Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Featured Image

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./





Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./





Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./





Moyo Mtakatifu wa Yesu,/ Rafiki mpenzi wa Yuda Tadei,/ nakutumainia./





(Mwisho Sali: Baba yetu (x3), Salamu Maria (x3) na Atukuzwe(x3).


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Victor Mwalimu (Guest) on July 13, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Anthony Kariuki (Guest) on June 30, 2017

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Daniel Obura (Guest) on June 6, 2017

Tumaini ni nanga ya roho

Esther Nyambura (Guest) on May 16, 2017

Baraka kwako na familia yako.

Joyce Mussa (Guest) on January 11, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Esther Nyambura (Guest) on December 4, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

Paul Kamau (Guest) on October 5, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Josephine Nekesa (Guest) on October 3, 2016

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Catherine Naliaka (Guest) on September 16, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Thomas Mtaki (Guest) on September 6, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Joyce Nkya (Guest) on June 17, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Sarah Mbise (Guest) on June 1, 2016

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

John Kamande (Guest) on April 19, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Peter Mbise (Guest) on April 6, 2016

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Anna Kibwana (Guest) on February 25, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Carol Nyakio (Guest) on February 16, 2016

Rehema hushinda hukumu

James Mduma (Guest) on February 10, 2016

Nguvu hutoka kwa Bwana

Grace Wairimu (Guest) on December 17, 2015

Mungu ni mwema, wakati wote!

Rose Amukowa (Guest) on November 27, 2015

Mwamini Bwana; anajua njia

Francis Njeru (Guest) on July 27, 2015

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Andrew Mchome (Guest) on July 18, 2015

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Philip Nyaga (Guest) on June 21, 2015

Endelea kuwa na imani!

Kenneth Murithi (Guest) on April 19, 2015

Rehema zake hudumu milele

Related Posts

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More