaenda nayo. Ghafla akatokea Simba mbele yake. Ili amtishie Simba, muindaji akatumia mwamvuli na kummiminia risasi Simba. Simba akafa palepale!
MVULANA: Sio kweli!! Lazima kulikua na mtu mwengine pembeni aliyempiga risasi Simba.
DAKTARI: Nashukuru umeelewa somo!!😂
😂😂😂😂😂😂😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃
Chezea kufulia!
Huu Mwezi jinsi nilivyofulia yaani hata nikikuta mende wamesimama wawili najua wananisema
😂😂😂
Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi
*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!
Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.
1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu…”
Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”
🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂😂😂😂_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_
Tofauti ya mke na mchepuko!!!
MKE NA MCHEPUKO.
Mke ni kama Tv na Mchepuko ni kama Simu.
Nyumbani unaangalia Tv lakini ukitoka unatoka na simu.
Mara chache unafurahia Tv lakini Muda mrefu unacheza na simu yako.
Tv ni bure kwa maisha yako yote, lakini Simu kama hujalipia hupati huduma.
Tv ni kubwa nzito na wakati wote ni ya zamani. Lakini simu ni nzuri, nyembamba, na ni rahisi kubeba.
Gharama za huduma za tv ni ndogo sana, Lakini gharama za huduma za Simu ni kubwa na pia ni lazima kuzitimiza.
Tv ina remote lakini Simu haina.
Kitu muhimu zaidi simu ina njia mbili za kuwasiliana unaongea na unasikiliza lakini Tv unalazimika kusikiliza hata kama hutaki au unataka.
Unaweza kununua Tv mara moja na ukatumia kwa kipindi kirefu lakini Simu mara zote unabadilisha inategemea na fasheni.
Ya mwisho na ya kuzingatia
Tv haina Virusi lakini Simu inayo.
KUWA MAKINI.
Kali ya mwaka iliyotokea Benki Baada ya wezi kuiba
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuni…unaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuni…😂😂😂😂
Lugha za namba ni noma
Leo kuna mdogo wangu nimemtumia meseji nimemuomba aniazime chaja yake ya simu. Akanijibu 21002 Nikawa mkali nikamuambia kuchajia mara moja tu ndio HELA yote hio si bora nikanunue Chaja yangu mpya. Akaniambia nimesema TUMIA TU 😂😂mtatuua na lugha zenu😜
Angalia nilivyookoa maisha ya mtu leo
Nmeokoa maisha ya mtu asubuhi ya leo huwezi amini.Nmekutana na ombaomba nikamuuliza atajisikiaje nikimpa sh.30,000/-
Akasema ATAKUFA kwa furaha.Nikaondoka bila kumpa ili ASIFE.😃😃😃😃
Kilichompata huyu jammaa baada ya simu yake kuita msikitini
Jamaa alisahau kuzima simu akiwa msikitini anaswali GHAFLA simu ikaita akaingiza mkono ili aikate, kwa bahat mbaya akaminya cha kupokelea, alipohangaika kuzima akajikuta kaminya laudspika ikasikika sauti ‘ETI HONEY UMESEMA NIWEKE KITIMOTO KIASI GANI? 😄😄😄🙆🙆🙆🙆
Hii ya mamba na kiboko kali, Wewe unaonaje?
Eti kati ya MAMBA na KIBOKO nani kiboko???😜😜😜😜
Mi naona MAMBA ndo kiboko!😳
Ujinga mbele kwa mbele😜😜😜😜😜🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻🏃🏻
Misemo ya kina dada
Misemo ya kina dada
walianza na halohalooo!
Wakaja unalo babu weee!
Ikafuata utajijuuu!
Ikafupishwa utajiJJ!
Mara ghafla kantangazeee!
Haikukaa sana kansajiriii!
Ikatoka nyingine nishiiiiida!
Unaijua iliyotoka Leo?
Heh! Heh! Heeeh! MB zenyewe 8 nikudownload unanini?
Huyu Jamaa ubahili umezidi kwa hiki anachomwambia huyu dada
Kama ni ubahili hapa umezidi
mdada Bby naomba hela nimpeleke mdogo wangu hospital kang’atwa na nyoka
JAmaa embu mpe huyo nyoka cm niongee nae.. maisha yanakaba..😂😂
Raha ya kuoa mke ambaye hajasoma
Ukioa mke asiyesoma hata hili unaweza kufanya
KUOA MKE AMBAE HAJASOMA RAHA SANA LEO NIMEMUAMBIA MWEZI HUU HATUTOLIPWA MSHAHARA KWAKUA HAUNA TR 30 KAENDA KUNGALIA KARENDA KARUDI ANANIAMBIA HAMNA SHIDA MME WANGU TUTAVUMILIA TU
🤣🤣🤣
🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂
Duh. Chezeya kuhama!
Pale imebaki siku moja uhame kwenye nyumba ya kupanga af unakuta umebakiza unit 60 za umeme, inabidi tu uchemshe maji hadi yale ya kuflashia choo
😡😡😡😡😡
Soma alichokisema mlevi baada ya kukuta watu wakimpiga mwizi
Mlevi mmoja aliona wananchi wakipiga mwizi akawaambia “mwacheni msimpige, hii tabia yenu ya kupiga wezi mtakuja shtukia mnampiga Yesu, maana imeandikwa atakuja kama mwizi!”
Tenda Wema Uende Zako
Nimekuta panya ana struggle kuingia chini ya mlango wa jirani yangu…
Nikagonga mlango Jirani kafungua panya akapenya mi nkaenda zangu…..
Tenda Wema Uende Zako!!! Sipendi Ujinga mimi kwanini panya wa watu apate shida
Huyu kashauzwa!! Angalia kilichomkuta sasa
Jamaa alionekana Mnyooooonge sana ikabidi mpita njia amuulize…
Kaka, mbona u mnyonge hivyo?”
Jamaa : ‘aaaaah we niache tu, kuna rafiki yangu nimemkopesha laki tano akafanye PLASTIC SURGERY ya uso, Mwanaharamu sasa nashindwa kumtambua!!!
😂😂😂😂😂😂
Duh! Hiki nacho chombo cha moto?
_Sheria inasema kila anaetembea na chombo cha moto barabarani sharti awe na leseni._
_Sasa hawa wauza kahawa mbona wanatembea na chombo cha moto lakini hawakamatwi 😡._
_Hizi sheria zinapendelea._
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Alichofanya mke baada ya mme wake kupenda kumchunga sana
Alifanya hivi;
Siku ya kwanza
MUME: Halooo vipi mke wangu salama weye?.
MKE: Salama tu
MUME: Uko wapi?
MKE: Jamani si niko nyumbani
MUME: Mhh kama kweli uko nyumbani washa blender nisikie…..mke akawasha blender
MKE: Umesikia?
MUME: Okay haya mi natoka kazini naja
Siku ya pili
MUME: Vipi mko salama huko?
MKE: Tupo kama ulivyotuacha
MUME: kwani uko wapi?
MKE: Niko nyumbani napika
MUME: Washa brender kama kweli uko nyumbani
Mke akawasha blender
MKE: Umesikia?
MUME: Poa ntarudi baada ya masaa mawili
Siku sita baadae mume akaamua kurudi bila kumtaarifu mkewe alipofika home kamkuta mdada wa kazi yuko peke yake.
MUME: We mama yako yuko wapi?
MDADA: Sijui ameondoka na blender toka asubuhi
Huyu mke ni shida!
MUME: “Unajua mi unanishangaza sana, kila siku nakusikia mara useme TV yangu, gari yangu, chumbani kwangu, mara hoo watoto wangu. Sisi ni mke na mume, kila kitu ni chetu. Jirekebishe bwana”.👴😎😎😒
MKE: Yuko kimya anaendelea na shughuli zake za kupekua kabatini kama hasikii, na hakumjibu kitu mumewe.👵😷
MUME: Akamuuliza kwa hamaki,”Sasa hapo unatafuta nini?”.👴😡
MKE: “Sidiria yetu!!”👙💏
MUME: (kamfungia kabatini alafu kamwambia. “nipo chumbani , “)👴😷😷
💃💃💃💃💃💃
😂😂😂😂😂😂
Recent Comments