Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Featured Image

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida)

Mwanzo, kwenye Msalaba:

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

Kwenye chembe ndogo za awali:

K: Ee Mungu utuelekezee msaada W: Ee Bwana utusaidie hima
W: Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

KATIKA KILA FUNGU SALI SALA ZIFUATAZO:

Kwenye chembe kubwa:

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa, na siku zote, na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

Ee Maria Mama wa Msaada wa daima
Sikiliza maombi ya roho zetu
Unaweza kutusaidia katika mahitaji yetu
Ee Maria kwa matumaini twakuita wewe.

Kwenye chembe ndogo:

Kama unasali mwenyewe: β€œEe Maria, utusaidie! (mara kumi)
Kama mnasali zaidi ya mmoja kwa pamoja: K; Ee Maria, W: Utusaidie. (mara kumi)

MWISHO SALI SALA ZIFUATAZO:

Salamu Maria

Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa, na saa ya kufa kwetu. Amina. (mara tatu)

Tunaukimbilia

Tunaukimbilia ulinzi wako, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe siku zote, kila tuingiapo hatarini, ee Bikira Mtukufu na mwenye baraka,. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Agnes Lowassa (Guest) on September 20, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Anna Malela (Guest) on September 6, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

John Malisa (Guest) on August 23, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Sarah Karani (Guest) on August 19, 2017

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Anna Mahiga (Guest) on June 24, 2017

Neema na amani iwe nawe.

Richard Mulwa (Guest) on June 22, 2017

Imani inaweza kusogeza milima

Samuel Were (Guest) on March 25, 2017

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Victor Sokoine (Guest) on March 16, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

John Malisa (Guest) on January 3, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Edith Cherotich (Guest) on December 4, 2016

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Bernard Oduor (Guest) on December 4, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Moses Kipkemboi (Guest) on September 4, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Anna Mchome (Guest) on August 21, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Joseph Kitine (Guest) on August 19, 2016

Nakuombea πŸ™

Peter Mbise (Guest) on May 10, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Samuel Omondi (Guest) on February 26, 2016

Endelea kuwa na imani!

Alice Jebet (Guest) on January 16, 2016

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Diana Mallya (Guest) on December 31, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Robert Okello (Guest) on October 8, 2015

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

John Lissu (Guest) on July 31, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Catherine Mkumbo (Guest) on May 29, 2015

Neema ya Mungu inatosha kwako

Joseph Njoroge (Guest) on May 9, 2015

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Sarah Mbise (Guest) on April 17, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Related Posts

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makun... Read More

SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

Sala ya kuomba Kifo chema

Sala ya kuomba Kifo chema

Enyi Yesu na Maria na Yosefu,

nawatolea Moyo, na roho, na uzima wangu.

Enyi Yesu na M... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More