Vichekesho Vya Krismass

Tofauti ya ukopaji wa mzungu na mswahili

MZUNGU: Hi, I need $100, will pay back on Monday

MSWAHILI: Kaka vipi, shwari? Dah.. hatuonani mzee, mishe vipi, mnatunyima nini? Juzi nimekuona kwa mbaaaliโ€ฆ mzee shavu dodo, full kipupwe! Sie tupo bwana, shida tu, afu misiba mingi tu, wife nae kajifungua ghafla. Sasa, kuna cheque naisubiri haijatoka hadi leo, wanasema itatoka next week, hapa nimekwama kweli. Naweza pata ‘Laki Moja’ ya karibu hapo nitarudisha mwisho wa mweziโ€ฆ?๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Hii ndio ngoma droo kwa wanaume kati ya wanawake

{ NGOMA DROO}
Sikuizi utawasikia wadada wakisema kuachwa na mwanaume asie na pesa nisawa na kuluhusiwa hospital

{Sasa na sisi} wanaume tunasema
Kuachwa na demu mpenda pesa nisawa na kumaliza mkopo benk ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Wanaume atutakagi ujinga!!!! Wanaume heeeeee๐Ÿƒ๐Ÿพโ€โ™‚๐Ÿƒ๐Ÿพโ€โ™‚๐Ÿƒ๐Ÿพโ€โ™‚๐Ÿƒ๐Ÿพโ€โ™‚

Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa

Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia

“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”

Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.

#UTOTO RAHA ๐Ÿ˜‚

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ‘†๐Ÿป๐Ÿ‘†๐Ÿป๐Ÿ‘†๐Ÿป

Soma huyu mtoto anachosema sasa, Ndoto za watoto bwana! Kazi ipo!

Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?

ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe Nehemiah ??
Nehemiah : mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiweโ€ฆโ€ฆ”
Akameza mate kisha akaendeleaโ€ฆ.
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa Nehemiah .!!

Kuna watu makauzu ila huyu kazidi.. Soma hii!

Kakubaliana vizuri na msichana fulani hivi kuwa aibuke gheto, mchizi kajipanga vizuri kabisaโ€ฆ. mara saa nne hivi mdada kasema hana nauli.
Mshkaji kajikunja kamtumia Elfu tano maana mwenye shida alikuwa ni yeyeโ€ฆโ€ฆ
Baada ya nusu saa yule dada akamtumia meseji.
“Jamani mpenzi, kumbe baba hatoki nilijua atatokaโ€ฆ sorry bae sitaweza kuja kwa leoโ€ฆ sooo sorry!”
Mshkaji jiii! hajajibu kituโ€ฆ..

Baada ya muda kidogo meseji ikaingia katika simu ya binti, akajua mchizi kajibu. Mh! kutazama ni meseji kutoka Mpesa.

“CA90F0511 IMETHIBITISHWA Tshs 5000 ILIYOTUMWA KIMAKOSA KATIKA ACCOUNT YAKO IMETOLEWA SALIO LAKO NI Tshs 5”

Halafu ndo ikaingia meseji ya mshkaji.
“BASI POA SIKU NYINGINE KAMA VIPI”

#dada wa watu mashavu yakamshukaโ€ฆ hakuamini kilichotokeaโ€ฆ. yaani jamaa keshawapigia Voda na pesa fasta imezuiliwaโ€ฆโ€ฆ

Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo

๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜ .. TABU KUDATE NA MADEMU WA CHUO
Demu ;ย Baby Safari Hii Nataka Pale Hostel Niwafunike Mashoga Zangu Wote.
Jamaa ;ย Poa Sweetie Ondoa Shaka Nitakununulia #Turubai Utawafunika Woteโ€ฆ!!!
Demu:ย Mxiuuuuuuuu Lione Sura Kama Goti La mbuzi Na Namba yangu futa Nakublock Mpaka Sanduku la postaโ€ฆ!!!

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚nmecheka adi nmelazwa

Angalia kilichotokea baada ya dogo kupewa ada na kuitumia kubeti

Dogo kampigia simu baba yake;
DOGO: Baba katika zile shilingi laki mbili ulizonipa
nikalipe ada nimetumia shilingi alfu 30 kubeti
BABA : Unasema nini we mpumbavu mshenzi
mkubwa? Nimekukanya mara ngapi kuhusu kubeti?
DOGO : Lakini baba
BABA : Lakini baba nini ngoja urudi utaona
ntakachofanya.
DOGO : Nilitaka kukwambia kuwa nimeshinda
shilingi milioni 3
BABA : Ndio hayo ninayosema wewe mpumbavu
sana kwanini hukutumia laki nzima kubeti? Si
ungepata pesa nyingi zaidi? Ngoja urudi niwataarifu
ndugu zako kuhusu uulivyo na akili za kuamua
haraka mwanangu mpenziโ€ฆ

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Je, Chuoni kwako Kukoje?

FACT!
1.Ukiona geto lina feni, sabufa, meza ya plastic na kitanda ch sita kwa sita na Pc UJUE ni jamaa wa UDSM.

2. Ukaona geto lina nguo nyingi za watu tofauti tofauti, unga mwingi, vtunguu vng, nyanya halaf pembeni, Vitabu vya kutosha na lundo la karatasi za betting ujue huyu JAMAA ni wa SAUT.

3. Ukaona geto halina kitu ndani zaidi ya mkate wa bakheresa na kopo la maji UJUE huyu jamaa ni wa UDOM๐Ÿ˜‚โ˜

4. Ukaona geto lina visamaki vikavu mezani, Notes za kutosha mezani na jaba pembeni UJUE huyu ni MJAMAA WA MWENGE/MWECAU๐Ÿ˜œ๐Ÿ‘ค

5. Ukaona geto lina Mawigi mengi na dressing table pembeni, ngazi ya kuwekea viatu UJUE huyu mjamaa ni wa RUCO IRINGA๐Ÿ˜˜

6. Ukaona geto lina spray za kila aina, Nguo nyingi hasa za mitumba ambazo zimemodolewa mpaka tight UJUE huyu MJAMAA ni wa USHIRIKA MOSHI.

7.Ukiona geto lina Nyanya na mikungu ya ndizi halafu halafu nje kuna jiko la Mkaa UJUE huyu mjamaa ni wa TEKU mbeya๐Ÿ˜ณ

8. Ukiona geto lina tranka na nje wamevulia buti, viatu vya matope UJUE huyu Mjamaa ni Wa SMUCO MWIKA.

9. Ukaona geto ndan mashuka ya kimasai kinabao, hapa usipatwe na Mashaka, Jua huyu ni Mjamaa wa MAKUMIRA. ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ

10. Ukaona geto lina vimodo, vimini, miwani za tittled, jiko la mafuta ya taa, kitandani mito zaidi ya Minne,Visarafu kwenye meza, Tshirt nyingi za semina za family planning, Ukimwi n.k halafu chini tv ya chogo na king’amuz cha continental Ujue huyu MJAMAA ni wa TIA DSM ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ๐Ÿ˜ฑ

โฌโฌโฌโฌโฌโฌโฌโฌโคตโฌ๐Ÿ†™๐Ÿ†™๐Ÿ†™๐Ÿ†™
JE, KWAKO KUKOJE? ???
๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹๐Ÿ˜‹

Kichekesho cha mke wa mvuvi

CHEKA KIDOGO

MVUVI MASKINI NA MKEWE MALAYA.
Mvuvi mmoja alikua akiishi na mke wake huku
akiwa hajui kama mkewe malaya,
Leo hii kamuaga mkewe baada ya kuondka
mkewe akaanza kuingiza wanaume kama
kawaida
Hawara 1;nakupenda
Mke Wa Mvuvi;oke, Nipe Penz Haraka Kabla
Mume wngu hajarudi.
Hawara 1;oke!
Basi picha likaanza wakati wanaendelea mara
mlango ukagongwa, akamwambia hawara mume
wangu huyo jifiche darini jamaa akafanya,, mke
wa mvuvi akaelekea mlangon kumbe alikua
hawara 2.
mke wa mvuvi; aaahaa kumbe ni wewe nilijua
mume wangu bas njo haraka kabla mume wangu
hajarudi..
picha likaendelea huku wa darini akiona vyote,
mlangon kukagongwa
mke wa mvuvi; mume wangu hyo jifiche uvungun
jamaa akafanya kisha mke akajikoki kumpokea
mumewe,
mke wa mvvi; oooh! mume wngu pole umechoka
eeh leo umepata samaki mkubwa nashukuru sana
tulikua hatuna mboga
mvuvi;usinishukuru mimi mshukuru aliye juu.
hawara 1; sipo mwenyewe mwingine yupo
uvunguniโ€ฆย 

Kisa cha mzaramo na mchaga

MZARAMO V/S MCHAGA.
Mzaramo alitangaza anatibu magonjwa yooooooote
kwa tsh. 100,000/=
Na kama akishindwa kukutibu anakurudishia laki
yako nakukuongeza laki nyingine.
MCHAGA akaona hii fursa yakujipatia hela aiwezi mpita akaenda kutibiwa.
MZARAMO: “unaumwa nini?”
MCHAGA: “Sisikii ladha ya aina yoyote mdomoni kabisaaaa..”
MZARAMO: “sawa, toa laki kabisa..”
Mchaga akatoa.
MZARAMO akamuagiza msaidizi wake; “Naomba kikopo no.27 mpe anywe huyu..”
MCHAGA akanywa akatema faster; “Puh puu puu, Aisee huu si mkojo huu..?”
MZARAMO: “Umepona karibu tena..”
Mchaga aka-mind sana Kesho yake akarudi tena hakuamini ameliwa pesa yake.
MCHAGA: aisee nina tatizo la kumbukumbu nasahau
sanaaaaa..”
MZARAMO akamwambia “hakuna tabu, toa laki tukupe tiba..’
MCHAGA akatoa pesa akijua leo lazima afanikiwe..’
MZARAMO: “nesi naomba kikopo no.27..”
MCHAGA: “ASA CHALII ANGU HICHO SI CHA JANA CHA MKOJO HICHO AISEE..?”
MZARAMO: “UMEPONA KUMBUKUMBU UNAYO.

๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜

Cheki nilichomfanyia boss wangu

Bosi wangu karudi safari yake kutoka serengeti..! Si akanitumia picha, lakini ilikuwa network yenyewe tabu.. kwahio picha haikufunguka na kwa vile niliona itachelewa kufunguka na ataona sikumjibu basi nami..

Nikampelekea msg nikamuandikia umependeza saana bosi mashaallahโ€ฆ!!
sasa baada tu ya kumfika msg.. na huku picha ikafunguka kumbe picha ya Sokwe..!!
Basi Kaniambia kesho niende ofsini kwake kuna barua yangu..
Nahisi hyo barua ina pesa, hapa cjalala, nmekosa usingizi kabisa,nawaza ninunulie nn hyo pesa.Na kesho asubuhi sa 12 asubuhi atanikuta ofisini kwake naisubiri barua, sipendagi ujinga mimi.

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    Kitabu cha SMS Maalumu kwa Umpendaye
    Kitabu cha SMS Maalumu kwa Umpendaye
    1 X Sh2,500 = Sh2,500
    ๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About