Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Madhara yatokanayo na ukeketaji

Featured Image
Ukeketaji au tohara ya wanawake ni hatari sana kwa msichana
anayetahiriwa. Wasichana hufa kutokana na madhara yake
makubwa zaidi kwa vile:

  • Hutokwa na damu nyingi.

  • Uambukizo unatokea iwapo vifaa vilivyotumiwa

  • havikuwa safi. Uambukizo unaweza kuenea mpaka katika


viungo vya ndani vya uzazi na kusababisha ugumba na
hata vifo.

  • Hatari ya kuambukizwa Virusi vya UKIMWI wakati wa


ukeketaji.

  • Kuziba kwa mkojo na damu ya mwezi (hedhi) ndani ya


mwili wa mwanamke na kusababisha uambukizo.

  • Matatizo na maumivu makali wakati wa kujamiiana na


wakati wa kujifungua kutokana na kupungua ukubwa wa
uke. Ukeketaji wa wanawake mara nyingi una madhara
ya kisaikologia ambapo wasichana hupoteza tumaini
na imani kwa walezi au wazazi na wanaweza wakapata
mateso ya kujisikia waoga, kufadhaika, kutojiweza na
kutokuwa kamilifu kimwili.

Zaidi ya hayo, ukeketaji unampunguzia mwanamke hamu ya
kujamiiana. Kufanikisha hamu ya ngono inategemea kwa kiasi
kikubwa viungo vya uzazi vya nje. Ukeketaji hata hivyo unaharibu
umbile na kazi za viungo vya uzazi vya nje vya mwanamke.
Ina madhara kimwili na kisaikologia ambapo mara nyingi
huleta matatizo ya mahusiano ya kimwili kati ya mwanamume
na mwanamke. Kisimi ni sehemu ya mwili wa msichana chenye
ashiki na hisia kali ya viungo vya uzazi. Kinasisimua ashiki kwa
mwanamke anaposhikwa. Sehemu ya ndani ya mashavu na kisimi
kwa kiasi kikubwa vinahusika na hali kiwango cha raha ya na
kufikia mshindo wakati wa kujamiiana. Wakati kisimi na viungo
vingine vya uzazi vimeondolewa, ashiki na raha hupungua kwa
kiasi kikubwa. Endapo mwanamke amekatwa vibaya sana au uke
umeshonwa, kuna uwezekano wa kupata maumivu na matatizo
wakati wa kujamiiana na wa kujifungua.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Hatua gani zichukuliwe dhidi ya wanaowakeketa au kuwachezea unyago Albino juani?

Hatua gani zichukuliwe dhidi ya wanaowakeketa au kuwachezea unyago Albino juani?

Swali hili linaonyesha mambo mawili ambayo ni mabaya. Jambo
la kwanza ni ukeketaji ambao ni ... Read More

Je, watu wanapendelea kujaribu njia za kuleta msisimko wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kujaribu njia za kuleta msisimko wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Karibu sana kwenye makala hii ya blog, ambapo tutajadili kuhusu kwa nini watu wanapendelea kutafu... Read More

Kuna fikra kuwa Albino ni watu wa kawaida je, kisayansi hii ni kweli?

Kuna fikra kuwa Albino ni watu wa kawaida je, kisayansi hii ni kweli?

Hii ni kweli kabisa. Watu wanaoishi na ualbino ni watu wa
kawaida kama binadamu wengine wote... Read More

Kumaliza ashiki au hamu ya kufanya mapenzi

Kumaliza ashiki au hamu ya kufanya mapenzi

Kwa vijana mara nyingine siyo rahisi kufahamu afanye nini mara anapopata ashiki (hamu) ya kutaka ... Read More

Ni umri gani ambapo vijana wanapaswa kuelezwa juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango?

Ni umri gani ambapo vijana wanapaswa kuelezwa juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango?

Vijana balehe wote wana haki ya kupata habari juu ya mambo yote
wanayoyapenda. Watoto wanavy... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Kama kijana, kuna wakati unaweza kukutana na msichana na unataka kuzungumza naye kwa kina lakini ... Read More

Je, Ni Vipi Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono?

Je, Ni Vipi Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono?

Je, ni vipi kuepuka shinikizo la kufanya ngono? Hii ni swali ambalo vijana wengi hujikuta wakijiu... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Uoga kabla ya Kufanya Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Uoga kabla ya Kufanya Ngono?

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Uoga Kabla ya Kufanya Ngono 🌟

Karibu kwenye makala hii... Read More

Kwa nini mara nyingi mvulana ni mwepesi sana katika kuanzisha kufanya mapenzi? Na kwa nini mwanaume mara nyingi anafikia mshindo kabla ya mwanamke? Mwanaume anawahi kufika kileleni kwa nini?

Kwa nini mara nyingi mvulana ni mwepesi sana katika kuanzisha kufanya mapenzi? Na kwa nini mwanaume mara nyingi anafikia mshindo kabla ya mwanamke? Mwanaume anawahi kufika kileleni kwa nini?

Kwa kawaida i inakubalika kuwa wavulana ndiyo waaanze kuonyesha ishara za kujamiaana na tafiti zi... Read More

Kwa nini mara nyingine uume hausimami?

Kwa nini mara nyingine uume hausimami?

Ili mwanaume aweze kujamii ana, ni lazima uume usimame na kuweza kupenya ukeni. Kama mvulana anasisi... Read More
Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Hapana, huwezi ukarithi uvutaji wa bangi. Lakini mara nyingi watoto huiga tabia za wazazi wao. Wa... Read More

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mape... Read More