Vihoja Vya Wakaka Na Wadada
Je hili ni kweli kuhusu mpenzi maskini na Tajiri?
Siku hizi kudekezwa na kupetiwa petiwa tunawaachia matajiri
Hakuna mwanamke yupo tayar kulalia kifua cha maskini ambacho moyo unadunda
Deni,, Deni,Deni, Deni .
๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐ถ๐ฝโโ
Mume alichomjibu mchepuko wa mke wake
๐ย Jamaa kamuaga mkewe anaenda semina Songea kwa wiki nzima kumbe kahamia kwa demu nyumba ya pili toka kwake. Siku ya 1 kalala asubuhi alipoamka kachungulia kwake kukoje,
Si kamuona jamaa yuko nje ya nyumba yake kavaa taulo lake anapiga mswaki. Akapiga kelele, ‘We nani?’, Jamaa akajibu, ‘Mshikaji mambo ya mjini, mume wa huyu demu kasafiri kaenda Songea mi ndo najivinjari hapa’. Mume kajibu kwa uchungu, Shenzi mkubwa, ngoja nirudi toka Songea nakuua.๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
*Mniache mimi sipendi Ujinga Ujinga ๐๏ฟฝ๐๏ฟฝ๐๏ฟฝ๐
Kwa Wadada wanaotaka kuolewa
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuniโฆunaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuniโฆ๐๐๐๐
Maajabu ya wananchi wa Tanzania, Je, wajua hili?
JE WAJUA TANZANIA NI NCHI PEKEE AMBAYO WATU WANAPOANZA KUCHAT huanza kwa kiingereza ‘morning’ na hupiga stor zote kwa kiswahil mwishon humalizia tena kwa kiingereza ‘ g9t
Cheki kilichompata huyu dada!!
NDOA inafungwa KANISANI Mchungaji akauliza-Yeyote mwenye Pingamizi La Ndoa hii kufungwa aje Mbele, +++ KIBABU kikasimama na kwenda Mbele,
Bi harusi akaanguka na akazimia ghafla!๐ญ๐ญ๐ญ
Mchungaji- Tuambie Babu Pingamizi Lako!
Babu-Nimeamua kuja mbele,kule nyuma sisikii vizuri! watu hoiiii!!
hata mimi hoiโฆ๐๐๐๐๐๐๐
Sababu ya girlfriend ๐ง kuniblock
Nimeblockiwa bila kosa X Girlfriend From no where kanitext eti Hi; Vp na huko kwenu mvua inanyesha โฆNimemjibu kwani nimekutumia text ina matope?
sipendangi ujinga mimi
Wazo la jioni hii
๐ขWAZO LA JIONI HII ๐ข
KAMA MWAKA JANA ULIPIGA HATUA NA HUJAFIKIA MALENGO MWAKA HUU PIGA MSAMBA๐
Angalia jamaa alivyouweza huu mchepuko wake
Kuna mchepuko nilimtumia nauli jana ili aje,.kwang sasa leo kaniambia eti ” nimesahau ile line yenye M-pesa home plz nitumie tena kwa tigo mpenz””!! Me nikajifanya chizi nikatuma Kule kule kwenye voda (aliosema kaacha home) Nikatuma huko message ivi “nikuongezee Sh. Ngapi tena mpenz..!!” Akanjbu “elfu 20,000 tu mpenzi” Mtuhurumie jamani ๐๐๐
Kilichompata huyu jammaa baada ya simu yake kuita msikitini
Jamaa alisahau kuzima simu akiwa msikitini anaswali GHAFLA simu ikaita akaingiza mkono ili aikate, kwa bahat mbaya akaminya cha kupokelea, alipohangaika kuzima akajikuta kaminya laudspika ikasikika sauti ‘ETI HONEY UMESEMA NIWEKE KITIMOTO KIASI GANI? ๐๐๐๐๐๐๐
Huyu mchungaji ni noma, cheki alichomwambia pedeshe
Mchungaji kamfuata pedeshe moja maarufu kwa
kumwaga pesa kwenye kumbi za muziki;
MCHUNGAJI: Kijana, tuko katika harakati za
kujenga kanisa, jitafutie nafasi katika ufalme wa
mbingu kwa kuchangia ujenzi huu. Na Mungu
atakubariki zaidi
PEDESHE: Samahani Mchungaji haitakuwa vizuri
mimi kuchangia kanisa, fedha zangu ni haramu,
huwa nazipata kwa utapeli na kuuza madawa ya
kulevya.
MCHUNGAJI: Yote ni heri, pesa yako tutatumia
kwa kujenga eneo la choo we toa tu!!!
Angalia huyu house girl wa mzungu alichokifanya na anachokisema
House girl mmoja alipewa kazi na mzungu mara akavunja sahani.
Mzungu aliporejea,kazin akamuuliza ‘what happened to my plate?
House girl akajbu: ‘The dog wow wow friji paaa, mchuzi mwaaaa the vyombo pangalapangala the sahan ngelengenjeeโฆโฆthe pasuka paaaaaaaa
๐๐๐๐hadi saiz mzungu bado anasoma dictionary hajui lugha gani imetumika
Angalia walichofanyiana hawa wanadoa, Kati ya huyu mme na mke nani zaidi?
MUME wakati anakata roho huku mkewe akiwa amemshikilia alisema mke wangu, mi natubu kwako, kwani nilifanya mapenzi na dada yako, mdogo wako, rafiki yako na mama yako
MKE akamnong’oneza mume wake na kumwambia mbona mimi nayafahamu yote, ndio maana nimekupa sumu ili na wewe ujue uchungu wake. JE NANI ZAIDI?
Huyu jamaa kawaweza polisi watatu, cheki alichowaambia
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: kimya
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: we nani kwani?
Polisi::: sisi polisi
Jamaa::: mnataka nini?
Polisi::: kuongea na wewe
Jamaa::: kuongea na mimi?!
Polisi::: ndio
Jamaa::: mko wangapi?
Polisi::: tuko watatu
Jamaa::: kama mko watatu si muongee wenyeweโฆ!!!
Soma hii, kama wewe ndio mzazi wa huyu msichana ungefanyaje?
Wewe ni mzazi mwanao anasoma kidato cha tatu mkoani umemsafirisha leo kwenda shule baada ya masaa matano ukasikia gari alilo panda mwanao limepata ajali wamekufa watu wote upo ktk harakati za kuandaa msiba,
mwanao anakupigia simu baba/mama mimi mzima sijafa mpenzi wangu ABDUL aliniambia nishuke Chalinze ili niwe nae kwa siku mbili alafu niende shule je, wewe mzazi unge mfanyaje mwanao?
Kweli shilingi yaua, Huyu jamaa kapatikana, angalia anachomjibu mke wake,
Jamaa alikuwa anagombana na mkewe,hatimae
akamwambia kwa ukali
“Unajua nimechoka sasa, haya kusanya nguo
zako naโฆโฆ..
Kabla hajamalizia sentensi simu
ya mkewe ikaita, kumbe alikuwa ni baba yake.
Basi mzee akaanza kuongea na binti yake huku
jamaa anasikia
“Aisee mwanangu nimebahatika kuuza ile
nyumba yangu sasa nimeona niwatumie milioni
20 mjaribu kuanzisha mradi na mwenzio.
Haya mwambie yeye nitampigia kesho kama
ana mradi mwingine nimpe hela kidogo”.Baada
ya simu kukatwa mke akamgeukia jamaa
akamuuliza,”eeenhee!!! ulikuwa unasema
umenichoka nikusanye nguo zangu halafu
iweje? Jamaa kwa upole akajibu “Nilikuwa
nasema ukusanye nguo zako na unipe nifue”.
Angalia nilichomjibu huyu kuhusu kabila langu
Kuna mtu kanikeraย et nmemkubalia urafiki Leo tuย Facebook anataka kujua kabila langu
Bac akajifanya mjanjaa etย akaniuliza mbu kwenu mnawaitaje
Mimi nkamjibu hatuwaiti wanakujagaย wenyewe
๐๐๐๐๐๐๐
Si kwamba cjamuelewa ila sipendagi Ujinga Mimi
Mlevi kazua tafrani, angalia alichokifanya hapa
MLEVI mmoja aliingia baa akavuta kiti na kukaa mhudumu akatokea kumsikiliza.
MHUDUMU: Nikusaidie nini?
MLEVI: Eeh! nipe bia ya baridi kisaha wasikilize wote waliokaa hapa, wape bia na wao maana sipendi kunywa pombe wengine wananiangalia
Akaja mhudumu wa jikoni “nikusaidie nini?”
MLEVI: Niletee supu kisha wasikilize wote waliokaa hapa na wao wape supu sipendi kunywa supu watu wananiangalia
Safari hii watu wakapiga makofi
Baadae akamuita mhudumu
MLEVI: Niandikie bili zangu kisha waandikie wote bili zao sipendi kulipa huku watu wananiangalia
Wale wateja wakamvaa na kumshushia kichapoโฆ teh teh teh teh teh hii kali hakuna cha bure mjini hahahaha na jasho la mtu haliliwi wandugu
Hyuyu daktari ni noma, cheki anachokisema
Kuna Daktari wa Moyo alifariki wakamchongeaa jeneza lenye umbo la Moyo. Ghafla Daktari mwingine akaanza kucheka, watu wakamuuliza “kwanini unacheka unafurahia mwenzako kufariki?” Daktari yule akajibu “hapana mimi ni Daktari wa kutahiri nafikilia nikifa mtanichongea jeneza lenye umbo la โฆ.”
Kizungu nacho ni sheeeedeer
Mtalii: Do you have vegetables here.
Mtafsiri: Mnavyo vijimeza hapa.
Waiter: Vijimeza vidogo hatuna.
Mtafsiri: No sir, they don’t have.
Mtalii: OK, fine, do you have hot dogs.
Mtafsiri: Sawa, je mnao mbwa wa moto.
Waiter: Loh! Bwana we, hatupiki mbwa hapa.
Mtafsiri: They don’t cook here
Mtalii: What type of snacks do you have here.
Mtafsiri: Aina ngapi ya nyoka mnao hapa,
Waiter: We bwana we hapa hatupiki aina yeyote
ya nyoka, mwache akale nyumbani kwao.
Mtafsiri: They don’t cook any type of snacks
here,
maybe you can go back and eat at home.
Mtalii: OK, at least give us a cocktail juice.
Mtafsiri: OK, tupatie hata juisi ya mkia wa jogoo.
Waiter: Hebu tokeni na bangi zenu hapa, tena
sasa hivi kabla sijakasirika.
Mtafsiri: Lets get out of here
๐๐๐๐๐๐
Usicheke pekeyako









I’m so happy you’re here! ๐ฅณ




































































Recent Comments