Viamba upishi
Mashonanguo mkono 1
Tui la nazi kikombe 1
Karanga zilizosagwa kikombe Β½
Mafuta vijiko vikubwa 4
Kitunguu 1
Nyanya ndogo 2
Chumvi kiasi
Hatua
β’ Chambua mashona nguo mateke, osha na katakata.
β’ Menya osha na katakata kitunguu.
β’ Osha, menya na katakata nyanya.
β’ Kaanga karanga, ondoa maganda na saga zilainike.
β’ Kuna nazi na chuja tui.
β’ Kanga kitunguu, weka nyanya na koroga mpaka zilainike.
β’ Weka mashona nguo na chumvi kisha koroga sawa sawa,
funikiakwa dakika 5 -10.
β’ Changanya tui la nazi na karanga, ongeza kwenye hizo mboga
ukikoroga kwa dakika 5, punguza moto ili ziive taratibu.
β’ Onja chumvi na pakua kama kitoweo.
Uwezekano
Changanya mnavu, mgagani, mashonanguo kidogo ki¬dogo au
mboga nyingme.
Tumia maziwa au krimu badala ya tui la nazi.
Weka nyama au dagaa au samaki au mayai badala ya - karanga.
No comments yet. Be the first to share your thoughts!