SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

๐Ÿคฃ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜‚

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Ilinde ndoto yako

Ndoto ni nini?

Ndoto ni zile ndoto za kiuhalisia ambazo mtu anaweza kuwa nazo akiwa macho na anatumia mawazo yake kutengeneza au kuunda picha ya maisha anayotamani kuishi siku zijazo. Hizi si ndoto ambazo mtu anaota usiku akiwa usingizini, bali ni matakwa ya dhati ambayo yanamfanya mtu ajizatiti na kutia bidii katika mambo anayofanya ili kuyafikia malengo yake.

Kila mtu ana ndoto tofauti ambazo anatamani kuzifikia, na mara nyingi ndoto hizi huwa zinaongoza maisha yake na kumpa dira na mtazamo wa maisha yake ya baadaye. Ndoto hizi zinaweza kuwa kubwa au ndogo, na zinaathiri jinsi mtu anavyochagua kuishi maisha yake ya kila siku, jinsi anavyofanya maamuzi, na hata jinsi anavyoingiliana na watu wengine.

Kwa mfano, mtu mwenye ndoto ya kuwa Rais atajituma katika masuala ya uongozi, atajifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na siasa na uongozi wa jamii au nchi. Ataweza pia kujihusisha na harakati mbalimbali za kijamii au kisiasa ili kujenga umaarufu na kuwa na uwezo wa kufikia ndoto yake.

Kwa upande mwingine, mtu anayetamani kuwa mwimbaji bora atajikita katika kuendeleza kipaji chake cha uimbaji, kuhudhuria mashindano ya muziki, na pengine atajitahidi kuwa karibu na watu wengine waliofanikiwa katika tasnia hiyo ili ajifunze mbinu za kufanikiwa.

Wale wenye ndoto za kumiliki vitu kama nyumba za kifahari, magari, au kuwa bilionea, mara nyingi wanajikuta wakihusika katika kufanya kazi kwa juhudi zaidi, kujifunza na kutafuta taarifa juu ya uwekezaji, na kutafuta njia bora za kukuza uchumi wao binafsi.

Ndoto za kutembelea nchi fulani zinaweza kumfanya mtu aweke akiba ya pesa, ajifunze kuhusu tamaduni mbalimbali, na hata kujifunza lugha tofauti ili kujiandaa kwa safari yake. Kwa kufanya hivi, mtu huyo anajiweka katika nafasi nzuri ya kufikia ndoto yake na kuifanya iwe halisi.

Kwa ujumla, ndoto za mchana ni muhimu sana katika kuhamasisha na kutoa motisha kwa mtu kufikia mafanikio makubwa maishani. Zinamfanya mtu kuwa na malengo, azimio la dhati, na muelekeo wa wapi anapenda maisha yake yawe siku za usoni. Ndoto hizi zinapoambatana na mipango mizuri na jitihada za makusudi, mara nyingi huwa na matokeo chanya na kutimia kwa matarajio ya mtu.

Zote hizo ni ndoto ambazo kila mmoja alikua nazo huenda ni kipindi anakua au hata sasa bado anayo.
Kwa bahati mbaya sana watu wengi wamekuwa na ndoto kubwa sana wakiwa wadogo na kuzipoteza walipoanza kuingia kwenye uhalisia wa maisha.

VITU VINAVYOWEZA KUIPOTEZA NDOTO YAKO.

Ugumu wa Maisha.

Maisha yanavyozidi kubadilika na kuwa magumu ndipo baadhi ya watu huanza kuasahu vile vitu ambavyo walikua wanatamani waje kuwa navyo. Maisha yanapokuwa magumu sana wengi huona haiwezekani tena wao kufikia ndoto zao hivyo kukata tamaa kabisa na kuamua kuwa na maisha ya kawaida.
Mtu anaweza kujitazama vile alivyo na kuona yeye hafananii kabisa kuja kuwa Rais wa nchi hii labda kutokana na familia aliyotokea au maisha yanayoendelea sasa hivi.
Nakuomba kama unapitia hali hiyo anza kuikataa kabisa ili usije kupotea.

Marafiki wabaya.

Marafiki na watu unaokuwa nao mara kwa mara wanaweza kuwa sababu kubwa sana kukupoteza kabisa na kukufanya wewe uache kupigania ndoto yako.
Ndoto yako ni ya thamani sana ndio maana inapata upinzani.
Ndio maana utaambiwa haiwezekani. Ndio maana watakucheka ukiwaambia wewe unataka kuwa Rais wa nchi hii au unataka kua Bilionea.
Mara zote watu wanakuhukumu kutokana na hali uliyonayo sasa hivi.
Unaweza kuachwa na Mpenzi wako umpendaye kwa sababu tu yeye anaangalia maisha uliyonayo sasa hivi na hata ukimueleza ndoto zako haamini kutokana na hali yako ya maisha uliyonayo sasa.

Ufanyeje?

Kaa nao mbali wale watu ambao hawana ndoto kama za kwako. Kaa mbali na watu ambao wanafikiri kama kuku. Yaani wao wamejiona kwamba ni maskini na haiwezekani kuwa tajiri labda kuiba tu. Inawezekana ni watu wako wa karibu sana labda kaka, dada, wazazi.
Ufanyeje?
Usikubali kuwasikiliza weka pamba sikioni. Mimi kuna mtu aliniambiaga hizo ni ndoto za mchana haziwezi kutokea kamwe lakini sijakata tamaa naendelea kufanyia kazi ndoto zangu.

UNALINDAJE NDOTO YAKO?

Iandike.

Kama unasema una ndoto lakini bado ipo kichwani bado hujaelewa maana yake. Katafute Notebook nzuri sana ya gharama Huwezi kuandika ndoto ya kuwa Bilionae kwenye note book ya elfu mbili aisee.
Tafuta notebook ya Gharama hata ya 20,000 ili uweze kuitunza vizuri. Andika kila kitu unachokitaka kwenye dunia hii. Hakikisha umeandika kila Kitu na usiache hata kimoja.
Hii ni njia ya kwanza ya kuilinda ndoto yako. Nikikutana na wewe sehemu Uniambie au unionyeshe kilipo kitabu chako cha ndoto. Andika ni Jinsi gani unaweza kupata vile vitu. Ni ujuzi wa namna gani unahitaji ili uweze kufikia ndoto zako. Ni watu wa namna gani unahitaji kuambatana nao ili ufanikiwe kwenye doto zako. Andika ni Baada ya Muda gani utakua umefikia Ndoto zako. Sasa hapa Ni somo jingine kabisa jinsi ya kuandika malengo. Malengo ya muda mfupi na Muda mrefu.

Soma ndoto zako kila siku Asubuhi na kabla ya Kulala.

Soma kila siku namaanisha kila siku asubuhi na jioni. Kwanini usome kila siku ? Unaichora au unaiingiza picha ya ndoto zako ndani ya ubongo wako hii itakufanya chochote utakachokutana nacho kama hakiendani na ndoto yako uweze kukiepuka na kama kinaendana basi uweze kukivuta. Unaposoma inajijenga kwenye akili yako na kutengeneza ukaribu wa wewe kuifikia zaidi.
Soma na tafakari.

Tenga Muda peke yako.

Hakikisha unatenga Muda wa peke yako angalau kila wiki ukiwa peke yako sehemu ambayo haina usumbufu wowote. Sehemu hiyo utakua unaipa akili yako nafasi ya kutafakari juu yako wewe. Jitazame ulivyo sasa halafu jitazame wewe ukiwa umefikia kwenye ile ndoto yako. Kama ni gari basi anza kujiona jinsi unavyoliendesha lile gari la ndoto yako. Kama ni Rais ebu jione ukiwa Ikulu basi Jione ukiongoza majeshi. Kama ni Bilionea anza kuona ukiwa Bilionea utakavyokua. Utakavyoweza kubadilisha maisha ya watu wengi sana Duniani. Ona jinsi dunia inavyofurahia Mungu Kukuumba wewe kwasababu maisha yao yamebadilika. Nashauri hili ufanye angalau lisaa limoja ukiwa peke yako bila simu wala kifaa chochote cha mawasiliano.

Soma Vitabu na Fanyia Kazi ndoto yako Kila siku.

Soma vitabu ambavyo vitakuza ufahamu wako ili wewe uweze kuifkia ndoto yako.
Kama unataka kuwa Rais wa Nchi lazima ujue kua unakwenda kuongoza watu hivyo vitabu gani usome ili ukuze ufahamu wako.
Unataka kuwa Bilionea hutaweza kuwa bilionea na ufahamu ulionao sasa hivi mali zote zinatakiwa ziongozwe na wewe hivyo jijengee tabia ya kujisomea vitu mbalimbali juu ya ile ndoto yako.
Ili ufikie Ubilionea unaanza na hatua moja anza leo kupiga hatua moja moja hadi ufikie kule unakotaka. Usikubali kabisa siku ipite ujafanya chochote juu ya Ndoto yako ni kupoteza fursa.

Kama tunavyojua fursa ya kwanza ni uhai tulionao leo hivyo usitumie vibaya leo siku zote unakuwaga na leo tu. Ukiweza kuipangilia leo vizuri itakufikisha kwenye ndoto yako.

Jipongeze

Kwenye kila hatua unayopiga jipongeze ili kujiongezea hamasa na wewe uweze kusonga mbele. Unaweza kujipa zawadi ndogo ndogo ambazo huwa unazipenda kila unapopiga hatua kuelekea kule unapotaka.

Iseme ndoto yako sehemu yeyote unapokuwa.

Kwanini uiseme kwa sababu una Imani na Imani ni kua na hakika juu ya mambo yasiyoonekana.
Hata Yusuf alianza kuwaambia ndugu zake kwamba anaona ndoto anaona akiwaongoza. Walimkemea lakini hakusita kuendelea kuwaambia.
Hii itakusaidia unapokamilisha iwe ushuhuuda kwamba huyu jamaa alituambiaga anakuja kuwa Rais, Bilionea, Mtu mkuu sana.

Kuwa na ndoto kubwa ni jambo la muhimu sana katika maisha. Mara nyingi, inasemekana kwamba ikiwa una ndoto ambazo hazikutoi usingizi, basi unaelekea katika mwelekeo sahihi. Mara nyingine, watu watakuita mchawi au Freemason wanapoona unafanikiwa. Lakini, kumbuka, maneno hayo hayana msingi kama yanasemwa wakati unapoanza tu kuota ndoto zako kubwa, kama vile kujenga ghorofa au kumiliki gari la kifahari kama BMW, wakati huna chochote.

Watu wanaokatisha tamaa mara nyingi ni wale wale ambao hawawezi kuona mbali kuliko hali yako ya sasa. Hawaelewi kwamba ndoto huenda zaidi ya hali ya sasa. Kama mtoa hamasa Norman Vincent Peale alivyosema, “Panda picha ya mafanikio ya kustaajabisha katika akili yako. Fikiria hili kwa nguvu. Kisha, fanya kazi kwa ujasiri kila siku kufanya picha hiyo kuwa uhalisia.”

Ni muhimu pia kutambua kwamba kuisema ndoto yako, kuiweka wazi mbele ya wengine na kujiamini, kunaweza kukujengea ujasiri. Hiyo ina maana ya kuendelea kutafakari kwa bidii jinsi ya kuifanya ndoto yako iwe kweli. Usemi unasema, “Ujumbe mzito huvunjika moyo pale unapotamkwa.” Hivyo, endelea kuongea kuhusu matarajio yako, mipango yako, na ndoto zako. Hii itakupa nguvu ya kuvumilia nyakati ngumu na kukusaidia kubaki thabiti katika njia yako.

Naamini una kila kitu kinachohitajika kuilinda ndoto yako. Itapasa uwe na nidhamu, uvumilivu, na azma thabiti. Kikubwa zaidi, uwe tayari kujifunza na kukua. Kila hatua unayopiga kuelekea katika ndoto yako, hata ikiwa ni ndogo, ni hatua muhimu.

Kumbuka kwamba hakuna jambo la maana ambalo hutokea usiku mmoja. Mafanikio ya kweli hujengwa kidogokidogo. Kwa hiyo, hata kama unakabiliwa na kejeli au shutuma, usiruhusu hiyo ikuvunje moyo. Kama alivyosema mwanasiasa na mwandishi wa Marekani Adlai Stevenson, “Ni jambo kubwa kuweza kukumbuka wakati umefanikiwa, kwamba kuna wakati pia uliwahi kushindwa, na kwa vipimo vilevile, ukatumia fursa hiyo kukua na kuboresha.”

Hivyo basi, lipokee wazo la mafanikio moyoni mwako, liweke hai katika mazungumzo yako na hatua zako, na kisha, lifanyie kazi kwa ajili ya kesho yenye matumaini. Jitahidi kwa kila njia kuona ndoto yako ikitimia. Jipe moyo na usisahau kusherehekea kila hatua unayopiga kwa mwelekeo chanya.

Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yake cheki kilichomkuta

Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yakeโ€ฆ.

Alikuwa anasubiri mjomba na mkewe walale tu halafu ananyata mdogo mdogo mpaka chumbani kwa binamu yake.

Siku moja umeme ulikuwa umekatika ikabidi aamue kuvua nguo kabisachumbani kwakeโ€ฆ.

Akanyata taratibua akafungua mlango akazama chumbani kwa mjomba ake bila kujua, ghafla umeme ukarudiโ€ฆ

MJOMBA; we mshenzi umefata nini chumbani kwangu tena uko uchi

JAMAA; nimekuja kukuaga kesho naondoka

MJOMBA; ndo uje uchi?

JAMAA; ndio kwasababu nimeshapaki kila kitu kwenye begi

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Magonjwa hatari 10 yanayotibika kwa kutumia mbegu za Maboga

Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma, mbegu za maboga ni tamu na zinaweza kutafunwa nyakati zozote na mahali popote hasa kwa wapenda kutafuna-tafuna kama mimi. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10 yafuatayo:

1. UGONJWA WA MOYO:

Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa mhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni mhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo. Mbegu hizi pia zina mafuta mengine mhimu zaidi kwa watu wenye ugonjwa wa moyo yenye OMEGA 3.

2. HUIMARISHA KINGA YA MWILI:

Mbegu za maboga zimebarikiwa kuwa na kiasi cha kutosha cha madini ya zinki (zinc). Kazi kubwa ya madini ya zink ni kuimarisha kinga ya mwili. Upungufu wa madini ya zink unaweza kupelekea matatizo kadhaa mwilini ikiwemo kuzaa watoto njiti, kuishiwa nguvu za kiume, matatizo ya homoni, chunusi nyingi mwilini, watoto kuwa na uwezo mdogo shuleni kimasomo na matatizo mengine kadhaa ya kimwili na kiakili.

3. HUONGEZA UWEZO WA MACHO KUONA

Mbegu za maboga zina Vitamini E, vitamini A, lutein, beta-carotene na zeaxanthin, vitu hivi vinavyopatikana katika mbegu za maboga ni mhimu kwa ajili ya nuru ya macho. Vitamini A na madini ya zinki ni mhimu kwa ajili ya uzalishaji wa โ€˜melaninโ€™ kimengโ€™enya mhimu ambacho hutengenezwa kwa asili na miili yetu kwa ajili ya ulinzi wa afya ya macho.

4. KINGA YA KISUKARI

Kisukari ni moja ya ugonjwa unaoendelea kwa kasi kuwasumbua watu wengi kila pembe ya dunia. Mbegu za maboga zina vitu vitatu mhimu zaidi ambavyo ni โ€˜Nicotinic acidโ€™, โ€˜Trigonellineโ€™ na โ€˜D-chiro-inositolโ€™ ambavyo husaidia kushusha damu sukari mwilini na kudhibiti kazi za insulini hivyo kuwa kinga na kuleta ahueni kubwa kwa watu wenye kisukari.

Kama unasumbuliwa na kisukari fanya mazoea ya kutafuna mbegu za maboga kila siku na unipe mrejesho hapa.

5. DAWA BORA YA USINGIZI

Mbegu hizi zimegundulika pia kuwa na kirutubisho kinachozalisha homoni za usingizi. Kwenye mbegu za maboga kuna vimengโ€™enya viwili mhimu zaidi ambavyo huhusika na usingizi na afya ya akili moja kwa moja navyo ni โ€˜L-tryptophanโ€™ na โ€˜tryptophanโ€™. Gramu 100 tu za mbegu za maboga zina kiasi cha kutosha cha โ€˜tryptophanโ€™ mpaka mg 576. Tryptophan ndiyo inahusika kuleta usingizi wenye utulivu pia huondoa msongo wa mawazo au stress mwilini. Kwa kuongezea mbegu za maboga zina kiasi kingi cha vitamini za kundi B. Muda mchache kabla ya kwenda kulala tafuna mbegu za maboga na utapata usingizi mtulivu kabisa mpaka asubuhi.

Kwahiyo kama una tatizo la kukosa usingizi jaribu kutumia mbegu za maboga na uniletee majibu hapa. Kumbuka kukosa usingizi mara nyingi huwa ni matokeo ya msongo wa mawazo na kama ulivyoona mbegu hizi zinaondoa pia stress! Kazi ni kwako ndugu.

6. DAWA BORA YA UVIMBE

Mbegu za maboga zinao uwezo mkubwa wa kuondoa sumu mwilini sambamba na uvimbe (inflammation). Kama ujuavyo sehemu kubwa ya vivimbe mwilini ni matokeo ya sumu kadhaa mwilini. Mbegu za maboga zitakuondolea uvimbe mwilini bila kukuachia madhara yoyote mabaya hapo baadaye. Kama unasumbuliwa na uvimbe popote jaribu kutumia mbegu za maboga na utuletee majibu. Mbegu za maboga pia ni dawa nzuri kwa aina nyingi za kansa mwilini.

7. HUONGEZA MAZIWA KWA MAMA ANAYENYONYESHA

Mbegu za maboga zina protini nyingi bora itokanayo na mimea isiyo na madhara kama ile ya kwenye wanyama. Pia zina OMEGA 3. Mama mjamzito hata unayenyonyesha tumia mbegu za maboga na utakuwa na uhakika wa kutoa maziwa ya kutosha kwa ajili ya mtoto.

8. DAWA NZURI KWA MATATIZO YA TEZI DUME

Wataalamu wengi wa lishe wanapendekeza mbegu za maboga zitumike kwa wanaume wa rika zote yaani vijana hadi wazee kwani zimethibitika kuwa msaada mkubwa kwa afya ya tezi dume. Tafiti nyingi zinasema mbegu za maboga zina kiasi kingi cha madini ya Zinki madini ambayo ni mhimu SANA kwa afya ya tezi dume na husaidia uponyaji wa tatizo la tezi dume moja kuwa kubwa kuliko nyingine tatizo lijukanalo kwa kitaalamu kama โ€˜benign prostatic hyperplasiaโ€™. Wanaume kazi ni kwenu.

9. ZINAONGEZA NGUVU ZA KIUME

Maajabu mengine ya mbegu za maboga ambayo ulikuwa huyajuwi bado.

Utaniuliza kivipi zinaondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume? Kwanza kabisa zinaondoa msongo wa mawazo/stress kitu ambacho ni namba 1 katika kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, lakini pia zinashusha lehemu (cholesterol), zinatibu kisukari, zinatibu tezi dume (matatizo kama ya ngiri nk), zinashusha kisukari, zina protini nyingi ya kutosha na yenye ubora na mbaya zaidi ni kuwa zina madini ya ZINKI madini mhimu kuliko kitu kingine chochote kwenye upande wa nguvu za kiume na kinga ya mwili. Bado huelewi? Zina madini ya chuma pia

Uzuri ni kuwa mbegu hizi hazina uchungu wowote, ni tamu kuzitafuna wakati wowote na mahali popote hata ukiwa ofisini unaweza kuwa nazo pembeni unatafuna huku unaendelea na kazi zako. Sambamba na hilo kama tulivyoona pale juu kwamba zinaongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha kwa upande wa wanaume zinaongeza pia uwingi wa mbegu za kiume (sperm count) ukitafuna mbegu za maboga siku mbili tu utaona ukimwaga bao linatoka la kutosha na zito kweli kweli basi ujuwe ni mbegu za maboga hizo.

10. ZINAONDOA PIA MSONGO WA MAWAZO (STRESS)

Msongo wa mawazo au stress kama mlivyozoea wengi ni tatizo linaloendelea kuwasumbua watu wengi miaka ya sasa. Mbaya zaidi wengi huwa hawaelewi nini madhara ya hizo stress wanazojipa. Yaani stress au msongo wa mawazo unaweza kukuletea magonjwa mengine mwilini zaidi ya 50, hivyo utaona ni jinsi gani ilivyo mhimu kwako kuweka chini stress zako na uendelee na maisha kwani kuendelea kuwa na stress ni hatari zaidi kwa afya yako.

Moja ya sababu kuu ya watu wengi kuwa na stress ni usawa usio sawa wa homoni zao (hormonal imbalance). Hivyo kama una tatizo la homoni kwenye mwili hebu weka mazoea ya kutafuna mbegu za maboga kila siku na hutakawia kuona tofauti. Mbegu za maboga zina kimengโ€™enya mhimu sana kwa kutuliza mawazo kiitwacho โ€˜tryptophanโ€™ na asidi amino zingine mhimu zinazohusika kutengenezwa kwa homoni nyingine ijulikanayo kama โ€˜serotoninโ€™. Kama ulikuwa hujuwi ni kuwa serotonin ni homoni inayohusika na kazi mhimu sana ya kurekebisha matendo ya kitabia na kutoa matokeo chanya kwa mambo yanayohusu usingizi, hali ya mawazo kwa ujumla na mambo yanayohusu njaa.

Mbegu za maboga ni msaada mkubwa kwa kina mama waliofikia ukomo wa siku zao na huondoa matatizo ya kiafya yatokanayo na kukoma kwa hedhi. Ni msaada kwa watu wenye saratani mbalimbali, huimarisha ukuaji na ustawi wa mifupa na meno, huondoa harufu mbaya ya kinywa na husaidia pia wenye tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu kila mara.

NAMNA NZURI YA KULA MBEGU ZA MABOGA:

Unaweza kula zikiwa kavu na ndiyo utapata faida nyingi zaidi ingawa mimi napenda kuzikaanga kidogo kama dakika 15 hivi na huwa nazichanganya na maji ya chumvi ya mawe ya baharini kidogo kwa mbali ili kupata radha.

Unahitaji ujazo wa kiganja kimoja cha mkono wako cha mbegu za maboga kwa siku ujazo wa kama nusu kikombe cha chai hivi kwa siku.

Alichofanya maasai baada ya kupanda Tax

Baada ya kupanda daladala aina ya DSM kutoka Mbagala chalambe mpaka Mwenge na kulipa sh 500.Masai akachukua tax wakati wa kurudi.walipofika sasa shughuli ilikuwa hivi.

Masai: we dureva? Naulisa Ng’ombe na mbusi ipi ngali?
Dereva: Ni ng’ombe ghali Masai.
Masai: kwanini Ng’ombe ngali?
Dereva: kwa sababu ni mkubwa zaidi ya mbuzi
Masai: umepata..na mbusi na kuku ipi ngali
Dereva: ni mbuzi kwa sababu nae ni mkubwa kuliko kuku.
Masai: Umepata..
Masai: sasa me nimekwenda kule mwenge kwa ngali kubwa nikalitoa sh. 500 hii yko ndogo unasema nikupe 40,000 wewe acha wizi.. Nitakupa 250 Tu..wee acha lbia moraniโ€ฆ!!!

Baada ya mwanamke kukataa kufungua mlango angalia kilichomkuta

MUME: Fungua mlango!

MKE: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.

MUME: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.

MKE. Kufa huna faida yoyote duniani!

MUMEย kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo chubwiiiiiii!

MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.

MKE: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.

MUME: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka usiku huu na khanga moja.

Hii ndiyo Ladha ya bia zote usiyoijua

Ladha ya bia ya 1 hadi ya 6..

Kwa wanywaji wazuri wa bia,

chupa ya kwanza ๐Ÿบ huwa haileti hisia yoyote. Mnywaji humaliza chupa hiyo bila kuona matokeo yoyote zaidi ya kupoza kooโ€ฆ Na mara nyingi huwa mkimya, pengine huwa anasoma gazeti lake au kwa siku hizi anawasiliana na ndugu na jamaa kupitia simu yake.

chupa ya pili ๐Ÿบ๐Ÿบ kimsingi ndipo mazungumzo ya awali na wanywaji jirani huanza na haya huwa mazungumzo ya busara, yakihusu muelekeo wa ligi mbalimbali, siasa, idadi za ajali na kadhalika na wakati huu hata takwimu hutolewa zilizo sahihiโ€ฆ.

Mtu anaweza kukutajia wachezaji wote wa ligi daraja la tatu la huko Ujerumani bila kukosea, hata idadi ya wachezaji wa Yanga bila kukosea.. Ila wakati huu kama unaanzisha mashindano ya kucheua ni wakati mzuri kwani bia ya pili huongeza hisia za kucheua.

Bia ya tatu ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ huanza kumfanya mnywaji aanze kusikia furaha na pia huu huwa wakati ambapo karanga na korosho huliwa sanaโ€ฆ. Pamoja na mazungumzo kuhusu mpira na siasa, ghafla mazungumzo kuhusu michepuko huanza kujitokezaโ€ฆ..

Bia ya nne ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ huanza kusababisha masikio yaanze kupoteza nguvu za kusikia kwani utaona mnywaji ghafla amepandisha sauti, na ukijumlisha na kuwa baa zetu huwa na muziki una kelele utadhani waliopo wote wana matatizo ya kusikiaโ€ฆ.. bia hii humsaidia kuongea kwa nguvu kushindana na kelele za muziki.

Bia ya tano ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ ni hatari kidogo kwani ukiinuka kwenda chooni mara nyingi unarudi hujafunga zipuโ€ฆโ€ฆna kipindi hiki ni kibaya kwa wanywaji wa kike maana unaweza kumkuta akienda chooni akijiangalia kwenye kioo anaanza kulia peke yake na kulalamika; โ€˜Mi sipendwi mpaka leo sijaolewaโ€™ au โ€˜ Mume wangu sijui yukoje hanijaliโ€™

Japokuwa lazima isemwe ukweli ukifikisha bia hii, maisha ni raha sana unaweza ukaanzisha shoo ya kukata mauno katikati ya baa na kudai wewe ni mkali kuliko Shilole.

Kuanzia bia ya sita ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ๐Ÿบ na kuendelea, chochote utakachosema au kufanya ni wazi kesho yake asubuhi utajilaumu sana. โ€ฆโ€ฆ. โ€ฆKuna watu husema ukilewa ndipo unakuwa mkweli, hivyo basi wakati huu hata bosi wako akitokeza unamueleza ukweli jinsi alivyo fala na hajui kuendesha kampuni.

Au unasema ukweli jinsi unavyompenda mke wa jirani yako ambaye mmekaa mnakunywa naye. Kimsingi uwezekano wa kutapika pia upo karibu na kama umekaa na mchumba wako huu ni muda ambao pia uchumba unaweza kuvunjikaโ€ฆโ€ฆ.

Huyu jamaa amekomeshwa, majambazi ni shida!

CHEKA KIDOGO
Majambaz waliliteka gar moja lililokua limeshehen abiria
Baada ya abiria kusachiwa na majambaz hao na kukutwa hawana pesa, majambaz wakasema kila m2 atapigwa viboko (bakora) kutokana na namba ya shati alilovaa
Aliyekua hana namba atasalimika
Kaz ikaanza, jamaa alievaa jez ya ROONEY wa Man U akapigwa fimbo 10, mwengine alievaa nguo ya 50cent akapigwa 50, n.k, sasa kwa pemben kulikua na jamaa analia sn yaani kila akijiangalia, kumbe alikua amevaa fulana limeandikwa LOWASA 2015 duuuh! Unajua kilichotokea ngoja niweke cm chaji kwanza.

Padri Akimbia wakati wa kuungamisha, chanzo ni hiki

Padri alikuwa amekaa katika confession booth kanisani
peke yake.
Mara kukaingia jamaa mmoja akapiga magoti upande wa
pili, akafanya ishara ya msalaba kisha akaanza kuungama
{confess}
“Padri nimekuja kuungama dhambi zangu, leo nimefanya
dhambi kubwa sana.”
Padri, “Endeleaโ€ฆ”

“Bosi wangu aliniita nyumbani kwake, akaniambia
amegundua nimeiba shilingi millioni 100 kazini. Akasema
nisipozitoa atanipeleka polisi, sa kwa ukweli mi naogopa
kufungwa.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu,nikatoa bastola nikamuuaโ€ฆ.. Yesu atanisamehe?”

Padri: “Utasamehewa.”
“Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango
unafunguliwa kutazama, Loh! Mke wa bosi, alipoona
kilichotokea akasema anapiga polisi simu.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuua na yeye piaโ€ฆ Yesu atanisamehe hilo?”
Padri: “Utasamehewa.”

Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke, lakini mlinzi
akakataa kunifungulia, ati amesikia mlio wa
bastola. Nikaona ataniletea kizuizi huyu.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuuaโ€ฆ.. Yesu atanisamehe?”
Padri:”Utasamehewa.”

“Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda
nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi
akabisha hodi, nikawaza mambo gani tena, akasema alirudi
nyumbani na kukuta yaliyotokea akanionesha diary ya
babake, inayoonesha nilikuwa na appointment naye
wakati nilipomuua. Nikamuuliza nani mwingine anayejua?
Akasema ameanzia kwangu kisha anaenda polisi.

Nikatazama huku na huku nikakuta tuko wawili peke
yetu, nikamuuaโ€ฆ.. Yesu atanisamehe na hilo?”

Kimyaaโ€ฆ.
“Padri yesu atanisamehe?”
kimyaโ€ฆ.

Jamaa akatazama kwenye confession booth padri
hayupo, lakini kwenye kona moja akaona kabati la nguo
za mapadri linatikisika. Kufungua akaona padri kajificha ndani anatetemeka huku akitokwa na jasho.

Jamaa, “Sasa baba mbona umekimbia?”
Padri kwa taabu akajibu, “Nilitazama huku na huku
nikagundua tuko wawili peke yetuโ€ฆโ€ฆ.”

Je, Wewe unayesoma huu ujumbe una ndoto?

KILA mtu duniani ana ndoto ingawa haijalishi ni ndoto gani uliyonayo.
Ndoto uliyonayo ina thamani kubwa kuliko fedha wala kitu chochote kile. Ndoto uliyonayo ina nguvu kubwa ya kubadilisha maisha yako na kukufikisha sehemu ambayo ulitaka ufike ama zaidi ya pale ulipotarajia kufika.

Ndoto yako inaweza kukupeleka sehemu mbalimbali duniani ukazunguka kufanya mambo yako si kwa sababu una fedha sana, bali ni kwa sababu una ndoto. Ni vyema utambue nguvu ya ndoto uliyonayo ni kubwa kuliko fedha.

Ndoto inaweza kuzaa fedha kwa maana matunda yake yanaweza kuwa fedha, lakini katu fedha haiwezi kuzaa ndoto. Kwa hiyo bais, ndoto ni kubwa kuliko fedha.

Mtu mmoja aliwahi kusema kuwa, mtu maskini kuliko wote duniani ni yule asiyekuwa na ndoto!

Hivyo utakubaliana naye kuwa kila mwenye ndoto ni tajiri na si maskini, maana ana kitu cha thamani, cha pekee na cha tofauti ambacho hakuna mwenye nacho isipokua wewe mwenyewe.

Tatizo kubwa ni kwamba, watu wengi wameua ndoto zao kwa kisingizio cha kukosa fedha lakini wanashindwa kutambua kwamba hakuna fedha inayozidi ndoto isipokuwa ndoto inazidi fedha.

Tatizo lingine ni kwamba, watu wengi hawajui kuwa ndoto zao zina nguvu kubwa kufanikisha maisha yao kijamii, kiuchumi, kisiasa na kila nyanja.

Ndani ya ndoto zako kuna kila kitu unachokitaka ama unachokihitaji โ€“ iwe fedha, utajiri, umaarufu, familia nzuri, mume mzuri, mke mzuri, watoto wazuri, kazi nzuri, afya nzuri โ€“ hivyo ukiacha kutafuta fedha ukatafuta kutimiza ndoto zako utapata kila kitu ikiwemo utoshelevu na amani ya moyo.

Lakini tatizo lipo kwenye kufanya ndoto zako zitimie na zikuzalie mafanikio. Haijalishi una ndoto kubwa kiasi gani, kama hutaitimiza ikaja kwenye uhalisia tambua kwamba utakufa maskini ukiwa na utajiri wa ndoto, jambo ambalo linaumiza na linatesa maisha ya watu wengi wanaoishi maisha ya chini tofauti na walivyopaswa wawe.

Ndoto yako ndiyo imebeba kusudi la maisha yako. Kama hutaishi katika ndoto yako maana yake utakuwa hujaishi maisha yako ambayo kwa kiasi kikubwa yapo kwenye ndoto zako.

Mtu mmoja aliwahi kusema kuwa, watu wengi duniani hawaishi, bali wapo tu. Kuna tofauti kati ya kuishi na kuwepo. Kuishi ni kutimiza ndoto zako na ndani ya kusudi la maisha yako, lakini kama hutimizi ndoto hizo uko nje ya kusudi la maisha yako. Wewe utakuwa hauishi bali upo upo tu.

Anaamka asubuhi kwa sababu watu wanaamka. Ukimuuliza kwanini umeamka anasema ni kwa sababu watu wameamka! Hana sababu za msingi. Kataa kuishi bila agenda, bila kuwa na ndoto ambayo kila siku unapiga hatua kuifikia ama uko ndani yake sasa katika kuitimiza na kuifanikisha kwa kiwango cha juu.

Kila kitu kipo kwenye ndoto zako, tafuta kutimiza ndoto zako kuliko kutafuta fedha kwa sababu fedha ni moja kati ya bidhaa iliyomo ndani ya ndoto zako.

Sisemi watu wasitafute fedha, la hasha. Wazitafute, tena kwa bidi, ila wasisahau kutafuta kutimiza ndoto zao na kutumia fedha kama moja kati ya nyenzo za kuwawezesha kutimiza ndoto zao.

Ukweli ni kwamba, fedha daima huwa hazitoshi, hata kama ni nyingi kiasi gani. Kama unabisha waulize matajiri kama wamewahi kuridhika. Lakini katika kutimiza ndoto zako kuna utoshelevu kiasi na kuridhika kiasi fulani (satisfaction) hata kama si kwa asilimia 100.

Mwandishi mashuhuri wa vitabu, Myles Munroe, aliwahi kusema kuwa โ€œWatu wenye kusumbuliwa na msongo mkubwa wa mawazo ni wale ambao ndoto zao hazijatokea kwenye uhalisia, zinawasumbua.โ€

Inawezekana unasumbuka sana kwenye maisha yako kwa sababu hujatimiza ndoto zako, maana ndoto huwa haimwachi mtu akatulia, inampa mahangaiko, mfadhaiko wa kutaifuta.

Kila mtu anapaswa azae, ndoto yako izae, uwezo ulionao uzae. Unaweza kukuzalia mafanikio makubwa, hivyo usikubali kufa na kitu cha thamani kilichoko ndani yako.

Hakuna ndoto kubwa wala ndogo. Fikiria mtu aliyegundua lipstick, leo hii wanawake dunia nzima wanapaka lipstick, si jambo dogo tena.

Hukuja duniani kuwa mtu wa kuhangaikia fedha, inatakiwa fedha ikuhangaikie wewe, ikupende na ikutamani na si wewe utamani fedha.

Tengeneza miundombinu ya fedha na hiyo miundombinu iko kwenye ndoto zako, maono yako, kipaji

Faida 13 za kunywa juisi ya miwa

Unapopita maeneo mengi ya mijini na pembezoni wa miji utakutana na wafanyabiashara wa miwa wanaouza miwa na juisi yake. Wengi hununua juisi ya miwa kwa kuwa hufurahia utamu wake. Lakini umeshajiuliza juisi miwa ina faida gani kiafya?

Kuna faida nyingi za juisi ya miwa. Baadhi ya faida hizo ni kama zifuatazo;
1. Juisi ya miwa ina uwezo mkubwa wa kuipatia miili nguvu kwa haraka na kukata kiu ya maji. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari โ€œsucroseโ€ ambayo kazi yake kuu ni kutengeneza nguvu mwilini. Kwa hiyo wakati mwingine ukiwa na uchovu, badala ya kunywa vinywaji vya viwandani tafuta juisi ya miwa.

2. Ingawa juisi ya miwa ina utamu lakini inafaa sana kwa watu wenye kisukari. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari halisi ambayo ina uwezo mdogo wa kuzidisha kiwango cha sukari mwilini au kitaalamu inaitwa โ€œLow Glycemic Indexโ€. Kutokana na hilo juisi ya miwa inashauriwa kutumiwa kama mbadala wa vinywaji vingine vya viwandani. Ni muhimu pia kwa watu wenye kisukari kutumia juisi hii kwa kiasi kidogo au kulingana na ushauri wa Daktari.

3. Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa cha madini ya calcium, magnesium, potassium, chuma na manganese. Madini haya yana uasili wa ualkali ambao husaidia kupunguza uwezekano wa kupata kansa kama vile kansa ya Tezi dume โ€œProstate cancerโ€ na kansa ya maziwa โ€œBreast Canserโ€.

4. Juisi ya miwa inasaidia kuongeza kiwango cha protein mwilini na ku-imarisha ufanyaji kazi wa figo.

5. Juisi ya miwa iliyochanganywa na maji ya Nazi husaidia kupunguza maumivu hasa yanayosababishwa na maambukizi ya ngono โ€œSTDsโ€ na kidney stones.

6. Juisi ya miwa husaidia kulinda maini yasipate maambukizi. Hii ndo maana Madaktari hushauri matumizi ya juisi ya miwa kwa watu wenye ugonjwa wa Homa ya Manjano.

7. Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa cha madini ya potassium ambayo husaidia kuimarisha mmengโ€™enyo wa chakula.

8. Husaidia kuzuia maambukizi katika tumbo na utumbo.

9. Vilevile husaidia katika kutibu matatizo ya choo kigumu au kitaalamu inaitwa โ€œconstipationโ€.

10. Uchunguzi unaonyesha juisi ya miwa husaidia kuzuia meno kuoza na matatizo ya kupumua kutokana na kuwa na kiasi kikubwa cha madini. Kwa hiyo kama unafikiria kwenda kwa daktari kungโ€™arisha meno yako, kunywa juisi ya miwa mara kwa mara.

11. Juisi ya miwa husaidia katika kupambana na mabaka mabaka na kungโ€™arisha ngozi.

12. Juisi ya miwa huweza kutumika kama โ€ face mask na scrubโ€ kwa kuipaka kwenye ngozi na hivyo kusaidia katika kuingโ€™arisha na kuiimarisha uso.

13. Juisi ya miwa ina faida nyingi mwilini, ni muhimu kuhakikisha usafi katika utengenezaji wake.

Kumbuka: Juisi ya miwa isiyokuwa salama inaweza ikawa ni chanzo kikubwa cha magonjwa ya tumbo na kuhara.

Kuwa na kawaida ya kujiwekea Akiba ni njia na Siri ya kuwa tajiri

Watu wengi wanajiuliza, โ€œSiri ya utajiri ni nini?โ€ Je ni mbinu gani zinaweza kumsaidia mtu kupata utajiri? Siri kubwa ya utajiri ni kujifunza elimu ya namna ya kutafuta mtaji, kuwekeza kwa busara kwa namna ambayo daima panakuwa na ziada na faida.

Kuwa na lengo la kifedha, kuweka akiba, na kutumia fedha kwa hekima ni muhimu sana katika safari ya kuelekea utajirini. Kuweka malengo kunamaanisha kuwa na mpango madhubuti wa kifedha unaolenga katika kupata matokeo mazuri ya uwekezaji na matumizi ya fedha. Watu wenye mafanikio katika eneo la utajiri mara nyingi hutumia mipango ya muda mfupi, kati, na muda mrefu kuhakikisha kuwa wanafikia malengo yao.

Aidha, kuweka akiba ni nguzo muhimu. Hii inamaanisha kujinyima baadhi ya matumizi yasiyo ya msingi na kuhakikisha kuwa unaweka kando sehemu ya mapato yako kwa ajali ya siku zijazo. Akiba hii inaweza kutumika kama mtaji wa kuanzisha biashara au kuwekeza katika fursa zenye faida kubwa.

Kuwekeza ni hatua inayofuata baada ya kuwa na akiba ya kutosha. Hapa, elimu juu ya masoko ya fedha, biashara, na uwekezaji katika rasilimali kama hisa, mali isiyohamishika, na biashara huja kuchukua sehemu kubwa. Ni muhimu kujifunza na kuelewa ni wapi na lini kuwekeza. Kutafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa fedha kunaweza kusaidia kuepuka makosa na kupata mwelekeo sahihi.

Kwa kutumia mbinu hizi โ€“ kuweka malengo, kuweka akiba, na kuwekeza kwa hekima โ€“ mtu anaweza kujenga msingi imara wa kuelekea utajiri. Ni safari inayohitaji uvumilivu, nidhamu, na uelewa mpana wa maswala ya kifedha, lakini inawezekana kwa yule aliye tayari kujifunza na kuchukua hatua.

Kwa bahati mbaya sana, elimu hii haifundishwi darasani ila wafanyabiashara wachache na kila anayefanikiwa kujifunza siri hii huwa tajiri na huendelea kuificha.
Kwa bahati nzuri, katika utafiti wagu nimeweza kuigundua siri ya utajiri.Kwa kuwa ninapenda wasomaji wangu waweze kufanikiwa na wapate manufaa kwa kununua kitabu hiki nimeamua kuiweka siri hii wazi:โ€”

Siri ya kwanza ya kuelekea ukwasi ni kubuni mradi unaojipa, yaani unaoweza kuitoa ziada na faida.

Siri ya pili ya kuelekea kwenye utajiri ni kujifunza na kujenga tabia ya kuweka akiba-

Siri ya tatu ni kuwekeza fedha hizo za akiba katika vitega uchumi ambavyo vinazalisha faida endelevu.

Siri ya nne ni kujifunza namna ya kufanya biashara na kuanzisha biasharayako ili iwe indelevu.

Kuna njia mbili za namna ya kupata utajiri zenye uhakika.

Njia ya kwanza ni njia ndefu ambapo wataalamu na watafiti wa masuala ya fedha wameigundua njia hii ni rahisi kuifuata kwa sababu haihitaji uwe na kipato kikubwa, wanashauri kwamba ujenge tabia ya kuweka akiba, anza kuweka akiba ya T.shs 1,000 kila siku sawasawana TShs 30,000 kwa mwezi, matokeo yake ni kwamba kama utaweka akiba yako kwa kipindi cha miaka 65 bila riba yoyote utakuwa na akiba TSshs 23,725,000 (Milioni Ishirini na Tatu Mia Saba Ishirini na Tano Elfu). Kama utawekeza fedha hiyo na kupata riba ya asilimia 10% kwa kila mwaka itazaa na kukuletea TShs 2,750,000,000 (Bilioni Mbili na Milioni Mia Saba Hamsini). Hesabu hii inaweza ikakutisha na usiamini macho yako lakini hiyo ni siri ya nguvu ya hesabu na riba kama alivyozielezea mwanafizikia Enstein kwamba katika dunia hii hakuna kitu chenye nguvu kama hesabu za riba. Pengine njia hii inaweza kuwa ni ndefu sana na ya kukatisha tamaa. Wengi wetu hatuwezi kusubiri muda mrefu. Hivyo tungependa kuwa na mafanikio ya kiuchumi kwa haraka. Lakini nasisitiza kama kipato chako ni kidogo anza leo kuweka akiba ya TShs 1,000 kwa siku.Dundulizo la akiba hii hukutiririshia utajiri bila wewe kukusudia kwani utaweza kukidhi hitajiko la ghafla kama kuugua safari ya dharura gharama za likizo na hata kutumia mbinu hii kama mpango wa elimu kwa watoto wako iwapo utawaanzishia hivi mara tu kila mmojawapo anapozaliwa au unaweza kuutumia kama upanga wa siku zijazo kwa mirathi ukianza hivyo leo kwa kupangilia namna hiyo kwa kila kusudio lako la baadaye.

Tuangalie njia ya pili.- Njia ya pili ya mkato ni kuongeza kiwango cha kuweka akiba kama wewe ni mtu mwenye shughuli za kuzalisha ziada. Kipato chako kinaweza kuwa kinaongezeka kila mara. Badala ya kuweka akiba ya TShs 1,000 kwa siku jiwekee malengo ya kuweka akiba ya TShs 10,000. Anza kwa kutenga asilimia10% ya mapato yako hadi utakapofikia lengo la TShs 10,000 au zaidi kwa siku. Badala ya lengo lako kutimia kwa miaka sitini na tano (65) litatimia haraka zaidi. Kwa mfano ukiweka akiba ya TShs 10,000 kwa siku kwa muda wa miaka sita na miezi sita bila riba yoyote utapataTShs. 23,725,000. Ukiwekeza fedha hiyo na kupata riba ya asilimia 10% kwa miaka sita na miezi sita utapata TShs. 33,917,505.78. Kama fedha hiyo utaendelea kuweka akiba kwa riba hiyohiyo hadi kufikia muda wa miaka kumi utapata TShs. 63,112,201.43.Kwa kuwa kitu cha muhimu hapa ni kuweka akiba na kuwekeza akiba hiyo katika kitegauchumi chenye kutoa faida kubwa, utajiuliza jee uwekeze kwenye kitega uchumi chenye kutoa faida kiasi gani? Wataalamu wa mambo ya fedha wanashauri kuwa uwekeze fedha yako kwenye kitegauchumi chenye kutoa faida ya angalau asilimia 10% Kwa mfano unaweza kuwekeza kwenye Akaunti ya TAJIRIKA ya Standard Chatered Bankโ€ inatoa riba ya asilimia kumi 10% pia unaweza kuwekeza kwa kununua hisa katika soko la hisa na mitaji.Kwa wastani wa watafiti wa masuala ya fedha viwango vya mapato yatokanayo na hisa kwa gawio pamoja na kukua kwamtaji ni zaidi ya asilimia 11% ambayo ni makubwa kwa kiwango cha kawaida chaasilimia kumi (10%).

Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza

Zuzu: Mambo Anna!
Anna: Poa!
Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyesheโ€ฆ
Anna: Kitu gan?
Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda)
Anna: Haya nionyesheโ€ฆ

Zuzu: Funga mlango na madirisha kwanza (akafunga)
Anna: Haya nionyeshe sasa!..
Zuzu: Zima taa kwanza (akazima)
Anna: Mhmโ€ฆnionyeshe sasa!
Zuzu: Haya njoo hapa kitandaniโ€ฆ
Anna: Ok, nionyeshe!
Zuzu: Ona nimenunua saa ambayo inawaka yenyewe gizaniโ€ฆ Acha mawazo mabaya ww???

Matumizi ya maji kutibu shinikizo la chini la damu

Matumizi ya maji ya kunywa ni moja ya dawa rahisi kabisa ya shinikizo la chini la damu.

Hii ni kwa sababu Maji ni mhimu kwa kila ogani ndani ya mwili iweze kufanya kazi zake sawa.

Kwa hiyo sababu kuu ya mtu kuwa na shinikizo la chini au hata la juu ni matokeo ya mishipa ya damu kutokuwa na vimiminika vya kutosha.

Mishipa ya damu imeundwa kwa maji maji ya damu (serum) na seli za damu.

Maji yanapopungua kwenye mwili hata vipenyo vya mishipa yako navyo hupungua ukubwa wake jambo linaloleta kushuka kwa shinikizo la damu.

Matatizo yote haya ni matokeo ya kutokunywa maji ya kutosha kila siku.

Kwa sababu hii, ili kupandisha juu shinikizo la damu unahitaji kunywa zaidi maji sambamba na juisi nyingine za matunda au za mboga mboga kila siku.

Hii inasaidia kuongeza vimiminika katika mishipa ya damu.

Angalia huyu mvulana anachomwambia huyu daktari baada ya rafiki yake wa kike kupata ujauzito

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

MVULANA:ย Daktari, rafiki yangu wa kike ni mjamzito, lakini mara zote nimekua nikitumia kinga. Inawezekanaje hii?

DAKTARI:ย Ngoja nikusimulie hadithi. Kulikua na Muindaji ambaye alikua anabeba bunduki kila aendako. Siku moja, alichukua mwamvuli badala ya bunduki na akaenda nayo. Ghafla akatokea Simba mbele yake. Ili amtishie Simba, muindaji akatumia mwamvuli na kummiminia risasi Simba. Simba akafa palepale!
MVULANA:ย Sio kweli!! Lazima kulikua na mtu mwengine pembeni aliyempiga risasi Simba.

DAKTARI:ย Nashukuru umeelewa somo!!๐Ÿ˜‚

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ

MasterKutu 72WP: Dawa Maalumu ya KUTIBU na KUKINGA kutu, kuvu na ukungu kwenye nyanya, hoho, tikiti, viazi, nk

Master Kutu ni dawa ya kutibu na kukinga magonjwa ya ukungu, kuvu na Kutu katika mazao mbalimbali kama vile nyanya, vitunguu, tikiti, viazi, maharage, mboga mboga nakadhalika Master Kutu inatibu aina zote za ukungu na kuvu bila kuchagua. Master Kutu ina viambato viwili vikuu, Mancozeb and Cymoxanil, (Mancozeb 640g/kg + Cymoxanil 80g/kg).

  • Mancozeb inatumika kudhibiti Kutu na kuvu kwenye mbogamboga, matunda na nafaka. Inadhibiti โ€œpotato blight, leaf spot, scab and rustโ€.
  • Cymoxanil inazuia ni kiua kuvu kinachonyunyizwa kwenye majani ambacho kinatibu na kukinga kuvu kwenye nyanya, viazi mviringo, tango na tikiti nakadhalika.

Bidhaa hii inaletwa Kwako na Kampuni ya BareFoot International Limited. Wauzaji na wasambazaji wa bidhaa Bora za Kilimo Tanzania.

Mawasiliano

Simu:

+255 756 914 936

โ€”

WhatsApp:

+255 756 914 936

โ€”

Email:

info@bfi.co.tz

โ€”

NB: Tunapatikana Mikoa Yote Tanzania

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About