Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mackerel 2 Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha cha kula Pilipili iliyo katwakatwa (chopped scotch bonnet ) 1/2 Limao (lemon) 1/2 Chumvi (salt) kiasi Curry powder 1/2 kijiko cha chai Coriander powder 1/2 kijiko cha chai Mafuta 1 kijiko cha chai
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakaushe maji ( ukipenda unaweza kuwakata kati au ukawapika wazima) Baada ya hapo wakate mistari kila upande ( ili spaces ziweze kuingia ndani) kisha waweke kwenye bakuli na utie spice zote. Wachanganye vizuri kisha waweke frijini na uwaache wamarinate kwa muda wa masaa 3. Baada ya hapo washa oven kisha wapakaze mafuta na uwafunge kwenye foil na uwatie kwenye oven kwa muda wa dakika 20. Baada ya hapo fungua foil na uwaache kwenye oven kwa muda wa dakika 10 ili wapate kukauka kidogo. Na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuwala kwa kitu chochote upendacho.
Updated at: 2024-05-25 10:34:43 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga ngano vikombc 3 Unga mbegu za mchicha kikombe 1 Baking powder vijiko vidogo Maziwa kikombe 1 Sukari kikombe 1 Blue band kikombe Β½ Mayai 10-12
Hatua
β’ Chagua, osha, kausha mbegu za mchicha mweupe, kisha saga zilainike. β’ Chekecha unga wa ngano, unga wa mbegu za mchicha na baking powder Kwenye bakuli kubwa. β’ Ongeza sukari na changanya. β’ Ongeza mayai kidogo, kidogo ukikoroga na mwiko kwenda njia moja mpaka ilainike. β’ Kama rojo ni zito ongeza mayai, au maziwa ili iwe laini, ongeza vanilla na koroga. β’ Paka mafuta kwenye chombo cha kuoka au sufuria na chekechea unga kidogo. β’ Mimina rojo ya keki na oka kwenye oveni au kama ni sufuria funika, weka moto mwingi juu, chini weka moto kidogo. β’ Ukinusia harufu nzuri ya vanilla, funua, choma kisu katikati ya keki, kama ni kavu epua, pozesha na pakua kama kitafunio.
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Tambi za mayai ni moja kati ya vyakula ambavyo napenda kuandaa pale ninapokua ninaharaka au sina muda mrefu wakukaa jikoni.pishi hili huchukuca muda mfupi sana na nimlo uliokamilika.
Mahitaji
Tambi Β½ paketi
Vitunguu maji 2 vikubwa
Karoti 1
Hoho 1
Vitunguu swaumu(kata vipande vidogo) kijiko 1 cha chakula
Carry powder kijiko 1 cha chai
Njegere zilizochemshwa Β½ kikombe
Mafuta kwa kiasi upendacho
Mayai 2
Chumvi kwa ladha upendayo
Njia
1.Chemsha maji yamoto yanayotokota,ongeza chumvi na mafuta kidogo,weka tambi kwenye maji hayo chemsha adi ziive.Chuja maji yote ili kupata tambi kavu 2.Katika bakuli piga mayai kisha weka pembeni 3.Katika kikaango,weka mafuta,vitunguu maji ,vitunguu swaumu,hoho, karoti na carry powder,kaanga kwa pamoja katika moto mdogo kwa muda mfupi kwani mboga hazitakiwi kuiva. 4.Ongeza tambi na njegere katika kikaango,geuza kila mara ili kuchanganya . 5.Ongeza mayai kwenye tambi kisha geuza kwa haraka bila kupumzika adi mayai yaive na tambi ziwe kavu.Tayari kwa kula
Katika hatua hii ongeza moto uwe wa wastani,moto ukiwa mdogo mayai yatafanya tambi zishikane na kufanya mabonge.
Updated at: 2024-05-25 10:37:37 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Boga la kiasi - nusu yake
Tui zito la nazi 1 Β½ gilasi
Sukari Β½ kikombe
Hiliki Β½ kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Menya boga kisha katakata vipande vya kiasi. Weka katika sufuri tia maji kiasi ya kuchemshia na kuwiva bila ya kubakia maji mengi. Changanya tui na sukari na hiliki kisha mimina juu ya boga wacha katika moto dakika chache tu bila ya kufunika. Epua mimina katika chombo likiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:34:48 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Matunda ni mojawapo wa kundi la vyakula, ni muhimu sana kwa afya bora. Matunda yakitengenezwa vizuri yanavutia sana na yanakuwa ni chakula kizuri sana.
Mahitaji
Embe iliyoiva kiasi Nanasi Tango Tikiti maji Zabibu Papai
Matayarisho
1. Ondoa maganda kwenye embe, nanasi, tango, papai na tikiti maji kisha kata kata vipande vidogo vidogo vya mraba
2. Changanya vipande vya matunda kwenye bakuli safikisha weka na zabibu zilizotolewa kwenye kikonyo chake.
3. Weka kwenye friji yapate ubaridi kidogo
4. Saladi yako tayari kwa kuliwa
Waweza kula saladi hii kama mlo wa kati au kama mlo kamili wa usiku.
2. Unaweza kutwanga kwa kutumia kinu au kuchemsha kidogo na kisha kusaga kwa kutumia mashine. Ukitumia mashine uwe makini usije ukasaga sana ukaharibu.
3. Kaanga karanga kidogo na kisha zisage ziwe unga unga.
4. Chemsha kisamvu chako hadi kiive.
5. Katakata kitunguu, karoti na na nyanya
6. Anza kuunga kisamvu kwa kukaanga vitunguu, weka karoti na kisha nyanya na vikishaiva weka kisamvu na koroga pamoja kisha weka karanga. Acha vichemke kwa muda na unaweza pia weka na nazi tui la kwanza.
7. Baada ya muda mfupi epua na kitakiwa tayari. Waweza kula kwa ugali, wali, chapati, makande n.k
Mapishi ya Wali Mweupe Kwa Mchuzi Wa Kuku Wa Balti
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Kuku 1 mkate vipande vipande
Vitunguu 3 katakata (chopped)
Nyanya 5 zikatekate (chopped)
Tangawizi mbichi ilokunwa au ilosagwa 1 kijiko cha kulia
Thomu (kitunguu saumu) kilosagwa kijiko 1 cha kulia
Bizari mchanganyiko (garam masala) kijiko 1 cha chai
Jira/bizari ya pilau (cummin powder) kijiko 1 cha chai
Dania/gilgilani ilosagwa (coriander powder) kijiko 1 cha chai
Mtindi/maziwa lala (yoghurt) vijiko vya kulia 4 mjazo au paketi moja ndogo.
Malai ya kupikia (cooking cream) kikombe 1
Kasuri methi (majani makavu ya uwatu/dried fenugreek leaves) 1 kijiko cha kulia
Mafuta ya kupikia Β½ kikombe
Chumvi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha kuku vizuri mwache achuje maji. Weka mafuta katika sufuria kaanga vitunguu mpaka vianze kugeuka rangi ya brown hafifu. Kisha tia tangawizi na thomu ukaange. Tia kuku ukaange mpaka ageuke mweupe kisha tia nyanya endelea kukaanga ziwive. Piga mtindi vizuri katika kibakuli uwe nyororo. Epua sufuria weka kando kisha tia mtindi uchanganye vizuri pamoja na kuku. Rudisha katika moto acha uchanganyike na kuku kidogo kisha mwagia malai ya kupikia (cooking cream) Tia kasuri methi/majani makavu ya uwatu yaliyovurugwa. Acha katika moto dakika 1 tu. Epua umimine katika chombo na nyunyizia ikiwa tayari kuliwa na wali mweupe.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kidali cha kuku 1 kikubwa Swaum,tangawizi 1 kijiko cha chai Limao 1/2 Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai Curry powder 1/2 kijiko Paprika 1/2 kijiko cha chai Hoho jekundu 1/2 Hoho la njano 1/2 Kitunguu 1/2 Chumvi Olive oil
Matayarisho
Katakata kuku ktk vipande vya mishkaki ya kawaida kisha vimarinate na vitu vyote, kasoro hoho na kitunguu.Ni vizuri kuziacha either usiku mzima au kwa masaa machache ili spice ziingie vizuri. Baada ya hapo katakata hoho na vitunguu vipande vya wastani kiasi. Baada ya hapo Taarisha vijiti vya mishkaki kisha tunga nyama pamoja na hoho na vitunguu kisha nyunyuzia mafuta na kisha uzichome kama mishkaki ya kawaida. Itakapoiva itakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama ndizi za kuchoma, viazi na n.k.
Updated at: 2024-05-25 10:22:24 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga π₯π«
Kama unapenda kufurahia vitafunio na unakabiliwa na mzio wa karanga, basi hii ni makala sahihi kwako! Leo, kama AckySHINE, ningependa kushiriki nawe vidokezo 10 vya vitafunio visivyo na karanga ambavyo utaweza kufurahia bila wasiwasi wowote. Tuko pamoja kwenye safari hii ya kufurahia vitafunio bila kujali msongamano wa mzio. Hebu tuanze! πͺπ
π Matunda yaliyokaushwa: Matunda yakiwa yamekaushwa ni chaguo bora la vitafunio vya afya. Unaweza kuchagua matunda kama tini, zabibu, na apple zilizokaushwa. Ni vitafunio vya asili na vyenye ladha tamu na bora.
π₯ Mboga mboga za chumvi: Badala ya vitafunio vyenye mafuta mengi, jaribu mboga mboga za chumvi kama vile karoti, matango, na pilipili mboga. Ni vitafunio vya chini katika kalori na vyenye virutubisho vingi muhimu kwa afya yako.
πΏ Popcorn: Ni vitafunio maarufu sana na vinapatikana kwa urahisi. Unaweza kununua popcorn zilizopikwa tayari au kutengeneza mwenyewe nyumbani. Kumbuka kutumia mafuta ya kupikia ya afya kama vile mafuta ya mzeituni au ya alizeti.
π Ndizi: Ndizi ni vitafunio vyenye ladha tamu na vinafaida nyingi za kiafya. Unaweza kuchukua ndizi kama vitafunio vyako vya asubuhi au jioni. Pia, unaweza kujaribu kuongeza chaguzi zingine kama ndizi iliyochomwa au ndizi iliyokatwa na kuongeza juisi ya limao juu yake.
π₯ Mayai: Mayai ni chaguo bora la vitafunio visivyo na karanga. Unaweza kuwapika kukawa mayai ya kuchemsha au kukaanga. Pia, unaweza kuchanganya mayai na mboga mboga kama vitafunio vya kuchoma kwa afya.
π₯¨ Mikate ya kusaga: Mikate ya kusaga ni chaguo bora la vitafunio vinavyotumika kila wakati. Unaweza kupaka jibini ya cheddar au mchuzi wa nyanya juu yake. Ni vitafunio vyenye ladha tamu na rahisi kubeba popote uendapo.
π₯¦ Korosho: Korosho ni vitafunio vingine vyenye ladha nzuri na vinafaida nyingi za kiafya. Unaweza kuchagua korosho zisizosindikwa au zilizopikwa kwa mafuta kidogo. Ni chaguo nzuri la vitafunio vya kati na vyenye chumvi kidogo.
π Kabeji za kukaanga: Kabeji za kukaanga ni chaguo bora la vitafunio vya afya. Unaweza kukata kabeji vipande vidogo na kuzikaanga kwenye mafuta kidogo. Kabeji ina kiwango kidogo cha kalori na ina virutubisho vingi muhimu kwa afya yako.
π Embe: Tunda hili tamu linapatikana kwa urahisi na ni chaguo nzuri la vitafunio visivyo na karanga. Unaweza kula embe kama vitafunio vyako pekee au kuchanganya na matunda mengine katika smoothie ya asubuhi.
πͺ Biskuti visivyo na karanga: Soko limejaa biskuti zilizotengenezwa kwa ajili ya watu wenye mzio wa karanga. Unaweza kujaribu biskuti zilizotengenezwa kwa kutumia mafuta ya alizeti au mafuta ya kokoa badala ya mafuta ya karanga. Ni vitafunio vya afya na vyenye ladha nzuri.
Kwa hiyo, kama AckySHINE, napenda kukuhimiza kufurahia vitafunio bila wasiwasi wa mzio wa karanga. Kuna chaguzi nyingi nzuri huko nje ambazo utaweza kufurahia bila wasiwasi wowote. Kumbuka daima kusoma maelezo ya viungo kabla ya kununua vitafunio ili kuhakikisha hakuna karanga yoyote iliyomo.
Je, wewe ni mpenzi wa vitafunio? Ni vitafunio gani visivyo na karanga unapenda? π
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Miguu ya kuku (chicken legs) 10 Kitunguu swaum na tangawizi (ginger & garlic paste) 1 kijiko cha chakula Limao (lemon) 1 Pilipili iliyosagwa (ground scotch bonnet) 1/2 Giligilani iliyokatwakatwa (chopped coriander) kiasi Chumvi (salt) kiasi Mafuta ya kukaangia (veg oil)
Matayarisho
Safisha kuku kisha mtie kwenye sufuria na viungo vyote (kasoro mafuta na giligilani) kisha mchemshe mpaka aive na umkaushe supu yote. Baada ya hapo mkaange katika mafuta mpaka awe wa brown kisha mtoe na uweke katika kitchen towel ili kuchuja mafuta. Baada ya hapo weka katika sahani na umwagie giligilani kwa juu. Na hapo kuku wako atakuwa tayari kwa kuliwa.