SMS Nzuri: Meseji za Vichekesho Vya Jumamosi
Angalia nilichomfanyia huyu dereva sasa
Tulikua kwa basi tunaelekea arusha,ile namcheki dereva kumbe ni best yangu na basi ilikua kwenye spidi hatari, nikaenda kumziba macho nkamuuliza otea mi ni nani, kabla hajanijibu nikasikia kishindo kikubwa sana
NA SASA HIVI NIMEZINDUKA NIMEONA ABIRIA WOTE TUPO WODI NAMBA 3 HAPA KCMC MOSHI. 🤕🤕🤕🤕
SODA ZA WAGONJWA PLIIIZ!!! 🙏🙏🙏🙏🙏
Ujinga wa ndoto ndio huu
👉Ujinga wa ndoto ndiyo huu
••Utaota umeokota dolla ukiamka empty…
••Utaota umeokota dhahabu ukiamka kitandani patupu daadeeki OTA Sasa UMEKOJOA…..
😂😂😂😂😂😂
Mkwe kazua mpya, Hii dunia ina mambo sana
Mama mkwe alimuuliza mkwewe “binti” samahani mbona mtoto hajafanana na mwanangu kabisa?
Binti akajibu, “bila samahani mama huku chini nina njia ya uzazi sio mashine ya photocopy”
mama mkwe hoii!! Chezea Wakwe Wa Bongo wewe.
Safari ni safari
FUNDISHO : SAFARI NI SAFARI
Maisha ni ya ajabu sana, wakati mwingine maisha ni mazuri na mwingine ni mabaya, katika maisha yetu tumeshapitia safari nyingi sana na za aina mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Lakin kiukweli kila safari ni safari tuu.
Japokua kila safari ina changamoto zake lakini mwisho wake ni ule ule , kila safari ina uzuri na upekee wake.
Vile vile kila safari ina ubaya wake, kwa mfano kila safari ina gharama yake kulingana na upekee wake.
Usiwe na wasiwasi na mashaka na aina ya safari ulionayo, jipe moyo utaimaliza na kupata ulichokitarajia. Haya ndio maisha na wote tunatakiwa tuyafurahie.
Ingawa kila mtu ana safari yake bado wote tunatakiwa tufurahie pamoja kwa safari tuliyo nayo. Hata Uwe Na safar ya aina gani wewe furahi tuu. Hii ni kwa sababu safari mwisho wake ni mmoja kwa wote burudani ni ile ile
Safari🍺 ni safari 🍺hata kama ni ya chupa au ya kopo mwisho wake 💤💤
😋😜😜😂😂😂
Ulijua ni nn??
Hiki ndicho kifo mbele ya Mwanamke
Hiki ndiyo kifo.
KIFO NI NINI..
Kifo ni pale girlfriend wako anapofanya fujo Club akiwatukana MABAUSA Huku akisema
“BABY WANGU HATA HAWAOGOPI”
😀😀😀😀
Angalia huyu bibi alichotufanyia kwenye gari
tulikua kwenye gari kibao ad wengne mlangon likasmimama kituo kimoja kulikua kuna bibi anataka kupanda
Konda- bibi twende sit kibao ata utalala
Bibi – oooh sawa mjukuu
Konda – simama tu apo wanashuka mbele
Bibi – akacheka sana tu
Konda- mbona unacheka bibi
Bibi – mjukuu hawa wote hawashuki wanakufa apo mbele
Watu- simamisha gar
Saiv bibi kabaki mwenyewe amelala sit ya nyuma😆😆😅😂😂
Angalia huyu mwanafunzi anachomjibu huyu mwalimu wake
1. Ticha:”Punda ni mnyama anaefugwa nyumbani,lakini akiwa mwituni anaitwa pundamilia….Je sungura anayeishi mwituni anaitwaje?”
ZUZU:”Sunguramilia.”
2.Ticha:”Rais wa kwanza wa kenya aliitwa KENYATTA…Je rais wa kwanza wa
Tanzania aliitwaje?”
ZUZU:”TANZANIATTA.”
3. Ticha:”Kuku yuko katika jamii ya NDEGE…Je samaki yuko katika jamii ya nini?”
ZUZU:”MELI.”
4. Ticha:”Coach wa Arsenal anaitwa ARSENE,wa Man-city anaitwa MANCINI….Je wa
Liverpool anaitwaje?
ZUZU:”LIVER.”
5 Ticha:”Ukiwa na mbuzi 10,wezi waje waibe 5,utabaki na nini?”
ZUZU:”Hasira nyingi sana!”
Vituko vinavyoandikwa kwenye daladala
Huwa naenjoy sana kusoma yaliyoandikwa nyuma ya daladala hasa ninapokuwa kwenye foleni. Misemo maarufu
ya kwenye daladala.
1.Yatima hadeki
2.Utamu wa chips mimba
3.Ukitaka kujua ugumu wa kudai kopesha ukweni
4. Usiyempenda kaja
5. Kobe hapimwi joto
6. Acha kazi uone kaz kupata kaz
7. Ukichezea koki utalowa
8. Heshima pesa kipara kovu tu!
9. Mtumbwi hauna saitmira.
9. Silaha pesa bastola mzigo
10. Hata uoge mjini huendi
11. Chezea mshahara usichezee kazi.
12. Ukiona manyoya ujue kishaliwa
13. Ikisimama Panda
14. Pombe pombe tuu kunywea bar mbwebwe
15. Njia ya chooni haioti nyasi
16. Likizo ya maskini ugonjwa
17. When i grow up i want to be a scania
18. Hata bibi alikuwa binti
19. Kisigino hakikai mbele
20. Kama mapenz pesa kaolewe na benki
21. Hata barabara ina matuta lakin huwez panda viazi
22. Mavi hayana miba lakin ukikanyaga lazma uchechemee
23. Paka haishi kwa msela
24. Ukipendwa ujue kuna boya kaachwa
25. NIPO NIPO KWANZA
26. Mchana nzi ucku mbu
27. Ucmshangae funza kukata viuno ndio mwendo wake
28. Kama umelipenda(gari) bonyeza nyota liwe lako
29. Supermarket hawauzi mkaa
30. We nisubiri mi nakungoja.
31. Zetu dagaa kuku tamaa
32. Hata uwe na heshima vipi huwezi kumpokea askari bunduki
H
😆😆😆😆😜😜😜😝😝😝
Share na wenzako kuongeza siku za kuishi
Njia nne za kufikisha Habari kwa haraka
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuni…unaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuni…😂😂😂😂
Maswali ya kijinga yakijibiwa vizuri
Haya ndiyo majibu mazuri😁😁👇👇👇👇👇👇👇👇
Q: Umenyoa nywele?
A: *Hapana, nimebadilisha kichwa.*
Q: Hiyo simu umenunua?
A: *Hapana nimeitengeneza mwenyewe.*
Q: Utakula mboga na nini?
A: *Mdomo*
(Simu inaita usiku,then aliyepiga anauliza) Q: Nimekuamsha?
A: *Hapana nilikuwa naota jua hapa nje.*
Q: Gazeti la leo linasemaje?
A: *Sijaongea nalo.*
Q: Gari limejaa, nitakaa wapi?
A: *Usijali dereva anashuka kituo kinachofata utapata kiti.*
Q: Hiyo ni ajali?
A: *Hapana ni driver ameamua kupark gari upside down* .
Q: Umepause movie?
A: *Hapana wamechoka kuact wanarest.*
😂😂😂😂😂😂
🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂
Hawa wanaume wanaopenda wanawake hovyo barabarani wamepatikana, hawatarudia 😂😂😂
Marafiki wawili (Jose na Ben) walikuwa wanatembea mtaani akatokea mwanamke akarusha busu kwa mmojawapo kupitia dirishani katika jengo la ghorofa tatu.
Wakaanza kujadiliana kama ifuatavyo:
Ben: Muone yule mrembo amenirushia busu
Jose: tafadhali achana na huyo mwanamke, usimjali..
(baadae yule mwanamke akamuashiria aende)
Ben: yule mwanamke ameniita!
Jose: Rafiki yangu, usiende. Nakutafadhalisha.
Ben: Kwa nini unaniambia nisiende Wakati mrembo kama yule ananiita? Huo ni wivu
Jose: Ben, Ninakutafadhalisha tena, usiende, tafadhali usiende kule (akihisi kutotiliwa maanani)
(Rafiki yake alimpuuza na alienda kwa yule mwanamke, mwanamke alishuka kukutana naye na wakapanda juu. Ghafla wakiwa wanataka kuanza taratibu za kula uroda, wakasikia mlio WA gari getini).. 🔊🔊
Lady: _(akiangalia kupitia dirishani)_
Oooh! Yule ni mume wangu!!
Ben: Mama yangu !
Nipo matatani, kweli ? ..!!
Lady: Usiwe na khofu, jifanye kuwa Dobi na anza kupiga pasi hizo nguo
(akimuonyesha lundo la nguo)
(Ben alitumia masaa matano kukamilisha kunyoosha zile nguo kwa sababu yule mume hakutoka tena siku ile)
(Siku iliyofuatia Ben alikwenda kwa Rafiki yake)
Ben: Kaka, unaweza kuamini Jana nimepiga pasi nguo kwa masaa matano???
Jose: Lakini nilikwambia usiende. Nguo zote hizo ulizonyoosha, Nilizifua Mimi Juzi!!
😂😂😂😂😂😂😂😂😂
When an experienced person speaks … 👂you must listen..!
Huyu mlinzi bwana
High school Flashback!!
.
Watchman : Amkeni muende morning preps.
Allan : Mimi ni mgonjwa.
Watchman : Unaumwa na nini hiyo?
Allan : Bionomial Nomenclature.
Watchman : Eeh, lala tu kijana. Hiyo kitu ni
mbaya. Imeuwa watu South Africa.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
#_Sipendagii ujinga kabisaa mimi
KICHEKESHO: Ukiona masikini Kachinja kuku
Ukiona masikin kachinja kuku basi kat ya kuku au yeye kuna mmoja atakua mgonjwa 😆😆😆😆
Angalia ndoto nyingine zilivyo na Majanga
Ndoto zingine bwana usiombe zikupate
Mimi usiku wa kuamkia Leo nikiwa nimelala nimeota naendesha gari Yangu aina ya BMW mpya Mara gafla ikakwama kwenye tope .hivyo ikabidi nishuke ili kuisukuma loh! Yani kudadeki ile kuamka nikakuta nimesukuma kitanda hadi sebleni Daaa ilinisikitisha sana jiangalie sana sese hivi ndio narudisha kitanda chumbani .angalizo angalia ndoto unazo ota unaweza kuota upo baharini ukaamka unajikukuta unaogelea kwenye Jaba la Maji shauri yako.
Alichokisema mwizi baada ya kushinda bahati nasibu
Hapa mtaani kuna mwizi sugu ameshinda mil.10 za bahati nasibu ??.
Alipoulizwa atafanya nini na hela nyingi hizo
Akasema anataka kupanua shughuli zake. Mimi sijamuelewa na sasa hivi watu wameanza kuhama mtaa…
😂😂
Angalia huyu house girl wa mzungu alichokifanya na anachokisema
House girl mmoja alipewa kazi na mzungu mara akavunja sahani.
Mzungu aliporejea,kazin akamuuliza ‘what happened to my plate?
House girl akajbu: ‘The dog wow wow friji paaa, mchuzi mwaaaa the vyombo pangalapangala the sahan ngelengenjee……the pasuka paaaaaaaa
😂😂😂😂hadi saiz mzungu bado anasoma dictionary hajui lugha gani imetumika
Huyu mme ni shida
MKE..mume wangu unaweza kuua simba kwasababu yangu???
MME: Hapana mke wangu, sema kingine
MKE:unaweza kunipa nione watsapp yako nione msgs?
MME: Haya sema huyo simba yukwap nikamuue
Cheka kidogo, angalia anachosema huyu mchaga
Mchaga baada ya kufa akaulizwa na malaika anayetoa roho: Mangi hapa ni njiapanda kulia ni Mbinguni na kushoto ni Jehanamu, Je unachagua kwenda wapi?
MANGI: Bwashee, mi nabaki hapa hapa njiapanda aisee.
MALAIKA: Kwa nini?
MANGI: Aisee, nikifungua duka hapa si nitapata wateja wa Mbinguni na Jehanam. Yani patakuwa senta ya hatari, supu na nyama choma muda wote. Hata we utafaidi, unavyoenda kuchukua roho unaniletea stock nakupa hela yako cash mkononi. Na kila ukipita hapa unapiga mchemsho wako wa ulimi na bia mbili chap kabla ya kuingia mbinguni.
Kwanza nashangaa Shirima alipitaje hapa bila kushika ploti, au alikufa amelewa sana?
Alichokijibu chizi baada ya kuanguka ghorofani
Chizi kaanguka toka kwenye gorofa fasta watu wakamfuata kumsaidia wakamuulza VP IMEKUAJE?
Chz akajbu: ”HATA CJUI NA MIE NDO NAFIKA SASA HIVI
Recent Comments