Ujumbe mzuri wa kumwambia mpenzi wako kuwa yeye tuu mdiye kakutawala
Updated at: 2024-05-25 15:36:48 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu.
Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
SMS ya kimahaba kumueleza mpenzi wako maana ya mapenzi, Mapenzi ni nini?
Updated at: 2024-05-25 15:26:43 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mapenzi ni nini? Wale wasiopenda huita majukumu, wale wanaoyachezea huita mchezo, wale wasiokuwa nayo huita ndoto, na wale wanaoelewa huyaita mwisho wa safari, na mimi, mwisho wangu ni wewe.
SMS ya kumdekeza mpenzi wako na kumwambia unavyompenda
Updated at: 2024-05-25 15:24:50 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
mapenzi ni utoto,deka ulie nitakubembeleza,mapenzi ni zawadi tabasamu nibusu niambie kiasi gani unanpenda,naweza kusema asilimia kubwa jina lako limezunguka kuta wa moyo wangu.kamwe jina lako haliwezi kufutika.nakupenda sana.
Updated at: 2024-05-25 15:36:10 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako, naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA