Vihoja Vya Jumapili

Kilichompata huyu anayependa kusoma SMS za watu kwenye daladala

Jana nilipanda daladala nikapata seat nikaketi, nikawa nimejiachia ninachati kwenye simu yangu(Smart phone), kukawa na jamaa kasimama pembeni yangu, ye hakupata seat. Sasa akawa anasoma message zangu bila aibu yani anafutilia ninavyochati…

Basi nikasema ngoja nimtie Adabu mshenzi huyu…. Nikacheck saa yangu yamkononi kisha nikatext: “Oya Ben Kwaheri bwana, zimebaki sekunde 30 tu hili bomu💣 lilipuke… najua hatutaonana tena, nitunzie Familia yangu, wambie nawapenda sana…” Yule jamaa akajirusha dirishani……😂😅

​kwani mi napenda ujinga xx 😂😂😂😂😂😂😂

Angalia alichokifanya huyu mtu baada ya kuokota wallet ya thamani

Jamaa aliokota wallet, alipofika nyumbani akapiga simu kwenye radio station “naitwa Juma nimepiga simu kutangaza kuwa nimeokota wallet ndani ina laki7, ATM card na karatasi yenye PIN ya ATM card na kijimfuko cha dhahabu” Mtangazaji akasema, kwa hiyo ungependa kumrudishia mwenyewe kama anakusikiliza? Jamaa akajibu; hapana, ninaomba kumuombea dedication wimbo wa R.Kelly usemao “U SAVED ME” umfikie popote alipo!!

Je, hii ni kweli kwa wale wasichana wasiojibu meseji WhatsApp!!!?

Ukiona hivyo ujue ndio hivi

Mwanaume mwenzangu ukiona unamtext msg msichana WhatsApp kaisoma hajajibu, umetuma ya pili kasoma hajajibu, ukatuma ya tatu hajajibu mmmmmh😨😨 hapo ujue mwenzio kaangalia kwenye profile yako, kakagua picha weee mwishoni akajisemea tu “Huyu.mkaka hapana kwa kweli”🤣🤣🤣🤣🤣🤣

🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂

Huyu mchungaji ni noma, cheki alichomwambia pedeshe

Mchungaji kamfuata pedeshe moja maarufu kwa
kumwaga pesa kwenye kumbi za muziki;
MCHUNGAJI: Kijana, tuko katika harakati za
kujenga kanisa, jitafutie nafasi katika ufalme wa
mbingu kwa kuchangia ujenzi huu. Na Mungu
atakubariki zaidi

PEDESHE: Samahani Mchungaji haitakuwa vizuri
mimi kuchangia kanisa, fedha zangu ni haramu,
huwa nazipata kwa utapeli na kuuza madawa ya
kulevya.
MCHUNGAJI: Yote ni heri, pesa yako tutatumia
kwa kujenga eneo la choo we toa tu!!!

Simu ilivyozua utata

Mama alichukuwa simu akampa mwanawe. Mama..Mpigie babako mwambie chakula tayari. (Mtoto akachukuwa na kupiga) Mtoto…Mama simu ya baba imepokelewa na mwanamke. (Mama kwa hasira) Akirud atanitambua leo. (Baada ya muda kidogo baba akarud,kufika mlangon tu kapokewa na sufuria ya kichwa. Hajakaa vzur mwiko wa pua) Mama..Mwanangu ulipopiga simu ya babako mwanamke wake alisemaje?? Mtoto..Alisema mteja unaempigia hapatikan kwa sasa…..

Maujanja ya kumkalisha mwanamme wako nyumbani weekend haya hapa

Siku hizi wa naume licha ya kukimbia nyumba zao kwa kisingizio cha kazi maajabu weekend hasa Jumamosi utasikia wanaaga nafika hapo njiani naja naenda kununua gazeti.

Kumbe wanaenda kunywa supu unasubiri wee mpaka alasiri au jioni

Hivyo wanandoa wengi hili limekuwa tatizo mwanaume kiguu na njia asb mchana na njia kumuacha mama na watoto.

Nini kifanyike hasa weekenda Mwanaume ashinde NYUMBANI akikupumzikia??

Zipo njia nyingi mojawapo SUPU YA WEEKEND NA MAZUNGUMZO NA MKAO

Ni kweli wanawake wengi hamjuagi kuwakalisha waume home.

Anza hivi
Siku uko home wewe amka mapema kabla yake anza makeke jikoni…

Mara blenda priiiii… juice… ama milk shake…. hahahaha..Utaona anasogea jikoni..

Wakati anakunywa juice ama milk shake…Anza kukuna nazi…

Chambua mnafu…

Hapo jikoni kuna kanyama kanachemka… katia kitunguu tupia viazi 2 na ndizi.Hahaha..

ile harufu ikianza kutoka utasikia anafuata maji jikoni… hahahaha kwenye friji… wala hatumi..

Hahaahha… utasikia nini kiko jikoni?Hahahaa.

Mmiminie supu…

Na ndizi mbili na kiazi kimoja kapilipili mbuzi pembeni..

Muulize kuna chapati…Mpe.. hahahahaha..Akimaliza supu nakuapia atasinzia..

.Akishtuka ugali na mnafu na nyama umeiva…Mpe ale..Mshushie na glass ya mtindi…Hahahaha..

analewa full Hata kama kuna mama junior anaambiwa usipige…

Hahahahahaha….Baada ya hapo acha apumzike… aoge…

Kisha funga ka khanga kako kepesi jilaze pembeni.. woiiiiiiiii..

Mkimaliza muombe pesa ya sokoni…

NAKUAPIA HATA KAMA JANA YAKE ALIKUPA ATAKUPA TENA.

Hahahahaha.. jamani…

Hahahahaha… yani kwa raha ya supu… nakuapia utaambiwa hata mama alipiga simu jana… hahahaha.. ama utasikia mamii.. njoo uone njoo… unaitiwa kitu cha kwenye tv.. hahaha.

Hata hujaona mwanzo ila kwa raha yakasupu utaitwa…

Hata kama huna kalio nakuambia utapigwa kibao hata cha mgongo…. hahahahahahahahahaha.

Sasa wewe unaamka chai na mkate kama chuo cha uhazili…
Wali maharage kama jeshi la j

Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi

*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!

Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.

1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu…”

Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”

🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂😂😂😂_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_

Kweli tamaa ni mbaya, mke wa mtu kaponzwa na tamaa, ndio basi tena

Jamaa kaenda kwa mke wa rafiki yake:
JAMAA: Shem nakupenda!
MKE: Hebu toka hapa! Je rafiki
yako akijua? tena koma!
JAMAA: Ntakupa milioni 1!
MKE: Basi njoo kesho mchana
mume wangu akiwa kazini!

Kesho yake Jamaa kaja
na milioni 1 wakamalizana na mke wa rafki yake,
jioni ilipofika
Mume akarudi home na
kumuuliza Mkewe, “Rafki yangu SAM kaleta hela yangu milioni 1?”
MKE akajibu kwa unyonge, “Ndio!”
MUME: Yes! Ndio maana nampenda SAM kanikopa asubuhi jioni karejesha!!!!
Mke hoi……

Kilichotokea baada ya kichaa kumfumania mke wake na mwanamme mwingine

Jay akaruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospital ya Vichaa, akapakiwa ktk ambulance hadi karibu na nyumbani kwake, akaulizwa unapakumbuka? akajibu ndio nyumba yangu ileee, mara wakatoka watoto wawili wamevaa uniform akasema watoto wangu walee wanakwenda shule.. akatoka mwanamke akasema na mke wangu yulee, ghafla akatoka mwanaume Jay akasema na mimi yule naenda kazini. hivi Jay kweli kapona?

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About