Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Featured Image

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya warithi wa Mitume; Bwana, uwape wawe na uangalifu uliojaa upendo kwa mapadre wao
Kwa ajili ya Maaskofu wako waliochaguliwa na Roho Mtakatifu; Bwana, uwabakishe karibu na kondoo wako
Kwa ajili ya wachungaji wako; Bwana, uwafundishe kutumikia kuliko kutafuta kutumikiwa
Kwa ajili ya waungamishi na washauri wa kiroho; Bwana, uwafanye kuwa vyombo visikivu kwa Roho wako Mtakatifu
Kwa ajili ya mapadre wanaotangaza neno lako; Bwana, uwawezeshe kushirikisha Roho wako na Uzima wako
Kwa ajili ya mapadre wanaosaidia utume wa walei; Bwana, uwatie moyo wa kuwa mifano bora
Kwa ajili ya mapadre wanaofanya kazi na vijana; Bwana, uwajalie wawakabidhi vijana kwako
Kwa ajili ya mapadre wanaofanya kazi kati ya watu fukara; Bwana, uwajalie wakuone na wakutumikie kupitia hao
Kwa ajili ya mapadre wanaoangalia wagonjwa; Bwana, uwajalie wawafundishe thamani ya mateso
Kwa ajili ya mapadre fukara; - Uwasaidie ee Bwana
Kwa ajili ya mapade wagonjwa; - Uwaponye ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wazee; - Uwapatie tumaini la raha ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye huzuni na walioumizwa; -Uwafariji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaohangaishwa na wale wanaosumbuliwa; - Uwape amani yako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaodharauliwa na wanaonyanyaswa; - Uwatetee ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; - Uwatie moyo ee Bwana
Kwa ajili ya wale wanaosomea upadre; - Uwape udumifu ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; - Uwape uaminifu kwako na kwa Kanisa lako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; - Uwajalie utii na upendo kwa Baba Mtakatifu na kwa maaskofu wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; - Uwajalie waishi katika umoja na maaskofu wao ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; - Wawe wamoja kama Wewe na Baba mlivyo wamoja ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; - Waishi na kuendeleza haki yako ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; - Washirikiane katika umoja wa ukuhani wako ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote, wakiwa wamejawa na uwepo wako; - Waishi maisha yao ya useja kwa furaha ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; - Wajalie ukamilifu wa Roho wako na uwageuze wafanane nawe ee Bwana
Kwa namna ya pekee, ninawaombea mapadre wale ambao kwa njia yao nimepokea neema zako. Ninamwombea padre aliyenibatiza na wale walioniondolea dhambi zangu, wakinipatanisha na Wewe na Kanisa lako.
Ninawaombea mapadre ambao nimeshiriki Misa walizoadhimisha, na walionipa Mwili wako kama chakula. Ninawaombea mapadre walionishirikisha Neno lako, na wale walionisaidia na kuniongoza kwako. Amina.


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Diana Mallya (Guest) on June 5, 2017

Mungu akubariki!

Jane Muthui (Guest) on May 9, 2017

Mwamini katika mpango wake.

John Lissu (Guest) on April 29, 2017

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Simon Kiprono (Guest) on April 12, 2017

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Ann Wambui (Guest) on March 14, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Lucy Wangui (Guest) on November 17, 2016

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Jane Muthui (Guest) on October 29, 2016

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Samson Tibaijuka (Guest) on August 28, 2016

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Charles Mrope (Guest) on August 20, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Patrick Mutua (Guest) on August 6, 2016

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Lucy Mushi (Guest) on June 11, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Nancy Akumu (Guest) on May 1, 2016

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Peter Tibaijuka (Guest) on April 5, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Edward Chepkoech (Guest) on March 25, 2016

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Agnes Njeri (Guest) on February 25, 2016

Sifa kwa Bwana!

Lucy Kimotho (Guest) on January 29, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

John Mwangi (Guest) on January 10, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Francis Mrope (Guest) on December 28, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Mary Njeri (Guest) on July 25, 2015

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Frank Macha (Guest) on July 8, 2015

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Stephen Malecela (Guest) on May 20, 2015

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

James Malima (Guest) on April 11, 2015

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Edith Cherotich (Guest) on April 5, 2015

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Related Posts

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)

Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku ... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,... Read More

SALA YA MAPENDO

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu,

nakupenda zaidi ya cho chote,

kwani ndiwe mwema,

ndiwe mwenye kupe... Read More

SALA YA MTAKATIFU INYASI

SALA YA MTAKATIFU INYASI

Roho ya Kristo unitakase
Mwili wa Kristo uniokoe
Damu ya Kristo unifurahishe
Maji ... Read More

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye sik... Read More

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha ... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

Majitoleo kwa Bikira Maria

Majitoleo kwa Bikira Maria

(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na... Read More

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie B... Read More