SMS nzuri ya kumtumia umpendaye kumwambia unavyompenda na kumridhia
Siku zote kwangu ni sherehe ni wewe unishereheshaye,ukweli
usio na kejeli mapenzi yako yanatii kiu yangu,moyoni
mwangu nimeridhia… .nakupenda daima mpenzi!
Siku zote kwangu ni sherehe ni wewe unishereheshaye,ukweli
usio na kejeli mapenzi yako yanatii kiu yangu,moyoni
mwangu nimeridhia… .nakupenda daima mpenzi!
Usikimbie nyuki ukakosa asali, utamu wa samaki ni kula na wali, usizidishe siki akawa mkali. Ni mimi niliye na dhiki nakujulia tu hali.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Mapenzi ni upepo,mimi sivumi na kupotea,mapenzi ni mahaba
sili nikamaliza,nikimaliza nitakula nini kesho?nakuahidi
kukupenda leo hata kesho ukiwepo na hata usipokuwepo.
Je unakubali au unakataa kwa mujibu wa sheria ya mahakama
ya mapenzi kifungu cha mahaba unahukumiwa kuwa na mimi
milele,unaweza kukata rufaa kama hujatendewa haki.sawa?
Furaha yangu kubwa ni kuliona tabasamu lako, kujua uko na
furaha, na kuhisi upendo wako. Najua kuwa maisha mara
nyingine huwa ni makatili, na hiyo ni sababu niko hapa
kukuonyesha kuwa maisha yanaweza kuwa mazuri kama kuna mtu
anayekujali.
tazama, nimezama
ndani ya bahari
la penzi lako
siwezi
kusonga mbele
kurudi nyuma
sijielewi
haya mapenzi ya fujo hayafai
kama wanipenda
jaribu kunipa raha
Ni ngumu kwa watu wawili kupendana wanapoishi Dunia
tofauti, lakini Dunia hizo zikutanapo na kuwa kitu kimoja,
hiyo ndiyo maana ya kuitwa wewe na mimi.
maumivu ya kulipoteza penzi lako ni kubwa, lakini ni
makubwa zaidi baada ya kugundua haukuwa yule nileyedhani.
inaniuma sana
nikipoteza kitu cha thamani nitauzunika nitasahau ila
nikikupoteza wewe ni pengo lisilozibika kamwe.
Mapenzi ni matamu napia yana raha, wewe hauni ishi hamu, siku zote wanipa raha, wewe kwangu ni mtu muhimu, unaeng’aa moyoni mwangu kama nyota ya jaha. “NAKUOMBA USINIACHE MPENZI WANGU”
Mawingu yametanda napanda kwenye kitanda,
macho nayaangaza,
taratibu navuta shuka na kujitanda,
mishumaa pembezoni inaniangaza,
mziki laini wanibembeleza kitu pekee nilichokikosa
ni joto lako na vijimambo vyako kunako kitanda!
Simu huboa wakati mwingine, kwani ni lazima ufungue meseji
na kuzisoma, kuichaji simu kila mara, lakini usichoke
kwani ndiyo inayotuwezesha tuwasiliane
Mapenzi ni nini? Wale wasiopenda huita majukumu, wale
wanaoyachezea huita mchezo, wale wasiokuwa nayo huita
ndoto, na wale wanaoelewa huyaita mwisho wa safari, na
mimi, mwisho wangu ni wewe.
Kuna miezi 12 katika mwaka…siku 30 katika mwezi…siku 7
katika wiki, masaa 24 katika siku…dakika 60 katika saa……
lakini wewe ni mmoja tu maishani mwangu.
Hakika wewe ndiye wangu mahabuba unayejua kunipa huba,
napenda unavyoniganda mithili ya ruba, nahahidi kukupa
mahaba yanayozidi shaba. Nakupenda.
Ningependa siku moja utamani sana kuwa na mimi, na
uhangaike sana kunitafuta, ili ujue ni kwa kiasi
ninavyotamani kuwa nawe sasa.
Natamani ningekuwa chozi jichoni mwako ambapo ningetelemka
na kuishia midomoni mwako, lakini kamwe sitamani uwe chozi
jichoni mwangu nitakupoteza kila muda niliapo.
Ucku ulalapo jua kuna m2 akupendaye,mchana uwajibikapo
tambua yupo anayekuwaza ,jioni uwapo mazoezini jua yupo
anayekuonea wivu,hata uwapo kwenye kumbi za burudani
tambua mwenzio nakulilia,usitoe penzi kangu akilini hata
km upo mbali nami!moyoni mwangu hutafutika milele!
kila niamkapo mawazo yangu huwa kwako na upepo uvumapo
huhitaji uwepo wako na hasa nikukumbukapo kumbato
lako,nakupenda mpenzi
Najua kuna vishawishi vingi sana uko ulipo, lakini nikiwa
moyoni mwako, siku hii itakuwa nzuri zaidi kwetu,
tupendane daima lahazizi…
Recent Comments