Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Mapishi ya Biriyani Ya Kuku

Featured Image

Vipimo

Mrowanishe kuku na viungo hivi kwa muda mdogo tu

Kuku (Mkate kate Vipande) - 4 LB

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 Vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Pilipili nyekundu ya unga - 1 Kijiko cha supu

Bizari ya manjano (Haldi au Tumeric) - 1 Kijiko cha chai

Bizari ya pilau ya powder (Jeera) - 1 Kijiko cha chai

Gilgilani powder (Dania) - 1 Kijiko cha chai

Ndimu - 1 Kijiko cha supu

Mchele na vitu vya Masala:

Mchele (Basmati mzuri) (rowanisha) - 7 cups

Mafuta ya kupikia - kiasi

Vitunguu Vilivyokatwa - 8

Nyanya iliyokatwa katwa - 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 1 Kijiko cha supu

Garam Masala -1 Kijiko cha supu

Hiliki powder - ½ Kijiko cha chai

Tomatoe paste - 1 Kijiko cha supu

Pilipili mbichi zipasue katikati - 4

Chumvi - kiasi

Mtindi - 4 Vijiko vya supu

Kotmiri iliokatwa (Chopped) - ½ Kikombe

Mafuta ya kunyunyuzia katika wali - 3 Vijiko vya supu

Zaafarani au rangi ya biriani - kiasi

Namna Ya Kutaarisha Na Kupika

Weka kuku aliyerowanishwa na viungo vyake katika Foil tray au chombo chocote utakachomwagia wali humo humo na kupikia biriani, kisha mchome (Bake) mpaka awive na awe mkavu kiasi.

Wakati kuku anapikika, kaanga vitunguu katika karai au sufuria mpaka viwe brown na epua nusu yake weka kando.

Punguza mafuta yabakie kiasi tu, ongeza Thomu na tangawizi, na viungo vyote vya hapo juu isipokuwa Mtindi na kotmiri, endelea kukaanga hadi tomatoe zilainike.

Ongeza chumvi, malizia mwisho kwa kutia mtindi, kotmiri na vile vitunguu ulivyoweka kando. Masala yako tayari.

Mwagia masala juu ya kuku uliyekwishmpika changanya vizuri.

Chemsha Mchele uwive nusu, chuja na mwagia juu ya masala.

Nyunyiza mafuta kidogo juu ya mchele na zaafarani au rangi ya biriani.

Bake katika moto wa 350 – 400 kwa muda wa 15 – 20 minutes. Biriyani imekuwa tayari kuliwa.

Mtindi wa kutolea Biriyani:

Mtindi - 1 kikombe

Pilipili mbichi - 1 ndogo

Kitunguu saumu(/galic) thomu - chembe mbili

Nanaa - kiasi

Chumvi - chembe tu

Weka kwenye Blender na uchanganye, kisha mimina katika bakuli

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon

Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon

Vipimo

Mchele vikombe 3

Karoti 1 ikune (grate)

Mchicha katakata kiasi

A... Read More

Mapishi ya mboga mchanganyiko

Mapishi ya mboga mchanganyiko

Mahitaji

Viazi ulaya 4 vya wastani
Hoho jekundu 1/2
Hoho la njano 1/2
Hoho... Read More

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Viazi - 4

Vitunguu - 2... Read More

Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)

Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)

Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi i... Read More

Jinsi ya kutengeneza Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

Jinsi ya kutengeneza Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe vya chai

Siagi - 1 Kikombe cha chai

Hiliki ½ K... Read More

Jinsi ya kupika Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Jinsi ya kupika Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Viamba upishi

Unga 1 Magi (vikombe vya chai)

Sukari ya browni ½ Magi

Siagi i... Read More

Mapishi ya Ndizi mzuzu

Mapishi ya Ndizi mzuzu

Mahitaji

Ndizi tamu (plantain) 3-4
Tui la nazi (coconut milk) kikombe 1 cha chai
Read More

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 3)
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Viazi mbatata... Read More

Mapishi ya visheti vitamu

Mapishi ya visheti vitamu

VIAMBAUPISHI

Unga - Vikombe 2

Samli au shortening ya mboga - 2 Vijiko vya supu

<... Read More
Upishi na Mafuta ya Zeituni: Faida za Afya na Matumizi ya Mapishi

Upishi na Mafuta ya Zeituni: Faida za Afya na Matumizi ya Mapishi

Upishi na Mafuta ya Zeituni: Faida za Afya na Matumizi ya Mapishi 🍽️

Karibu katika ma... Read More

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - ... Read More

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Mahitaji

Nyama Ya Mbuzi - 1 Kilo

Mchele - 4 Magi

Vitunguu - 3

Nyanya - ... Read More