Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Jinsi ya kuandaa Muhogo, Samaki Wa Kuchoma Na Bamia

Featured Image

Mahitaji

Mihongo 3 - 4

Tui - 1000 ml

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu maji kilokatwakatwa - 1

Nyanya mshumaa - 3-4

Pilipili mbichi ndefu - 2-3

Pilipili boga - 2

Namna Ya Kutayrisha Na Kupika

Menya mihogo kisha ikate kate vipande inchi tatu hadi nne, kila kipande kigawe kitoke vipanda vinne. Toa mzizi katikati
Osha mihogo ipange kwenye sufuria ya nafasi na yenye mfiniko, ili upate nafasi ya kutia viungo unavyoona pichani na utokotaji wa tui wahitaji nafasi.
Panga/tandaza kitunguu, nyanya mshumaa/tungule,pilipili mbichi na pilipili boga juu ya mihogo, tia chumvi na tui lote.
Funika sufuria kisha weka jikoni moto wa kiasi kuchemsha tui lipande juu. Hakikisha tui halifuriki na kumwagika kwa kuchungulia au kufunika nusu mfuniko
Kwa mda wa nusu saa hivi ukiona sasa tui linatokota chini chini fuinika mfiniko na upunguze moto mdogo kabisa tui likauke kidogo na liwe zito.
Toa muhogo moja ubonyeze ukiona umewiva zima jiko na wacha sufuria hapo kwa muda wa 10. Mihogo tayari kuliwa.

Kidokezo.

Tui lote huwa chini baada ya mihogo kuwiva unapopakuwa teka kutoka chini uweze kupata uzito wa tui umwagie juu.

Bamia/Mabenda

Bamia - robo kilo

Nyanya - 3

Kitunguu maji - 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au ilosagwa - 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo (tomato paste) - 1 kijiko cha supu

Mafuta - 150 ml

Chumvi -1 kijiko cha chai

Pilipili boga - 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Kata vichwa vya bamia kisha zikate kate mara mbili zikiwa kubwa, ikiwa ni ndogo mno haina lazima kuzikata osha tu uweke kando.
Katika sufuria, katakata kitunguu, nyanya, pilipili boga tia ndani viungo hivi ongeza chumvi mafuta, thomu na nyanya kop
Washa moto mdogo mdogo huku umefunika sufuria kwa muda wa dakika 20 kisha ukiona mboga zimeshika kutokota ongeza bamia koroga.
Tia maji 200ml wacha kwa muda wa dakika 15 kupikika tena, ukionja utamu wa mboga na chumvi, hakikisha bamia pia zimewiva. Tayari kuliwa.

Samaki Wa Kuchoma

Samaki (dorado) au mikizi au una - 2 wakubwa (fresh)

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au iliyosagwa 1 ½ cha chai

Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayrisha Na Kuchoma

Safisha samaki vizuri mchane chane (slit) kwa ajili ya kuweka masala.
Changanya viungo vyote na chumvi samaki kisha paka katika samaki kote na ndani ya sehemu ulizochanachana. Mroweke kwa muda wa robo saa hivi.
Weka karatasi ya jalbosi (foil paper) katika treya ya oveni. Muweke samaki kisha mpike (grill) kwa moto wa juu achomeke hadi samaki agueke rangi na awive.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe

Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Mpunga - 4 vikombe

Nyama - 1 kilo moja

Kitunguu maji - 3

Mbata... Read More

MAPISHI YA LADU

MAPISHI YA LADU

VIAMBAUPISHI

Unga - 6 vikombe

Samli - ½kikombe

Baking Powder - ½kijiko cha ... Read More

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Ulaji wa mboga za majani ni muhimu kwa sababu zina vitamini na madini mengi na viwango vidogo vy... Read More

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora 🥗

Hakuna jambo bora kuliko... Read More

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele - 3 vikombe

*Maji ya kupikia - 5 vikombe

*Kidonge cha s... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Ufuta Na Jam

Jinsi ya kupika Biskuti Za Ufuta Na Jam

Viamba upishi

Unga 2 Viwili

Sukari ya kusaga 1/4 Kikombe

Siagi 250 gms

... Read More

Mapishi – Fish Finger

Mapishi – Fish Finger

Leo tunaangalia mapishi ya fish finger ( sijui kama unaweza kusema kidole cha samaki)!, Ni mlo mz... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu

Vipimo - Nyama

Nyama ng’ombe ya mifupa ilokatwa vipande - 1 kilo

Tangawizi na tho... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu

Vipimo - Nyama

Nyama ng’ombe ya mifupa ilokatwa vipande - 1 kilo

Tangawizi na tho... Read More

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Vipimo - Mahitaji Ya Nyama

Nyama ya n’gombe ya mifupa - 3 lb

Tangawizi mbichi il... Read More

Jinsi ya kupika Biriani Ya Nyama Mbuzi Ya Mtindi Na Zaafaraan

Jinsi ya kupika Biriani Ya Nyama Mbuzi Ya Mtindi Na Zaafaraan

Vipimo - Nyama

Nyama mbuzi - 1 kilo

Kitunguu menya katakata - 1

Nyanya/tungul... Read More

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Viazi - 4

Vitunguu - 2... Read More