Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe tegemeo langu na tumaini langu dhabiti. Ndiwe mwenye dawa ya maovu yangu yote, malipizi ya makosa yangu yote. Waweza kunipatia haja zangu na neema ninazoziomba mimi na wengine. Wewe uko ili kutusaidia sote, ndiwe mwanga mkuu usiozimika, ndiwe chanzo cha nguvu, uvumilivu, amani na faraja. Nina hakika kuwa maombi yangu hayatakuchosha, nawe hutaacha kunisaidia, kunilinda, kunipenda, kwani, ee Moyo Mtakatifu , upendo wako hauna mwisho. Ee Moyo Mtakatifu, unihurumie, kwa ajili ya maombi yangu, kadiri ya huruma yako. Nawe katika sisi, na kwa ajili yetu, ufanye lolote unalolihitaji, kwani tunajitoa kwako kwa imani na uhakika thabiti kwamba kamwe hautatuacha, kwa milele. Amina.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI
Majitoleo kwa Bikira Maria
SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU
SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU
Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania
KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU
Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema
SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE