Meseji ya kumsihi mpenzi wako azidi kukupenda
Natambua ugumu wa mapenzi
Mengi ni matamu, mengine ni machachu
Ila nakusihi usikate tamaa ya kunipenda kimoyo
Natambua ugumu wa mapenzi
Mengi ni matamu, mengine ni machachu
Ila nakusihi usikate tamaa ya kunipenda kimoyo
Nakupenda sana mwandani wangu ndiyo maana moyo wangu
hupatwa kidonda ninaokuona na mwingine hasa anapokuwa hana
sifa, nahisi kama anakutumia wewe kama mdori wake wa
kumfurahisha. Uwe makini ua la moyo wangu.
Leo ni siku ya furaha kwangu na kwa wakwe zangu,
unajua ni kwa nini? Ni siku waliyokuleta kwenye hii dunia,
happy birthday mpenzi!
Penzi, maisha yangu yote nimesoma juu ya neno hili,
nimeota juu yake, nimelilia, nimelihitaji. Sasa pamoja
nawe nimelipata.
mapenzi ni upepo,mimi sivumi na kupotea,mapenzi ni mahaba
sili nikamaliza,mapenzi ni raha kamwe cwez
kuipeza,nakupenda wewe pekee
natamani usaini moyoni mwang,ikiwezekana pia upige muhuri moyoni mwangu wajue nan mmiliki wa huo moyo wenye shibe upendo kwaajili yako mpenzi
Bongo zenye fikra kali huwa na mawazo, suluhu na sababu;
ubongo wa kisayansi huwa na kanuni, nadharia na takwimu;
wangu una wewe tu!
Ukilala Lala Salama Kumbatia mwili wangu Kama ukinikumbuka Sana Nipigie Kupitia Sim Yangu Matatizo Chuki Lawama Vumilia Mpenzi Wangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Hata kama nitajidanganya kwamba sikupendi, moyo wangu umeganda kwako na hakuna dalili za kukuacha, wewe ni wangu peke yako dear…
Lazima utakuwa mwizi sababu umeiba moyo wangu, umechoka
sababu unakimbia mara zote akilini mwangu, na labda mimi
sina shabaha sababu mara zote nikikulenga nakukosa.
Niliumbwa kwa ajili yako, mbele yako nitakushika mkono, nikuonyesha sayari yangu, pendo langu la undani, na NITAKUHESHIMU milele mpenzi wangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ingawa mwaka umekwisha, mawazo yangu katu sitobadilisha, amini ni wewe pekee unayenipagawisha, hakika kwa penzi lako kiu yangu katu haitakwisha!
Kuna bahari kati yetu. Misitu na milima inatutenganisha,
mimi si ‘Supamani’ lakini nipe sekunde moja nitavuka nchi
nyingi kukutumia mapenzi yangu. Umeipata hiyo? Pokea mapenzi yangu japo uko mbali.
upendo wa moyoni ndiyo dhati niliyoamini amini kwa haya
nisemayo nakupenda wewe ndiyo kaburi nitakalozikwa nalo
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka.
Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika.
Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka.
Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Matamu na maji yake hukata kiu haraka.
Weupe watui lake lina ladha ukipika.
Kupaka mafuta yake mwili hulainika.
Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika.
Hata na upepo wake uvumapo utacheka.
Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Maji hunitosha nisikiapo kiu, chakula hinitosha nisikiapo njaa, lakini wewe hunifaa kwa kila kitu!
Mpenzi kila tunapokuwa chumbani huwa napenda kuwa mbunifu, huwa najitahidi kuepuka udhaifu, ili mapenzi yangu yasikukifu, ENDELEA KUFURAHIA MAPENZI YANGU. Mchana mwema
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Wewe ni wapekee ninaekupenda, sifikirii kukusaliti na wala
sina wazo la kukutenda, nakuomba
tuendelee kupendana siku zote habbity wangu
Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje. Hodiiiiii, Hodiiiii, Tunaomba tufungulie Mlango,, sisi tunaitwa FURAHA, AMANI na UPENDO. Tumebeba HEKIMA, BUSARA na MAFANIKIO. Tulikuwa wengi HURUMA na UPOLE wanakuja nyuma. CHUKI na WIVU hawana nauli. TABU ni mahututi. SHIDA yuko jela. MATATIZO amepigwa shoti ya umeme. MIKOSI amefariki njiani. LAANA ameliwa na mamba. UVIVU ameungua na maji ya moto hajiwezi. Tutakuwa nawe daima maana tumefika kwa NEEMA . Mungu akulinde na mabaya yote katika dunia hii. ucku mwema.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
mapenzi ni utoto,deka ulie nitakubembeleza,mapenzi ni
zawadi tabasamu nibusu niambie kiasi gani unanpenda,naweza
kusema asilimia kubwa jina lako limezunguka kuta wa moyo
wangu.kamwe jina lako haliwezi kufutika.nakupenda sana.
Recent Comments