SMS Nzuri: Meseji za Vituko Vya Kukupa Mood Mpya
Angalia huyu demu alivyo mbulula
Jamaa aliamua kumtoa demu wake out kwaajili ya chakula cha usiku kufika hotelini wakakaa mezani mhudumu akaja,
Mhudumu: kaka nikuhudumie nini,
Jamaa: afathal NILETEE MENU LISTI
Mhudumu: dada na wewe?
Demu akajibu kwa pozi tena kwakujishaua, “NA MIMI NILETEE MENU LIST ILA USIWEKE CHUMVI NYINGI”
Chezea mbulula weweโฆ!!!
Swali la kizushi kwa wadada wanaovaa mawigi
Hivi wadada mnaovaa mawigi.
๐๐ฝย Utajisikiaje siku Boyfriend wako anaingia chumbani halafu anatundika NDEVU kwenye henga๐คฃ
Hii mitoto mingine mijinga, cheki alichokifanya huyu
Nimeamka asubuhi nikiwa na elfu 1 tu mfukoni, nikamtuma mtoto wa jirani akaninunulie maandazi nipate kunywa chai. Baada ya muda namuona anarudi huku analamba askrimu ya AZAM kama Simba vile. Nikamuuliza maandazi yako wapi? Akanijibu eti wakati anafika yanapouzwa maandazi akagundua kuwa kapoteza hela yangu, hivyo akaanza kurudi, ila bahati nzuri wakati anarudi ili kuja kunitaarifu kuhusu kupotea kwa hela yangu, njiani akaokota elfu 1 ambayo kuna mtu alipoteza ndio akaamua kununua askrimuโฆ.kwa sasa niko polisi na mtoto yuko dispensari na mamake๐๐๐๐๐๐๐
Angalia haya maswali ya huyu mtoto yalivyomagumu, ndio maana wazee wetu walikua wanatudanganya
Mtoto: Mama, hivi kabla hujanizaa uliniona!?
Mama: Hapana mwanangu sijakuona.
Mtoto: Kwahiyo ulivyonizaa ulijuaje kwamba ni mimiโฆ!??
Angalia huyu mgeni anachokifanya, wageni wengine ni hatari
Hata kama ni Mgeni this is too much.
Mwenyeji: Karibu mgeni karibu ukae,utapenda chai au soda?
Mgeni: Nipe nianze na soda wakati chai inachemka.
Mwenyeji: Utakunywa fanta au sprite?
Mgeni: Nipe fanta wakati sprite inapoa.
Mwenyeji: Utakunywa na keki au mkate?
Mgeni: Nipe keki mkate nitanywea chai ikishachemka.
Mwenyeji: Utapendelea ndiz au machungwa,
Mgeni: Nipe machungwa ndizi ntakula na wali
mchana.
Chezea mgeni ww.!!!
Angalia alichokifanya huyu mkaka alipoenda benki ๐ฆ
At the bank..
Teller: Hii pesa ni fake
Mkaka: Shida iko wapi..pesa ni yangu..account pia ni yangu..weka tu!!!๐๐๐
๐๐๐๐
Angalia nilivyookoa maisha ya mtu leo
Nmeokoa maisha ya mtu asubuhi ya leo huwezi amini.Nmekutana na ombaomba nikamuuliza atajisikiaje nikimpa sh.30,000/-
Akasema ATAKUFA kwa furaha.Nikaondoka bila kumpa ili ASIFE.๐๐๐๐
Namna wazazi wanavyoongea na mabinti katika umri tofauti
Miaka 13: Usipende wavulana ni wabaya.
Miaka 18: Sitaki nikuone na yule mvulana tena!
Miaka 23: Lini utatuletea mchumba wako?
Miaka 26: Wenzio wanaolewa.
Miaka 30: Tumekuambia kwamba acha
kuchagua sana wanaume, hutaki kusikia!
Miaka 33: Kuna mtu wa Mungu yupo kule
anaombea unaweza kupata mchumba
Miaka 36: At least pata mtoto mmoja.
Miaka 39: We will take care of all the wedding
billsโฆyeyote ni sawa sisi tutagharamia kila kitu mwanetu wee mlete tu .
Miaka 45: hivi kweli nani alikuroga.?
๐๐๐ changamkia fulsa umri ukifika
Hii ndio ndoto ya harusi ya kila msichana anayotamani
GIRL: Baby, hebu niambie harusi yetu itakuwaje?
BOY: Yaani hii haijawahi kushuhudiwa, ngoja nikupe kionjo kidogo tu
GIRL: Enheeโฆ
BOY: Kwanza siku ya kupeleka mahari nitaswaga zizi zima la ng’ombe napeleka kwa babu yako
GIRL: Ooh baby u care..
BOY: Siyo hivyo tu, baba yako ntamnunulia Range Rover Sport na mama mkwe ntampa Range Rover Evoque
GIRL: Baby u are awesomeโฆ
BOY: Halagu mdogo wako wa kiume ntampa Prado Tx, na hapo nimesukutua tu mdomo sijaanza kulaโฆ.
GIRL: Enheeโฆna sisi??
BOY: Sisi tutachukua mtaa mzima Oysterbay, kila wiki tutaishi nyumba tofauti
Halafu siku ya harusi yetu tutakodi zile meli zinabeba makontena ndiyo iwe ukumbi wetu, itatupeleka hadi Maldives
GIRL: Baby I love you
BOY: Tukitoka hapo tunaenda honeymoon Bahamasโฆ.halafu tunaenda Taiwan shopping ya fenicha, kisha Japan shopping ua electronics, halafu tunaenda Dubai nikununulie vito vya thamani
GIRL: Ooh my sweetheartโฆhalafu tukitoka huko??
BOY: Tukitoka huko nachukua ndoo ya maji nakumwagia uzinduke usingizini na ndoto yako imeishia hapo
Duh! Hiki nacho chombo cha moto?
_Sheria inasema kila anaetembea na chombo cha moto barabarani sharti awe na leseni._
_Sasa hawa wauza kahawa mbona wanatembea na chombo cha moto lakini hawakamatwi ๐ก._
_Hizi sheria zinapendelea._
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Bangi si mchezo, Angalia kilichowakuta hawa
Bangi si mchezo!
Jamaa kaikoleza si ikamtuma avue nguo!
Akavua nguo zote akaenda kwenye kioo, kujitazama akaona kama kavaa suti!
then akaenda kama alivyo zaliwa kwa masela wenzake akawauliza vp suti imenikaa? Mvuta bangi mwenzie akamwambia “imekutoa kinyama ila tai umeifunga chini sana”.
Soma alichojibiwa huyu mzee baada ya kudai kutaka kumsikiliza Nyerere
Mzee: Dereva ongeza sauti tumsikilize Mwalimu Nyerere!!
Dereva: ungemsikiliza mwalimu wako miaka iyo saivi ungekua na gari yako
๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐ ๐
Sitasahau mwaka huu
Sitasahau mwaka ule ambapo nilipeleka barua ya maombi yangu ya kazi kwenye kampuni moja maarufu. Wakati nasubiri majibu siku moja nikaenda kwa mama ntilie kununua maandazi akanifungia vizuri, kufika nyumbani hamu yote ya maandazi iliniishia pale nilipogundua karatasi iliyofungiwa maandazi ni barua yangu ya kuombea kazi๐๐
Hii kazi kweli kweli, Ungekua wewe ungefanyaje?
UNATOKA SEBULENI UNAENDA ZAKO CHOONI UNAINGIA TU HIVI GHAFLA UNAKUTANA NA MZIGO MKUBWA WA MAVI JUU YA CHOO ALAFU UNAAMUA KURUDI ZAKO ILE UNATOKA TU UNAMUONA DEMU MZURI ULIYEMTONGOZA JANA ANAKUJA KUINGIA CHOO ULICHOTOKA WW NA KINA MZIGO WA MAVI JUU NA AMEKUONA WW NDIO UMETOKA MLE NDANI ..unaamua kurudi ili uka flash bahat mby maji hakuna.!!!
๐๐๐HAPO NDIO UTAJUA KWANINI SIKU HIZI HATUPENDI UJINGA๐๐๐๐
Angalia huyu ticha wa Hesabu alichofanyiwa
Looku Looku* ๐๐
*Ama Kweli Mkuki Kwa Nguruwe kwa Binadamu Mchungu Skia Hiiโฆ.!!*
*Ishawahi kutokea Pale nilipokutana njiani na mwalimu aliyekufundisha MATHS secondary afu akaniambia nimuelekeze njia ya kwenda sehemu fulani.*
*_Nenda mbele kama 2KM hivi kisha kata kushoto,ila hakikisha ANGLE inakuwa ni 30.5 KUSINI MASHARIKI.Kisha tumia PYTHAGORAS na hakikisha una FOUR FIGURE ili kupata thamani ya ANGLE._*
*Mwalimu alisonya na kuondoka.*๐๐๐๐๐
*Stakagi ujinga kabisa mimi, wakati ananichapa alifikiri sifa*๐๐
๐ ๐๐ฝ๐๐ฝ *Mniache Tuu Mimi Sio Kwa Bifu Ilo Aiseee*๐๐พ
Huyu bibi kweli kiboko, cheki alichofanya akiwa na babu
Bibi na Babu walisafiri wakielekea kwa mtoto wao ambae hawajamuona zamani.
Walipofika njiani wakawa wamechoka Sanaa. Wakaamua kutafuta hotel ili walale.
Wakakubaliana walale kwa masaa 4. Wakalala, Walipoamka, mfanyakazi wa Hotel akawatoza Tsh. 500,000/=
Wale wazee wakashangaa hata kama ni hotel ya kisasa lakini sio laki tano kwa masaa 4.
Babu akagoma kulipa akasema aitiwe meneja.
Meneja akaja kuwasikiliza
Babu: ” Kwanini bili ni kubwa hata kama ni hotel ya kisasa?”
Manager;“kuna maswiming puli, ya kisasa “
Babu; “Lakini hatukuyatumia”
Manager; “Ah ah ah. Lakini mungeweza kama mngetaka”
Babu: “Hata hivo bado haithamini kuwa laki 5”
meneja: “Pia Kuna waimbaji kutoka sauzi, Uganda , Congo”
Babu: “Lakini sisi hatukuwasikiliza”
Meneja: “Ndiooo. Lakini mngeweza kama mngetaka”
Babu; aka give up na kumwambia mkewe andika cheki uwape,,
Bibi akaandika akampa meneja.
Meneja anaangalia anaona sh. 50,000
Akashangaa na kusema. “VP mbona hamsini'”
Bibi akajibu “450,000 ya kulala na mimi”
Meneja akajibu; “Lakini sijalala”
Bibi :“ungeweza kama ungetaka”
Ingekua wewe ndio baba au mama ungefanjaje?
Baba na mama baada ya kurudi safari pamoja wakakuta BARUA iko mezani SEBULENI ikisemaโฆ. “Baba na mama, ni matumaini yangu kuwa mtasoma ujumbe wangu huu kwenye karatasi niliyoiweka
juu ya meza, naomba msishtuke mana ni mambo ya kawaida kwenye maisha tunayoishi, najua mtaumia kwa vile bado nasoma na ndiyo nipo kidato cha kwanzaโฆ” Napenda kuwajulisha kwamba sasa hivi mnaposoma hii barua sipo nyumbani, nimetoroka mana nimegundua
nina uwezo wa kujitegemea kwa sababu mi ni kijana mwenye umri wa miaka 14 na ninajua kipi chema na kipi kibaya.
Tangu mwezi mmoja uliopita nilikuwa na uhusiano nabinti mmoja aliyeitwa Rachel, mwenye umri wa miaka 27 na kwa sasa
ndo naishi naye kwenye chumba alichopanga. Nilipokuwa nyumbani sikuwa napata hela za kutosha ila sasa nimeanza kushika noti za shilingi 10,000โฆ Msichana niliyenaye ni mzuri sana wa umbo na ninampenda sana, amenifundisha njia za kutafuta hela.
Amenipangia kazi ya kuuza madawa ya kulevya na yeye ikifika
usiku anaenda kuuza mwili wake, basi kila siku tunapata hela ya kutosha, huyu mchumba wangu ni msichana mwenye bidii, kwa siku analala masaa 6 tu maana mwanaume yeyote akija lazima awe naye
chumbani kwa muda wa masaa 3.
Msiwe na hofu, nipo salama kabisa na nimeamua kumwoa Rachel mana ni kila kitu kwangu. Pia amenunua gari la kubebea mbao kwahiyo biashara inaenda vizuri.
Rachel ameenda kupima afya na amekutwa na upungufu wa kinga
mwilini, mara nyingi namridhisha anapotaka kitu flani, iwe kufanya naye mazoezi ya viungo au kufanya naye mapenzi, si mnajua unapokuwa na mgonjwa unakuwa naye karibu.
Ila mi pia sijihisi vizuri mana kila saa nakohoa tu na sina uhakika kama nimeathirika. Tumepanga baada ya miaka miwili tutawatembelea, nadhani mpaka miaka miwili iishe atakuwa
ameshajifungua, na ni furaha yangu mtamwona mjukuu wenu. Wazazi wangU, sina la kuongeza kwaherini Mungu
akipenda tutaonana.
NB: “Baba na mama, mimi nipo chumbani kwangu najisomea,
mnachokisoma ni h/work ya mwalimu wa kiswahili alituambia tutunge hadithi fupi ya kusisimua, naomba muiangalie kama kuna
makosa!”
Ingekuwa wewe hapo ndi baba au mama ungefanyaje? SHARE na wenzako wasome.
Alichojibu dalali baada ya kufumwa na mke wa mtu ndani ya nyumba ya kupanga
Dalali aliwatafutia jamaa chumba Buguruni karibu na reli, nyumba nzuri sana. Jamaa na mkewe wakahamia kwa furaha, lakini furaha yao iliisha walipokuja gudundua nyumba ile iko karibu mno na reli treni ikipita mpaka kitanda kinacheza.
Siku hiyo dalali akapita mke akamwita na kumwambia tatizo wakati treni inapita, wakaanza kubishana, yule mama akamwambia dalali kwa kuwa kuna treni itapita sasa hiviโฆ njoo ndani uone mwenyewe.
Bahati mbaya wakiwa wamejilaza kitandani ili dalali aone adhabu wanayopata, Mzee mwenye mali alirudi ghafla, akauliza,
‘Nyie mnafanya nini hapa?’
Masikini dalali kwa woga mkubwa akajibu’ Tunangoja treni’
Sifa mbaya: Cheki kilichompata huyu mwanaume mpenda sifa
SIFA MBAYAโฆ
Jamaa alikuwa ndani ya daladala Mara simu ikaita alikuwa ni mkewe kwa sifa jamaa akaweka loud speaker ili watu wasikie wanavyopendana.
JAMAA;wife Mara hii umenimiss jaman
WIFE; kwa nini umekunywa uji wa mtoto?!!!
๐๐๐๐๐
Recent Comments