Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Jinsi ya kutengeneza Cookies Za Tende Na Tangawizi
MAHITAJI
Unga vikombe vikombe 4
Baking soda 1 kijiko cha chai mfuto
Siagi 400 gms
Sukari ½ kikombe
Tende chambua ukatekate ifikie ¾ kikombe
Tangawizi ya unga vijiko 2 vya chai
Vanilla 1 kijiko cha chai
Yai 1
Maziwa mazito vijiko 2 vya kulia.
MAANDALIZI
Changanya siagi na sukari katika mashine usage mpaka iwe laini nyororo.
Tia yai uchanganye vizuri
Tia tende na vanilla, tangawizi uchanganye vizuri.
changanya unga na baking soda kisha, mimina kidogo kidogo huku unachanganya kwa kijiko cha ubao (mwiko).
Unga ukiwa mzito ongeza vijiko 2 vya maziwa. Fanya viduara upange katika treya uliyopakaza siagi kisha uchome (bake) katika over moto mdogo wa kiasi dakika 15 vigeuke rangi viwive.
Epua vikiwa tayari
Mapishi ya Samaki wa kupaka
Mahitaji
Samaki (Tilapia 2)
Nyanya ya kopo (Tomato tin 1)
Kitunguu (Onion 1)
Tangawizi (ginger kiasi)
Kitunguu swaum (garlic clove )
Mafuta (Vegetable oil)
Pilipili (scotch bonnet pepper 1)
Tui la nazi zito (coconut milk 2 vikombe vya chai)
Curry powder 1/2 cha kijiko cha chai
Binzari nyembamba ya unga (ground cumin 1/2 kijiko cha chai
Binzari manjano (turmaric 1/2 kijiko cha chai
Chumvi (salt)
Limao (lemon 1)
Giligilani (fresh coriander)
Matayarisho
Marinate samaki na chumvi, limao, kitunguu swaum, tangawizi kwa muda wa masaa 6 au zaidi. Baada ya hapo wakaange au waoke katika oven mpaka waive ila usiwakaushe sana. Baada ya hapo saga pamoja nyanya ya kopo, kitunguu maji, kitunguu swaum na tangawizi. Kisha bandika huo mchanganyiko jikoni na upike mpaka ukauke maji kisha tia mafuta, binzari zote, curry powder, chumvi na pilipili na upike kwa muda wa dakika 5. Baada ya hapo tia maji kidogo (kama 1/2 kikombe) pamoja na tui la nazi. Acha uchemke mpaka tui liive na mchuzi ubakie kiasi. Baada ya hapo waweke samaki kwenye sufuria ya kuokea na kisha umwagie huo mchuzi juu ya hao samaki na owaoke (bake) kwa muda wa dakika 20. Ukisha toa kwenye oven katakata giligilani na utie kwenye hao samaki na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. unaweza kuwala na wali, ugali au chapati
Amri ya Pili ya Mungu: Tunakatazwa kuapa bure au uongo kwa Jina la Mungu
Katika amri ya pili ya Mungu tumekatazwa nini?
Katika amri ya pili ya Mungu tunakatazwa kuapa bure kwa Jina la Mungu
Kiapo cha uongo ni nini?
Ni kuahidi kwa kiapo bila nia ya kutimiza au kuvunja ahadi iliyotelewa.
Nguvu na Umuhimu wa Upendo
Utangulizi
Katika fadhila zote, upendo ndio unaonyesha uwepo wa fadhila nyingine
Upendo ni Amri kubwa kuliko zote
Upendo ni Utimilifu wa Sheria
Upendo ni Utakatifu
Upendo ni Ukamilifu
Upendo unazaa umoja
Upendo unadumisha Amani
Upendo ni Kila Kitu
Nguvu na Umuhimu wa Upendo katika Maisha ya Kikristo
Katika maandiko ya Kikristo, upendo una nafasi ya pekee na una nguvu kubwa sana katika kuonyesha uwepo wa fadhila nyingine zote. Upendo ni msingi wa kila tendo jema na ni kiini cha imani yetu. Hebu tuangalie kwa undani jinsi upendo unavyojidhihirisha katika nyanja mbalimbali za maisha yetu ya kiroho na kijamii.
Upendo ni Amri Kuu Kuliko Zote
Yesu Kristo alifundisha kwamba upendo ni amri kuu zaidi kuliko amri zote. Katika Mathayo 22:37-39, Yesu alisema:
“Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ya kwanza. Na ya pili inafanana na hiyo, Mpende jirani yako kama nafsi yako.” (Mathayo 22:37-39)
Amri hizi mbili zinabeba uzito wa sheria yote na manabii. Upendo kwa Mungu na upendo kwa jirani ni msingi wa maisha ya Kikristo na ni muhimu kwa kufanikisha maisha ya kiroho.
Upendo ni Utimilifu wa Sheria
Mtume Paulo anaeleza kwamba upendo ni utimilifu wa sheria. Katika Warumi 13:8-10, Paulo anasema:
“Msilimane deni lo lote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria. Kwa maana lile usizini, usiue, usiibe, usitamani, na likiwapo lingine lo lote, linajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Upendo haumfanyii jirani neno baya; basi upendo ndio utimilifu wa sheria.” (Warumi 13:8-10)
Upendo unatimiza sheria kwa sababu hautendi mabaya kwa wengine. Badala yake, upendo unaleta matendo mema na huruma kwa jirani.
Upendo ni Utakatifu
Upendo unahusiana moja kwa moja na utakatifu. Mungu ni upendo (1 Yohana 4:8) na anawaita wafuasi wake kuwa watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Mtakatifu ni mtu anayefuata amri za Mungu na kuonyesha upendo kwa wengine. Upendo wa kweli unatufanya kuwa kama Mungu kwa matendo na tabia.
Upendo ni Ukamilifu
Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwa wakamilifu kama Baba yao wa mbinguni alivyo mkamilifu. Katika Mathayo 5:48, Yesu alisema:
“Basi, iweni wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.” (Mathayo 5:48)
Ukamilifu huu unafanikiwa kwa njia ya upendo. Tunapopenda bila masharti, tunajitahidi kufikia kiwango cha ukamilifu ambacho Mungu anatamani tuwe nacho.
Upendo Unazaa Umoja
Upendo unaleta umoja miongoni mwa watu. Mtume Paulo aliandika katika Wakolosai 3:14:
“Zaidi ya yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.” (Wakolosai 3:14)
Upendo ni kama gundi inayounganisha watu pamoja na kudumisha umoja katika jamii na kanisa. Kwa upendo, tunavumiliana, tunaelewana, na kushirikiana kwa lengo la kufanikisha kusudi la Mungu.
Upendo Unadumisha Amani
Amani inapatikana kupitia upendo. Mtume Paulo katika Warumi 12:18 alieleza umuhimu wa kuwa na amani na watu wote:
“Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” (Warumi 12:18)
Upendo unatusaidia kuishi kwa amani na majirani zetu, kuleta maelewano na kuondoa migogoro. Tunapopenda, tunakuwa tayari kusamehe, kuvumilia, na kuleta amani katika mazingira yetu.
Upendo ni Kila Kitu
Upendo ni msingi wa kila kitu katika maisha ya Kikristo. Mtume Paulo alisisitiza umuhimu wa upendo katika 1 Wakorintho 13:1-3:
“Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo, au upatu uvumao. Tena nijapokuwa na kipawa cha unabii, na kujua siri zote, na maarifa yote; nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu. Tena nijapowapa maskini mali yangu yote, na nijapojitoa mwili wangu nichomwe moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.” (1 Wakorintho 13:1-3)
Bila upendo, matendo yetu yote ni bure. Upendo unatuwezesha kufanikisha maisha ya kiroho na kutimiza mapenzi ya Mungu kwa uaminifu.
Hitimisho
Upendo ni nguvu kuu inayojidhihirisha katika fadhila zote. Kwa upendo, tunatimiza sheria, tunakuwa watakatifu, tunakamilika, tunaleta umoja, na kudumisha amani. Upendo ni kila kitu katika maisha ya Kikristo na ni njia ya pekee ya kuonyesha uwepo wa Mungu ndani yetu. Kwa hivyo, na tujitahidi kuishi kwa upendo, tukiwa na uhakika kwamba tunafuata mapenzi ya Mungu na kutimiza wito wetu kama wafuasi wa Kristo.
Mapishi ya Ugali na dagaa
Mahitaji
Dagaa (dried anchovies packet 1)
Unga wa ugali (corn meal flour 1/4 kilo) (unaweza kutumia unga wa choice uipendayo)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2)
Kitunguu maji (onion 1)
Limao (lemon 1/4)
Pilipili mbuzi nzima bila kukata (scotch bonnet pepper1, do not chop)
Chumvi (salt 1/4 ya kijiko cha chai)
Mafuta (vegetable oil)
Hoho (green pepper)
Matayarisho
Chambua dagaa kwa kutoa vichwa vyao na utumbo, baada ya hapo waloeke katkika maji ya moto kwa muda wa dakika 5 na uaoshe tena katika maji ya baridi na uwakaushe uwaweke pembeni. Ukishamaliza katakata kitunguu na uandae nyanya tayari kwa upishi. Bandika sufuria ya kupikia dagaa jikoni na utie mafuta, yakishapata moto tia vitunguu pamoja na dagaa. Kaanga mpaka dagaa wawe light brown kisha tia nyanya, chumvi na pilipili. Pika nyanya mpaka ziive (ukitaka kujua kama nyanya zimeiva utaona zinatengana na mafuta) Baada ya hapo kamulia limao kidogo sana na tia pilipili hoho na zipike kama dakika mbili. kisha ipua.
Ukisha maliza kupika dagaa andaa chungu cha ugali. Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka, Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukisha iva pakua na usevu na mboga tayari kwa kuliwa.
Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi
VIAMBAUPISHI
Unga – 3 Vikombe vya chai
Siagi – 250 gms
Baking powder – 3 Vijiko vya chai
Mayai – 2
Chumvi – 1 kijiko cha chai
Maziwa – 1/2 Kikombe
Pilipili manga ya unga 1 Kijiko cha chai
MAANDALIZI
Katika bakuli la kusagia (blender) au mashine ya keki, tia siagi, chumvi na mayai, piga mpaka iwe kama malai (cream).
Tia Unga, baking powder, pilipili manga.
Tia maziwa.
Kata usanifu (design) unayotaka na sokota au kunja kwa usanifu unaopenda.
Pika (bake) katika moto wa 350º C – usiviache vikawa rangu ya udongo (brown) sana.
Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan
Mahitaji
Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa – 2 LB
Mchanganyiko wa dengu (hadesi, mchele, chooko, ngano, dengu n.k au nunua ya tayari iliyokwisha changanywa – 2 Vikombe
Kitungu maji (vikate vidogo) – 1
Mafuta – ¼ Kikombe
Nyana kata ndogo ndogo – 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawazi iliyosagwa – 1 Kijiko cha supu
Bizari ya haliym – 2 vijiko vya supu
Nyanya ya kopo – 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama na chumvi ½ kijiko mpaka iive, toa mafupa.
Chemsha mchanganyiko wa dengu mpaka ziive.
Katika sufuria weka mafuta, kaanga vitunguu vilainike, tia thomu na tangawizi, bizari ya haliym, nyanya ya kopo. Kaanga mpaka iwive.
Tia nyama iliyowiva na supu yake kidogo.
Tia mchanganyiko wa dengu tia kwenye mashine ya kusaga (blender), saga na ile supu ya nyama isagike vizuri
Mimina kwenye sufuria changanya, tia ndimu kidogo, acha moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 15.
Tia katika bakuli, pambia kwa vitunguu vilivyokaangwa vya rangi ya hudhurungi vikavu, pilipili mbichi (ukipenda) na kotmiri, ikiwa kuliwa.
Maswali na Majibu kuhusu Kanisa Katoliki
Sala ya kanisa ni nini?
Vyanzo vya sala za Kikristo
2. Litrujia ya kanisa
3. Fadhila za Kimungu
4. Matukio ya kila siku
Je, ni sahihi kusali sala kwa kurudia rudia mfano Novena?
Je ni makosa kurudia sala maneno yale yale kwa Mfano Rozari?
Sala kwa Mkatoliki ni nini hasa? Tunaposema sala tunamaanisha nini hasa?
Yesu alifundisha tusali vipi?
Ni ipi sala kubwa ya Kanisa?
Ni ipi sala bora kwa Bikira Maria? Kwa nini Tunasali kwa Bikira Maria?
Kwa nini watu wengi wanaomba kwa Bikira Maria?
Bikira Maria anatuombea kwa jina na mamlaka ya nani?
Je ni halali au ni sawa kwa Bikira Maria kutuombea kwa Jina la Yesu? Na Je tunajuaje kuwa Bikira Maria anaushirika na Yesu?
Je ni kweli kwamba Bikira Maria ni Malkia wa Kipepo?
Umwilisho maana yake ni nini?
Kanisa linafafanuaje fumbo la umwilisho?
Kanisa Katoliki ni nini?
Ni nini Msingi wa Imani na Mafundisho ya Kanisa Katoliki?
2. Mapokeo Matakatifu
3. Mamlaka ya Kanisa
Ni nani ameanzisha Kanisa Katoliki?
Yesu aliweka makanisa mangapi? Yesu hakufanya makanisa mengi?
Kwa kusudi gani Yesu alianzisha Kanisa?
Kanisa linatimiza kusudi la Yesu Kristo kwa namna gani?
2. Kwa Ukuhani wake yaani kuwatakasa watu
3. Kwa Uchungaji wake yaani kuwaongoza watu.
Alama za kanisa la kweli ni zipi?
2. Kanisa ni a Takatifu
3. Kanisa ni Katoliki
4. Kanisa ni la Kitume
5. Kanisa ni la Kimisionari
Kanisa ni Moja maana yake ni nini?
Kanisa ni Takatifu maana yake ni nini?
2. Kristo aliye Mtakatifu alijitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake ili kulitakasa
3. Roho Mtakatifu hulihuisha kwa upendo wake
4. Ndani yake wamo Bikira Maria na Watakatifu wengi wanaoliombea
Kanisa ni Katoliki maana yake ni nini?
Kanisa ni la Kitume maana yake ni nini?
Kanisa ni la Kimisionari maana yake ni nini?
Yesu amemweka nani kuwa mkubwa wa Kanisa?
Kanisa Katoliki laweza kudanganya katika mafundisho yake?
Jimbo Katoliki ni nini?
Tuwaonaje Wakristo ambao sio Wakatoliki?
Nje ya Kanisa Katoliki hakuna Wokovu maana yake ni nini?
Taifa la Mungu limeundwa kwa namna gani?
Maklero ni wakina nani?
Watawa ni akina nani?
2. Kwa kuishi masharti ya injili, utii, ufukara na useja mtakatifu.
3. Kwa kufuata mtindo wa maisha uliokubalika na Kanisa
Walei ni wakina nani?
Ushirika wa Watakatifu ni nini?
2. Ni muungano wa Waamini wote katika Ekaristi Takatifu.
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Mungu? Na kwa nini aheshimiwe?
Je, Bikira Maria kuitwa Mama wa Mungu maana yake ni kwamba yeye ndiye chanzo cha Yesu na Bila yeye Yesu asingekuwepo?
Je Bikira Maria anamwonaje Yesu? Bikira Maria Anamchukulia Yesu kama nani Kwake?
Kwa nini Bikira Maria anapewa Heshima kubwa
Je, Bikira Maria anastahili kuabudiwa? Je Tunamwabudu Maria?
Kwa nini tunamuheshimu Bikira maria na kusali kwake?
Ni kwa nini Bikira Maria anaitwa Mama wa Kanisa?
Bikira Maria anafaida yeyote kwa Kanisa?
Nafasi ya Heshima kwa Bikira Maria ni ipi?
Kwa nini wakatoliki wanaweka sanamu Kanisani?
Sanamu au picha sio haramu bali maana ya hiyo sanamu au picha ndio inaiharamisha.
Tofauti ya Sanamu za Kikatoliki na za kipagani ni Kwamba,
Sanamu za Kipagani: Sanamu hizi huchukuliwa kama Mungu na huabudiwa na kutolewa Sadaka kama Mungu Mwenyewe.
Sanamu za Kikatoliki: Sanamu hizi huchukuliwa kama ishara ya kile inachokiwakilisha, haiabudiwi kamwe bali inaheshimiwa tuu.
Jifunze kupitia Sanduku la Agano na Msalaba wa Yesu
Kwa nini tunasali mbele ya Picha/Sanamu na Hasa kufanya Ishara ya msalaba?
Kwa nini watu wanabusu picha na sanamu?
Je, inafaa tushike neno lolote la Agano la Kale kama Wayahudi?
Je, ufunuo wa Mungu unaweza kufafanuliwa rasmi na kila mtu?
Tupokeeje ufunuo wa Mungu?
Tunaweza kusadiki vipi?
Je, miujiza inaweza kutusaidia tusadiki?
Kanisa linahusika vipi na imani?
Je, tukipata mafundisho ya Kanisa tunapaswa kuyasadiki?
Tunapaswa kusadiki hasa nini?
Je, Mungu amegawanyika sehemu tatu?
Kwa nini Maria anastahili kuitwa “Mama wa Mungu”?
Je, Bikira Maria ni kama Bahasha au chombo cha kumleta Yesu tuu Duniani au anayo thamani zaidi?
Kanisa maana yake nini?
Je, Kanisa ni kundi la binadamu tu?
Je, tunaweza kuambatana na Yesu tukilikataa Kanisa?
Je, Kanisa ni muhimu kwa wote?
Wokovu unapatikana wapi?
Mtu akijua Kanisa ni la lazima kwa wokovu asiingie au ajitenge nalo, itakuwaje?
Je, anayejiunga na Kanisa na kudumu ndani yake ana hakika ya kuingia mbinguni?
Sifa kuu za Kanisa ni zipi na zinapatikana wapi?
Kanisa kuwa moja maana yake nini?
Kanisa kuwa takatifu maana yake nini?
Kanisa kuwa katoliki maana yake nini?
Kanisa kuwa la Mitume maana yake nini?
Kanisa limepewa na Yesu muundo gani?
Je, Yesu amejenga Kanisa lake imara juu ya mwamba?
Papa amejaliwa na Mungu mamlaka gani?
Maaskofu wote wamerithi mamlaka gani?
Maaskofu wanasaidiwa na nani?
Bila ya Maaskofu, mapadri na mashemasi, Kanisa lingekuwaje?
Walei wanaitwa na Mungu kufanya nini?
Watawa wanashika mashauri gani ya Kiinjili?
Ushirika wa watakatifu maana yake nini?
Je, Kanisa linaweza kutuondolea dhambi yoyote?
Ekaristi maana yake nini? Je ni kweli Yesu yupo katika Maumbo ya Mkate na Divai?
26Maana kila mnapokula mkate huu na kukinywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja. 27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana. (1Kor 11:23-27).
Yesu alituambia nini kuhusu Mwili wake na damu yake?
Damu na Mwili aliotupa Yesu ni nini? Ekaristi ni nini hasa?
Fundisho hili la mwili na damu ya Yesu (Ekaristi) lilikua Agizo tunalopaswa kulitii mpaka leo?
Mitume walitii Fundisho la Ekaristi na waliliishi?
Je mkate na divai vilichukuliwa na Mitume kama nini hasa? walichukulia Ekaristi kama nini?
Je ni lazima Kwa Mkristu kupokea Mwili na damu ya Yesu (Ekaristi)?
Je ni kwa nini madhehebu mengine hawakubali mafundisho haya ya Ekaristi Takatifu, Je ni mara ya kwanza watu kukataa?
Hata wakati Yesu akiyasema maneno haya Wafuasi Wengi Walimwacha kama Biblia inavyosema;
Mitume walifundisha nini kuhusu Mwili na Damu ya Kristu (Ekaristi)?
Je Yesu Yupo Mzima katika Ekaristi Takatifu? Na kwa nini Tunaabudu Ekaristi?
Kwa hiyo basi kama tunavyosoma katika Yoh 6:51; na
Je, daraja takatifu zinahitajiwa kabisa na Kanisa?
Je, wenye daraja wanastahili heshima?
Kanisa linaheshimu marehemu kwa namna gani?
Je, Kanisa linahimiza waamini wapokee Ekaristi wakati gani?
Biblia ni nini? Asili, Historia, waandishi na mipaka yake
Je, Biblia ilipatikanaje? Nini chanzo na asili ya Biblia.
Je, Biblia ndicho kitabu pekee cha neno la Mungu?
Je nje ya Biblia hakuna Neno la Mungu au Maandiko matakatifu?
Je Biblia ndiyo mafundisho ya Mungu pekee?
Biblia inatuthibitishia yenyewe kuwa haijakamilika na Si mambo yote yameandikwa Kwenye Biblia
Biblia inatuambia hivi…”Kuna mambo Mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo Kama yangeandikwa yote, moja baada ya jingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.”…Kwa mstari huu Biblia inatuthibitishia kuwa haikuandikwa vitu vyote.
Je Biblia ni mwisho wa Maandiko ya Mungu?
Sababu ya Kanisa katoliki kutumia mapokeo na Maandiko ya Watakatifu
Yesu alituambia nini kuhusu Neno la Mungu na Mwendelezo wa kazi ya Mungu ya kusema na watu?
Utengenezaji wa Makalio ni Hatari na Hutakiwi kufanya
Mwanamke wa miaka mitatu amefariki baada ya kuripotiwa kuelekea Uturuki kwa aina ya upasuaji kwa jina Brazilian Butt Lift [uongezaji wa makalio}.
Ni kwa nini upasuaji huu ni maarufu mbali na kwamba ni hatari kufanyiwa upasuaji huo ughaibuni.
Leah Cambridge kutoka Leeds alipatikana na mishtuko mitatu ya moyo baada ya kudungwa sindano ya ganzi katika kliniki moja katika mji wa Izmir, mwenzake Scott Franks aliambia gazeti la the sun.
Anaeleweka kufanyiwa BBL ama upasuaji wa kuongeza makalio ambapo mafuta kutoka katika tumbo hutiwa katika makalio.
‘Mrembo huyo alikubali kufanya upasuaji ughaibuni ambapo ni bei nafuu ikilinganishwa na Uingereza baada ya kukerwa na mafuta mengi katika sehemu yake ya tumbo baada ya kupata watoto’, alisema bwana Frank.
Majirani wake wamemtaja kuwa mtu anayevutia, wakiongezea kuwa wanaamini alielekea kufanyiwa upasuaji huo mwezi uliopita bila kumshauri mpenziwe.
Na bi Cambridge sio mwanamke wa kwanza Muingereza ambaye hamu yake ya kuwa na makalio ya kuvutia yalimwangamiza akiwa ughaibuni.
Joy Williams alifanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio yake mjini Bangkon nchini Thailand mnamo mwezi Octoba 2014.
Vidonda vyake vilipata maambukizi na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 kutoka mjini London , alifariki akidungwa sindano ya ganzi.
Miaka mitatu kabla , Claudia Aderotimi mwenye umri wa miaka 20 , kutoka Hackney , mashariki mwa London alifariki kutokana na matibabu ya kujiongeza makalio yake katika hoteli moja nchini Marekani.
Upasuaji wa kuongeza makalio hauonekani kuwa hatari zaidi ya aina nyengine zozote za upasuaji, kulingana na daktari wa upasuaji wa urembo Bryan Mayou.
‘Hatari yake ni upasuaji huo kufanywa na madaktari ambao hawajahitimu, nje ya kliniki bila kuwa na maelezo ya jinsi ya kujichunga baada ya matibabu hayo kufanywa’, anasema bwana Mayou, mwanachama wa muungano wa madaktari wa upasuaji nchini Uingereza.
Iwapo mafuta yataingizwa katika tishu ya sehemu ya makalio kuna hatari ya kuingiza mafuta hayo katika mishipa mikubwa ya damu.
Mafuta hayo yanaweza kupita katika mishipa ya damu , kuingia katika mapafu kabla ya kusababisha kifo.
Bwana Frank aliambia gazeti la The sun : Leah alikuwa amedungwa sindano ya ganzi akakumbwa na matatizo baada ya mafuta kuingia katika mishipa yake ya damu hatua iliofanya viwango vyake vya oxygen katika damu kushuka .
Hali yake iliimarishwa lakini alikumbwa na mishtuko mitatu ya moyo na hawakuwa na la kufanya.
‘Madaktari wa upasuaji kutoka jamii za kimataifa wameunda jopo kuchunguza kuripoti kuhusu utaratibu huo”, anasema Mayou.
‘Viwango vya vifo vinavyotokana na utaratibu huo ni kisa kimoja kati ya 3000 huku vifo vyote vilivyochunguzwa vikihusisha mafuta yaliopatikana ndani ya mishipa ya misuli ya makalio’, anasema.
Ni mtindo wa kisasa, miaka kadhaa iliopita kila mtu alipendelea kuwa mwembamba na walikuwa wakisema kuwa wanataka kufanyiwa upasuji ili kufanya makalio yao kuwa madogo.
‘Na hiyo ndio mbinu ambayo inaweza kutumika iwapo mtindo mpya wa kuongeza makalio utakwisha na mwathiriwa anataka makalio yake kurudishwa yalivyokuwa’, anasema.
Kwa nini watu wanapendelea sana kuwa na makalio makubwa ? ni kutokana na utamaduni maarufu wa kushabikia maungo yanayovutia.
Watu maarufu kama vile Kim Kardashian , Kylie Jenner na Cardi B wana umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijmaii ambapo huchapisha picha zao wakionyesha makalio yao yalio mviringo.
Jenner alichapisha katika blogi yake ambapo alisifu maumbile yake na uzani ulioongezeka.
”Sijaongezewa makalio. Unajua, nilikuwa na uzani wa 120 [lbs]. Nilikuwa mwembamba sana. Sasa nianelekea 136Ibs , lakini ni sawa napendelea uzani nilionao”.
Hatahivyo, Cardi B amefichua kwamba kabla ya kuingia katika fani ya muziki aliongezewa makalio huko mjini New York na kifaa alichowekewa ndani kilivuja kwa siku tano baadaye.
Katika mahojiano alisema kuwa alilipa takriban $800 (£564) kwa upasuaji huo baada ya kuwaona wachezaji densi wanzake walio uchi katika vilabu vya burudani walio na makalio makubwa wakipata fedha nyingi kumliko.
Chloe Simms, ambaye ni nyota wa kipindi cha runinga cha The Only Way Is Essex, amekuwa wazi kuhusu makalio yake aliyoongezewa baada ya kulalamika katika kipindi hicho kwamba alikuwa hana makalio.
Faida za kunywa juisi ya ubuyu
Mungu ameumba miti na mimea kwa ajili ya binadamu. Kila mti au mmea una makusudio yake. Mbuyu ni miongoni mwa miti yenye faida nyingi na maajabu mengi. Vitu vyote vilivyomo kwenye mbuyu vinatumika kama chakula au dawa kwa faida ya binadamu.
Faida za kunywa juisi ya Ubuyu
Unga wa ubuyu unaelezwa kuwa na vitamini na madini mengi kuliko matunda mengine yoyote unayoyajuwa.
- Inaelezwa kuwa unga wa ubuyu una vitamini C nyingi mara 6 zaidi ya ile inayopatikana katika machungwa.
- Ubuyu una kiwango kingi cha madini ya Kashiamu (Calcium) mara 2 zaidi ya maziwa ya ng’ombe, pia madini mengine yapatikanayo katika ubuyu ni pamoja na madini ya Chuma, Magnesiamu na Potasiamu ambayo ni mara 6 zaidi ya ile potasiamu ipatikanayo katika ndizi!
- Husaidia kujenga neva za fahamu mwilini
- Ina virutubisho vya kulinda mwili
- Ubuyu una vitamini B3 na B2 ambayo ni mhimu katika kuondoa sumu mwilini na umeng’enyaji wa madini ya chuma, kimsingi vyakula vyenye afya zaidi kwa ajili ya mwili ya binadamu huwa pia huwa na vitamin B2.
- Unaongeza kinga ya mwili sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamini C
- Huongeza nuru ya macho
- Husaidia kuzuia kuharisha na kutapika
- Ina magnesiam ambayo husaidia kujenga mifupa na meno
- 10Husaidia wenye presha ya kushuka na wenye matatizo ya figo
Unywe kiasi gani? Jipatie kikombe kimoja cha juisi ya ubuyu kila siku hasa usiku na baada ya wiki kadhaa utaona matokeo yake mwilini.
Ili upate faida za juisi ya ubuyu, zinazoelezwa hapa, lazima upate ule ubuyu halisi (mweupe) usiochanganywa na kitu kingine cha kuongeza ladha au rangi.
Faida za kufanya Masaji kiafya
Masaji uongeza kinga ya mwili
Masaji kushuka kwa homoni inayohusika na kupunguza maambukizi mbalimbali homoni ijulikanayo kama ‘cytokines’ vile vile masaji inashusha homoni inayohusika na matendo ya mashari homoni ijulikanayo kama ‘cortisol’.
Kufanya masaji hakukufanyi ujisikie ni mtulivu peke yake, bali pia kunaweza kukuongezea kinga yako ya mwili.
Masaji ya dakika 45 kwa siku imethibitika kuongeza uwingi wa seli nyeupe za damu (lymphocytes) ambazo ndizo hupigana dhidi ya vijidudu nyemelezi vya magonjwa mbalimbali mwilini.
Kufanya masaji huondoa tatizo la kukosa usingizi
Tafiti nyingi zinasema masaji inao uwezo wa kuamsha mawimbi ndani ya ubongo yanayohusiana na kutengenezwa kwa usingizi mzito (delta waves) na hii ndiyo sababu kwanini wengine hupitiwa na usingizi mzito mara tu baada ya mazoezi ya masaji.
Tatizo la kukosa usingizi linaweza kutibika kwa kufanya masaji tu kwakuwa masaji husaidia kupunguza uchovu na kuongeza uwezo wa kupata usingizi mtulivu kwa watu wa rika zote yaani watoto wadogo mpaka wazee ikihusisha wale wenye matatizo ya akili, kansa na magonjwa ya moyo, machache kati ya magonjwa mengi yawezayo kutibika kwa masaji tu.
Kuondoa mfadhaiko wa akili au Stress
Masaji huondoa hamaki na maumivu huku yakiongeza uwezo wa kupata usingizi mzuri na wa uhakika.
Masaji huondoa huzuni
Watafiti wanasema kuwa masaji kuongezeka homoni ijulikanayo kama ‘oxytocin’ na kupungua kwa homoni nyingine iitwayo ‘adrenocorticotropin’.
Oxytocin inahusika na matendo ya huruma, maono, upendo na ushirikiano wa kijamii. Wakati adrenocorticotropin yenyewe huhusika na kupungua kwa mfadhaiko (stress) moja kwa moja.
Kuondoa maumivu mbalimbali mwilini
Masaji hupunguza maumivu hasa ya mgongo na maumivu ya kichwa na maumivu ya kwenye mishipa.
Masaji huongeza uwezo wa kujiamini
Masaji hutuliza mwili na kuongeza concentration
Jinsi ya Kufuga vizuri kware Kwa Faida
Kware au Kwale au Kereng’ende ni jamii ya ndege ambao kwa sasa wanafugwa majumbani na wanaotaga mayai kama kuku ama bata na kwa wingi sana.
Ndege hawa ni wadogo 280gm – 300gm, rangi ya kwale ni kahawia au kijivu na wana michirizi au madoa. Mara nyingi miguu yao ni myekundu au rangi ya manjano na koo lao ni jekundu, jeupe, jeusi au rangi ya manjano.
Chakula
1. Kware anakula chakula chochote anachoweza kula kuku ikiwemo chakula cha broiler. Kama utaamua kuwapa chakula cha broiler unawapa “starter” kware wenye umri kuanzia siku moja hadi wiki ya tatu baada ya hapo unawapa Falcon au hill.
2. Ukiweza kuwatengenezea chakula chako mwenye kutumia pumba nk. Ni vizuri zaidi kwa mayai yenye lishe 100%
3. Kware 100 wenye umri wa mwezi hutumia kiroba cha kilo 20 kwa wiki 3.
4. Kware hawamalizi chakula kama kuku.
5. Pia kware hupewa majani kama mchicha nk.
Kutaga na kuatamia kwa Kware
Kware dume humpanda jike kwa muda kidogo, Hapo jike anakuwa tayari kutaga na hutaga mayai 290 hadi 310 kwa mwaka (hii hulingana na lishe nzuri atakayopatiwa).
Mayai ya Kware huatamiwa kwa siku 18 na huanza kuanguliwa vifaranga kwa muda wa siku 2, kuanzia siku ya 18 na hadi 20.
Njia bora ya kutotolesha mayai ya Kware ni kwa kutumia incubator ambapo mayai huatamiwa kwa wingi ndani ya siku 18.
Utunzaji wa vifaranga vya kware na chakula
Utunzaji wa vifaranga vya kware Siku 1 – 7
Vifaranga wapatiwe chakula “STARTER PELLET” na maji masafi ya kutosha. Siku ya 1 wawekee ‘GLUCOSE’ kwenye maji, Packet moja kwa lita 20 za maji, na siku ya pili hadi ya tano wawekee Amin Total kwenye maji, Wape maji pekee siku ya sita na siku ya saba wapatie chanjo ya Newcastle. Utawapatia joto kwa njia ya umeme kwa ‘BULB’ mbili (2) za 200watts kwa kila vifaranga 300, ama unaweza kuweka taa ya ‘Energy Server’ pamoja na jiko la mkaa uliofunikwa na majivu ambao utakidhi kuwapatia joto sawia kwa masaa 24 kwa siku 7. (Majivu yanasaidia moto kukaa kwa muda mrefu)
Banda/box lako liwe la ukubwa wa 1.5m x 1.5m (au eneo la ukubwa huo ndani mwa banda kubwa la kufugia kuku) lazima uzingatie usalama wa vifaranga dhidi ya panya, paka au vicheche. Unatakiwa kuweka magazeti au mabox chini kwenye sakafu yatakayosaidia usafi. Kwa week ya kwanza chakula kitawekwa chini na tunashauri utumie chakula cha pellet ili kusaidia vifaranga wasiteleze na kuathiri miguu. NOTE: Weka gololi au mawe kwenye drinkers zako ili kuzuia vifaranga wasizame ndani ya (drinkers) maji na kufa.
Utunzaji wa vifaranga vya kware Siku 8-14
Vifaranga wataendelea kupewa chakula “STARTER PELLET” na maji safi. Wataendelea kuhitaji ‘mwanga’ wa kutosha muda wote na joto la wastani bulb 2 za watts 100 au moja ya watts 200
Utunzaji wa vifaranga vya kware Siku 15-21
Uhitaji wa joto utapungua, ila ni kipindi ambacho wanakula chakula zaidi kwa ajili ya kukua. Ni vizuri waendelee kupata taa ili kupata mwangaza utakayowawezesha kula mchana na usiku.
Utunzaji wa vifaranga vya kware Siku 21 na Kuendelea
Kware wako hawatahitaji joto tena wawekee taa tu za energy server kipindi cha usiku, wape chakula na maji ya kutosha zaidi kwa ajili ya kukua.
UTAGAJI WA KWARE
WIKI YA SITA
Wiki ya sita kuelekea ya saba Kware wako wataanza kutaga mayai kila siku, kwa wastani Kware mmoja hutaga mayai 300 kwa mwaka.
Magonjwa ya Kware
Kware ni ndege wenye kinga kubwa na ni vigumu sana kushambuliwa na magonjwa kama kuku na mara wanapougua ni rahisi sana kutibika. Magonjwa yanayoweza kuwapata Kware ni typhoid, mafua na kuharisha .
Tiba za asili za kware
Waweza kuwatibu vifaranga au Kware wako kwa kutumia njia ya asili ambayo pia ni rahisi, gharama nafuu na bora zaidi kuliko kutumia madawa yaliyochanganywa na kemikali na yenye gharama.
Vifuatazo ni vitu vya asili vinavyotumika kutibu magonjwa mbali mbali kwa Kware na yanayopatikana kwa wingi katika maeneo ya mfugaji. Madawa haya hutumika kwa kiwango cha wastani na hayana kipimo maalum kwani hata ukiyazidisha hayana madhara.
Mwarobaini na Aloe Vera:
Madawa haya hutumika kutibu kuharisha damu pamoja na mafua kwa vifaranga vya Kware. Chukua kiasi kidogo cha mwarubaini kisha twanga vizuri kupata maji maji. Kamua maji yale, kisha weka katika maji uliyoandaa kuwanywesha vifaranga wako. Kata vipande vidogovidogo vya aloe vera (jani moja laweza kutosha) na tia katika maji yaliyochanganywa na mwarobaini, kisha wapatie vifaranga wanywe (Aloe Vera itaendelea kujikamua yenyewe ikiwa ndani ya maji huku vifaranga wakiendele kunywa).
Kitunguu swaumu:
Hii hutumika kukinga na kutibu vifaranga vya kware wanaosumbuliwa na kuharisha damu. Unachukua kitunguu swaumu na kuondoa maganda ya nje kisha kusafisha na kukata vipande vidogo sana, na kuwawekea kama chakula. Vifaranga wanapenda sana vitunguu hivyo na watakula kwa kasi kama chakula lakini ni tiba tayari. Unaweza kuwapatia kila siku hadi watakapo pona.
Maziwa:
Maziwa yanayotokana na ng’ombe pia hutumika kutibu ugonjwa wa kuhara pamoja na kuwapa nguvu Kware waliolegea. Mnyweshwe maziwa hayo Kware anayeumwa bila kuyachemsha na umnyweshe maziwa ya kutosha kiasi cha kushiba. Unamnywesha mara tatu kwa siku. Hakikisha maziwa unayotumia yanatoka kwa ng’ombe wanaotibiwa kila mara.
Angalizo
Siyo lazima Kware waugue ndipo uwapatie tiba hizi. Hakikisha unawapa tiba kabla hata hawajaugua hivyo utawakinga na magonjwa hayo. Waweza kuchanganya madawa hayo yote kwa wakati mmoja kwani hayana madhara.
Endapo madawa ya asili hayapatikani katika eneo la mfugaji basi waweza kuwatibu Kware kwa madawa yafuatayo ambapo vipimo huelezwa moja kwa moja kwa maandishi katika madawa hayo au kuelezwa na muuzaji pale utakaponunulia; Amprolium kwa ugonjwa wa kuharisha damu (Coccidiosis), Fluban,Coridix au Doxyco kutibu mafua (Coryza) na Esb3,Trisulmycine au Trimazine hutumika kwa homa ya matumbo (Typhoid).
ZINGATIA:
Wanapokosa madini ya kutosha kwenye chakula huweza kupata madhara yafuatayo:-
1. Kuharisha
2. Kunyonyoka manyoya
3. Kupunguza kasi ya kutaga mayai.
Chanjo Ya kware
Siku ya 7 lazima vifaranga wapatiwe chanjo ya “kideri/mdondo”
(respiratory & digestive diseases) kwa dawa inayoitwa ‘newcastle’. Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya 14 lazima wapewe chanjo ya “gumboro”. Chanzo cha
maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya 21 lazima warudie chanjo ya “Newcastle (aina ya IBDL)”. Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya 35 lazima wapate chanjo ya “Ndui”.
Soko la kware
Mayai ya Kware ni bidhaa adimu sana hapa nchini kwa kuwa ni wafugaji wachache waliojikita katika ufugaji huu, Ufuatao ni muhtasari wa wastani wa bei ya bidhaa za Kware sokoni
1. Trei ya (mayai 30) ya KWALE inauzwa shilingi 30,000 .
2. Kifaranga wa Kware wa siku moja anauzwa shilingi 2500 – 3000
3. Kware wa week 4 (mwezi mmoja) anauzwa kwa shilingi 10,000– 12,000
4. Kware aliyeanza kutotoa (week 6) huuzwa shillingi 20,000 – 25,000
5. Kware kwa aliyekomaa kwa ajili ya kitoweo huuzwa kwa shilingi 25,000
6. DROPING za Kware huuzwa kwa shilingi 10,000 kwa 50kg kwa wafugaji wa samaki
Soko la KWALE liko juu sana kwa mayai na nyama. KWALE pia hutofautiana bei kwa jike na dume.
FAIDA ZA KUFUGA KWALE
Ufugaji wa kwale hua na faida ukilinganisha na ufugaji wa ndege wengine
· Chanzo cha kipato kwa wafugaji.
· Hawana gharama sana katika suala kufuga.
· Hawataji utaalam sana katika kuwafuga.
· Mayai yake ni tiba ya magonjwa mbalimbali.
· Mayai yake hayakosi soko.
Sababu inayopelekea kushindwa kuishi maisha ya ndoto zako
1. Hauko Tayari kuthubutu na kujiunga
2. Kutokujiamini
3. Kutopata sehemu sahihi ya kupata ushauri
4. Kutokuwa na sababu za msingi au malengo ya msingi ya kupigania ndoto zetu
5. Kukaa katika shauli la wasio haki na barazani pa wenye mizaha
Hizo ni baadhi ya sababu zinazopelekea watu wengi kushindwa kuishi maisha ya ndoto zao na kuishi maisha ya kawaida tofauti na fikra zao.
Kuthubutu ni jambo la muhimu sanaaa katika maisha ya mwanadamu kwa maendeleo ya kwake ,familia ,jamii pamoja na taifa kwa ujumla hivyo ndugu zangu nawasihi tuweze kua watu wanaothubutu.
Tuondoe uwoga katika maisha yetu Kwamaana Uwoga Ndio CHANZO CHA UMASKINI WETU tukiendeleea kuogopa mazingira yanayotuzunguka na jinsi gani watu watatuchukulia na kutusema atutaweza kupiga hatua.
Changamoto ni hali ya kawaida katika maisha ya mwanadamu , kuogopa changamoto nalo ni Kosa kubwa katika maisha yetu.
…………..Mwisho kabisa nipende kusema……………
USIJILINGANISHE NA MTU MWINGINE MAANA JUA NA MWEZI HAVIFANANI VYOTE UNG’ARA KWA WAKATI WAKE. TENGENEZA MAISHA YAKO ILI WATU PIA WATAMANI KUWA KAMA WEWE.
Mapishi ya choroko
Mahitaji
Choroko kikombe 1 na nusu
Nazi kopo 1
Kitunguu kikubwa 1
Nyanya 1/2 kopo
Swaum 1 kijiko cha chai
Curry powder 1 kijiko cha chai
Chumvi kiasi
Olive oil
Pilipili nzima
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima kisha zichemshe mpaka ziive na ziweke pembeni. Baada ya hapo saga pamoja nyanya, kitunguu, na swaum kisha vipike mpaka maji yote, baada ya hapo tia mafuta na curry powder, pika mpaka nyanya zitoe mafuta kisha tia choroko,tui la nazi, maji nusu kikombe,pilipili na chumvi, kisha koroga vizuri na uache ichemke. Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na rojo ibakie kidogo sana, kisha ipua na mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Mi huwa napenda kuila na wali ila hata na ugali au chapati inaenda pia.
Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha
Wali Wa Mpunga
Mchele wa mpunga – 4 Vikombe
Tui la nazi – 6 vikombe
Chumvi – kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele kisha
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.
Mchuzi wa nyama Ng’ombe
Nyama – 1 kilo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa -2 viijiko vya supu
Viazi/mbatata – 2
Kitunguu maji kilokatwakawa (slice ndogo) – 2
Nyanya/tungule – 4
Nyanya kopo – 3 vijiko vya supu
Majani ya mchuzi/mvu – 3 msongo (bunches)
Bizari ya mchuzi (simba 2) – I kijiko cha chai
Ndimu – 1 kamua
Mafuta – ¼ kikombe
Chumvi – kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Weka nyama katika sufuri, tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi, ndimu na chemsha nyama hadi iwive na ibakie supu yake kidogo.
Weka mafuta katika sufuri nyingine, kaanga kitunguu. Vinapogeuka rangi tia majani ya mchuzi endelea kukaanga hadi vigeuke rangi ya hudhurungi (golden brown)
Tia nyanya/tungule, viazi/mbatata, endelea kukaanga mpaka nyanya ziive.
Tia nyama na supu yake kisha tia nyanya ya kopo, kotmiri, bizari ya mchuzi, chumvi uache mchuzi kidogo katika moto hadi viazi viive vikiwa tayari.
Mboga Mchicha
Mchicha – 4 michano/vifungu
Kitunguu – 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) – 3
Nyanya/tungule – 2
Tui la nazi zito – 1 kikombe cha chai
Chumvi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mboga iache ichuje maji.
Ikatekate kisha weka katika sufuria.
Katika kitunguu maji, kitunguu thomu kisage au kikatekate kidogodogo (chopped), nyanya.
Weka jikoni ipikike kwa maji yake na mvuke.
Tia tui endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi ikaribie kukauka ikiwa tayari.
Nilichojibu kwenye interview walipoulizia status
Nimetoka kufanya interview wakaniuliza status yangu nikaawabia status yangu ni Hey there! Iam using watsApp, wameniambia nitoke nje I think wanajadiliana namna ya kunipangia kituo cha kazi
Mapishi ya Tambi na nyama ya kusaga
Mahitaji
Tambi (Spaghetti)
Nyama ya kusaga
Kitunguu maji
Nyanya ya kopo
Kitunguu swaum
Tangawizi
Carrot
Hoho
Lemon
Chumvi
Curry powder
Mafuta
Fersh coriander
Matayarisho
Katakata vitunguu maji, carrot, hoho, kisha weka pembeni. Saga vitunguu swaum na tangawizi pamoja kisha weka pembeni. Baada ya hapo injika sufuria jikoni, tia mafuta. Yakisha pata moto tia vitunguu maji kaanga mpaka vigeuke rangi ya kahawia kisha tia kitunguu swaum na tangawizi.baada ya hapo tia nyanya ya kopo na iache ichemke mpaka iive. Baada ya nyanya kuiva tia curry powder na chumvi. Geuza mpaka mchanganyiko uchanganyike vizuri kisha tia nyama ya kusaga na uiache ichemke mpaka iive.Baada ya nyama kuiva tia Corrot na hoho na uzipike kwa muda wa dakika 2.Na baada ya hapo mboga itakuwa imeivaa, iipue na katia fresh coriander. Baada ya hapo injika sufuria yenye maji jikoni. Yaache yachemke na kisha tia chumvi na mafuta ya mzaituni (olive oil) na tambi. Acha zichemke mpaka ziive kisha zichuuje maji na chujio na baada ya hapo zitakuwa tayari kuseviwa na nyama.
SMS ya kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa unamjali na kumpenda milele
Tambua kuwa nakujali
Furahia kwamba nitakuwa na wewe
Katika siku zote za maisha yangu
Nitakupenda bila kikomo milele
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Watoto wa siku hizi ni shida! Angalia huyu mtoto anachomwambia baba yake
Ka ni wewe?
DOGO: baba mi siendi tena shule inaonekana walimu hawana uhakika na majibu yao.
BABA: Kwanini unasema hivyo?
DOGO: juzi walisema 3+4= 7, jana wakasema 1+6=7, halafu leo wanasema 5+2=7 sasa huoni kama wanatuchanganya.
ungekua wewe ungemjibu nini
Recent Comments